EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 28, 2014

BET AWARDS NI DIAMOND TENA KESHO


Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnumz’.
UMEKUCHA! Unaweza kusema kwa maana nyingine wakati wasanii kutoka Afrika watakapokuwa pamoja kwenye Ukumbi wa Nokia Theatre uliopo Los Angeles, Marekani katika sherehe za utoaji tuzo za BET 2014 kesho Juni 29.
Macho na masikio yote yameelekezwa kwa mtu mmoja kutoka Tanzania ambaye ni Nasibu Abdul ‘Diamond Plutnumz’.
Kupitia wimbo wa My Number One (Remix), aliomshirikisha staa kutoka pande za Nigeria, Davido, ndiyo uliompandisha chati za juu mpaka kufikia kujulikana kimataifa sambamba na kuingizwa katika tuzo mbalimbali za heshima.
Wapo wanaofurahia mafanikio yake na wengine kuchukia na kuona kama anapendelewa.
Katika makala haya yanachambua safari nzima za tuzo ambazo ameshashiriki na anazoendelea kushiriki kwa sasa;
Awashangaza Watanzania
Aliivunja rekodi iliyokuwa ikishikiliwa na mwanamuziki Abass Hamis Kinzasa ‘20%’,  ya mwaka 2011 ambayo alijinyakulia tuzo tano kwa mpigo zilizotambulika kama Kilimanjaro Music Awards 2011.
Katika tuzo za Kilimanjaro za mwaka 2014 zilizofanyika Mlimani City jijini Dar, Diamond aliondoka shujaa kwa kujizolea tuzo saba kwa mpigo na kuweka rekodi ya aina yake huku maswali mengi yakibaki midomoni mwa watu na hata wengine wakidhani amebebwa na hakustahili kupewa tuzo hizo zote.
Atemwa tuzo za MTV MAMA 2014
Mpaka Diamond anaelekea Afrika Kusini Juni 7 mwaka huu, alionekana kama msanii anayeongoza kwa kupigiwa kura nyingi na mashabiki akiwa na asilimia zaidi ya 60. Watanzania wengi walijua ataibuka kidedea.
Wakati wa ufunguzi wa tuzo hizo alianza kwa kufanya shoo ya nguvu akiwa sambamba na mwanamuziki kutoka Nigeria, Davido. Walilivaa jukwaa na wimbo wa My Number One Remix.

Hata wale ambao hawakujua lugha ya Kiswahili aliyokuwa akiimba Diamond katika wimbo huo walionekana kumfurahia kwa kucheza naye pamoja.
Kilichokuja kufanyika wakati wa utoaji wa tuzo hizo, Diamond hakuambulia kitu chochote. Tuzo zilimpita machoni na kukimbilia kwa wasanii kama Davido, Tiwa Savage, Uhuru pamoja na Mafikizolo.

Atatoka katika tuzo za BET 2014?
Habari kila kona ni siku ya kesho Juni 29, katika utoaji tuzo za BET 2014 ambapo Diamond ameingia katika kategori ya Mwanamuziki Bora wa Kimataifa kutoka Afrika akiwa sambamba na Sarkodie (Ghana), Mafikizolo (Afrika Kusini), Davido (Nigeria), Toofan (Togo) na Tiwa Savage (Nigeria) ambao wote kwa pamoja wameshaning’iniza kwapani tuzo za MTV Afrika 2014 na za BET 2012 kasoro Diamond kutoka Tanzania.
Abaniwa kupafomu
Swali gumu la kujiuliza ni jinsi mpangilio mzima uliopangwa na waandaaji wa tuzo za BET 2014 zitakazofanyika kesho.
Wakati wale waandaaji wa MTV Afrika 2014 walimpa Diamond nafasi ya kupafomu wimbo wake kwa kushirikiana na Davido, mambo yamekuwa tofauti kwa BET 2014.
Wamewakusanya wasanii wengi kutoka Nigeria mbaya zaidi ni wale wanaoshirikiana naye katika kugombea tuzo hizo ambapo kesho watapanda jukwaani kwa pamoja na kuimba wimbo maalum unaohusu Afrika.
Wasanii hao ni pamoja na Sarkodie kutoka Ghana, Mafikizolo kutoka Afrika Kusini, Tiwa Savage na Davido wote kutoka Nigeria.

Abakiza tuzo mbili tu
Bado anayo nafasi kubwa ya kusonga mbele na kugombea tuzo mbalimbali za kimataifa hata kama katika tuzo za BET atazikosa kesho. Mpaka sasa amebakiza tuzo mbili ambazo ni AFRIMMA 2014 na zile za KORA Africa 2014.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate