INAWEZEKANA usiamini kilichotokea, hiyo ni kama hukupata nafasi ya kuuona mchezo kati ya Hispania ambao ni mabingwa watetezi wa Kombe la Dunia, dhidi ya Uholanzi, jana, ambapo mabingwa hao walipata kipigo kikali na cha aibu.
Robin van Persie alifunga bao zuri la kichwa cha umbali wa mita 30 na kuisawazisha Uholanzi dakika ya 41 ya kipindi cha kwanza.
Uholanzi ikicheza kwa kujiamini, kushambulia na mpira wa kasi
ilifanikiwa kuifunga Hispania mabao 5-1 katika mechi ya Kundi B kwenye
michuano ya Kombe la Dunia ndani ya Dimba la Nova.Hispania ndiyo iliyoanza kufungua ukurasa wa mabao kwa kufunga katika dakika ya 27 kupitia kwa Xabi Alonso kwa penalti iliyotokana na straika wa Hispania, Diego Costa kuangushwa ndani ya eneo la hatari.
Uholanzi ilisawazisha bao hilo katika dakika ya 44 kupitia kwa Robin van Persie ambaye alifunga bao kali kwa kichwa huku akimuacha kipa wa Hispania, Iker Casillas akiwa hana la kufanya.
Mwanaume kazini.
Mabao matatu yaliyopatikana katika dakika ya 53 kupitia kwa Arjen
Robben, Stefan de Vrij dakika ya 64, van Persie tena katika dakika ya 73
ambapo bao hilo lilitokana na uzembe wa Cassillas ambaye alishindwa
kuucheza mpira aliorudishiwa, Robben tena dakika ya 80 yalitosha
kuwamaliza nguvu Hispania, ndipo wakakubali kipigo hicho mpaka mwisho wa
mchezo.
Robin
van Persie akimlamba chenga kipa wa Hispania, Iker Casillas kabla ya
kuifungia Uholanzi bao la nne katika ushindi wa 5-1 kwenye mechi ya
Kundi B Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil.
Cameroon Vs MexicoMexico ambayo ilikuwa na staa wa Manchester United, Javier Hernandez ‘Chicharito’ ilipata bao lake pekee kupitia kwa Oribe Peralta ambaye alimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Giovani dos Santos katika dakika ya 61.
Dos Santos alipiga shuti kali baada ya kuwatoka mabeki wa Cameroon iliyokuwa ikiongozwa na straika mkongwe wa Chelsea, Samuel Eto’o, ambapo kipa Charles Itandje akalipangua, ndipo Peralta akamalizia.
No comments:
Post a Comment