EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 18, 2014

VIFO MFULULIZO... MASTAA WAOMBEWA KANISANI

VIFO mfululizo vya mastaa wa filamu za Kibongo vinaumiza, vinatisha na vinawanyima usingizi wasanii ambapo sasa wameamua kuitikia wito na kuingia kanisani kuombewa, Risasi Mchanganyiko lina mkoba wenye kila kitu.
...Maombi mazito yakifanyika kwa Dotnata kutoka kwa Mchungaji Mbeyela. 
Wasanii waliotangulia mbele za haki kwa kufuatana ni Adam Kuambiana, Sheila Leo Haule ‘Recho’, George Otieno ‘Tyson’ na Said Ngamba ‘Mzee Small’.

Misiba hiyo imetokea ikiwa ni baada ya utabiri wa mtabiri maarufu Bongo, Maalim Hassan Hussein Yahya ambaye aliwatabiria vifo wasanii katika kipindi cha mwaka mmoja wa utabiri.
Mwakifwamba akiwa katika maombi
MASTAA KANISANI
Dawati la Risasi Mchanganyiko lilinasa habari kutoka katika chanzo chake, kilichoeleza kuwa Kanisa la Nchi ya Ahadi lilipanga kufanya maombi maalum, Jumapili ya Juni 15, mwaka huu kwa wasanii wa filamu Bongo kwa lengo la kuangamiza roho wa mauti anayekatisha ndoto zao.
Mchungaji Mbeyela akimwekea mkono Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba.
Pekupeku za gazeti hili zilionyesha kuwa, uongozi wa kanisa hilo ulisambaza ujumbe kwa wasanii mbalimbali wa filamu Bongo ukiwataka wafike kanisani hapo bila kukosa kwa ajili ya maombi.
“Wametoa tangazo hadi redioni, wamesisitiza wasanii waende kwa wingi ili wakaombewe. Wachungaji wa hilo kanisa wapo kwenye funga na maombi kwa ajili ya mambo mbalimbali yanayohusu nchi ikiwemo misiba ya wasanii wa filamu ambayo inatishia kiukweli,” kilisema chanzo hicho.
MAPAPARAZI KANISANI
Timu ya gazeti hili ikiambatana na wenzao wa Global TV walitinga kanisani hapo Jumapili iliyopita mishale ya saa tano asubuhi ambapo ilikuta kanisa likiwa limefurika waumini na baadhi ya wasanii wa filamu huku wengi wakiwa ni wale wanaochipukia.
...Simon Mwakifwamba na Illuminata Posh ‘Dotnatha’ wakiwa wamezama katika maombi mazito.
MWAKIFWAMBA, DOTNATHA WAWEKEWA MIKONO
Katika hali ya kushangaza sana, mastaa waliohudhuria walikuwa wawili tu; Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania ‘TAFF’, Simon Mwakifwamba na Illuminata Posh ‘Dotnatha’ ambao waliwekewa mikono na wachungaji waliokuwepo kwenye ibada hiyo.
Baadhi ya wachungaji waliowaombea mastaa hao ni Mchungaji Harris Kapiga na Mchungaji Mbeyela ambaye ni mume wa mwimbaji wa muziki wa Injili nchini, Upendo Nkone.
MCHUNGAJI ANENA
Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo, Harris Kapiga akizungumza na waandishi wetu baada ya ibada hiyo ya kuharibu roho wa mauti alisema, wasanii ni nembo ya taifa ndiyo maana wameona ni vyema kupambana na roho wa giza anayesababisha vifo miongoni mwao.
...Maombi ya nguvu yakiporomoshwa na mke wa Mchungaji kiongozi Harris Kapiga.
“Roho wa kifo ni kitu kamili. Anaishi katika ulimwengu wa giza, dawa yake ni maombi tu. Sisi kama kanisa tumeona ni vizuri kumlilia Mungu kwa ajili ya wasanii wetu, kwa maombi tuliyofanya, hakuna msanii mwingine atakayekufa katika kipindi hiki,” alisema Mchungaji Kapiga na kuongeza:
“Hatujali uchache wao, lakini tunaamini kuwa huko walipo watapokea uponyaji. Yaani hata kama kusingekuwepo na msanii yeyote, ibada ingeendelea kama kawaida. Kwa sasa nasema, wasanii wasiwe na wasiwasi juu ya roho wa mauti.”
Simon Mwakifwamba, Bahati Bukuku na Dotnata wakicheza wimbo wa Dunia Haina Huruma ulioimbwa na Bahati Bukuku.
MWAKIFWAMBA ANENA
Rais wa TAFF, Mwakifwamba alipoulizwa kuhusu uchache wa wasanii waliohudhuria ibadani hapo alisema: “Imani imekosekana kwa wasanii, maana kama wangekuwa nayo leo wengefurika hapa, lakini siwezi kuisemea nafsi ya mtu kwa maana kila mtu ana imani yake.
“Mimi nimefarijika sana na nina imani huyu pepo wa vifo anayetuandama hatakuwa na nafasi tena kwetu.”
Mchungaji Harris Kapiga akiongoza ibada ya maombezi Katika Kanisa la Nchi ya Ahadi, jijini Dar es Salaam.
DOTNATHA ACHARUKA
“Mimi nawashangaa wasanii wenzangu kwa kweli, hawana imani na mambo ya kiroho. Kiukweli ushirikika ni tatizo sana kwa wasanii. Leo kama wangekuja tukajumuika pamoja lingekuwa jambo zuri sana.
“Wasanii tupo kwenye hatari kubwa, lakini hii inatokana na wasanii wengi kujikita kwenye mambo ya kishirikina zaidi ya kumwabudu Mungu wa kweli. Nawashauri tumrudieni Mungu tutapona,” alisema Dotnatha.
Baadhi ya waumini wengine waliohudhuria katika ibada hiyo ya maombi.
TURUDI KWA MTABIRI
Hata hivyo, mnajimu maarufu nchini, Maalim Hassan Hussein Yahya hivi karibuni alisisitiza kuwa, vifo kwa wasanii nchini vitaendelea hadi mwaka wa kiutabiri utakapomalizika  hapo Aprili, mwakani.
“Huu ni utabiri na kama nilivyosema, utabiri ni mambo ya mahesabu ya kinajimu. Hakuna kitakachobadilika, vifo kwa wasanii, tena siyo Tanzania pekee - duniani vitaendelea hadi mwezi Aprili mwakani,” alisisitiza Maalim Hassan.
MTABIRI MWINGINE
Baada ya kifo cha Mzee Small aliibuka mtabiri mwingine, aliyejitambulisha kuwa ni Nabii wa Kanisa la Ufufuo lililopo Buza, jijini Dar es Salaam, Yaspi Paul Bendera ambaye amekazia kuwa vifo kwa wasanii wa filamu za Kibongo vitaendelea.
...Mchungaji Harris Kapiga (kushoto) akiongoza maombi.
Akizungumza bila hofu, Nabii Bendera alisema: “Watakufa wasanii 20 ndani ya mwezi huu (Juni). Huu si utani, ni maono.”
Bendera aliwataka wasanii wafike kanisani kwake ili awaombee na kuwapaka mafuta matakatifu yatakayowakinga na vifo.
Mwakifwamba na Dotnana wakiwa wamezama katika neno.
TUJIKUMBUSHE
Katika misa ya kumuombea marehemu Tyson iliyofanyika hivi karibuni katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar, Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Inuka Uangaze,  Buldozer Mwamposa aliwaombea wasanii wote akisema kuwa hakuna msanii atakayekufa tena.
Hata hivyo, licha ya kauli hiyo, siku chache baadaye mkongwe kwenye sanaa ya maigizo, marehemu Mzee Small alitangulia mbele za haki.
Mchungaji Mbeyela akizidi kuwaombea wasanii wa Bongo Muvi.
KUTOKA KWA MHARIRI
Sisi kama gazeti, hatuko upande wowote katika utabiri unaotangazwa na wanajimu na viongozi mbalimbali wa dini nchini lakini tupo pamoja na wafiwa katika kipindi hiki kigumu huku tukiamini kuwa kifo ni ahadi kutoka kwa Mungu.
Maneno yaliyotumika kwenye picha za wasanii picha ya kwanza, si halisi bali ni kama wanafikiri tu!
CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate