EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 21, 2014

HOFU YATANDA KWA WASHIRIKI WA SHINDANO LA TANZANIA MOVIE TALENTS

Baadhi ya washiriki wa Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) wakiwa mbele ya Majaji tayari kwa kupewa maoni yao na hatimaye kutaja watakaotoka chomwa na jua la utosi kwa Wiki hii. Kutoka Kulia ni Tishi Abdallah, Katikati ni Mtawa Kapalata na Kushoto ni Joshua Wambura.
Anneth Peter (katikati) akiwa mwenye huzuni kubwa kutokana na Mshiriki mwenza kutoka kanda ya Kaskazini Kareb John (hayupo pichani) kutoka kwenye shindano mara baada ya kuchomwa na jua la utosi.
 Washiriki wawili waliondolewa katika Shindano kwa wiki hii wakiwa mbele ya Jukwaa mara baada ya kutangaziwa kushindwa kuendelea kutokana na kuwa na idadi chache ya kura kutoka kwa watazamaji.Wa kwanza kushoto ni Kareb John na Malima Deogratius ambao wameaga mashindano.
  Kareb John na Malima Deogratius mara baada ya kutangaziwa kuyaaga mashindano.
 Mara baada ya Kareb John Kuaga mashindano Mshiriki kutoka kanda ya Kaskazini Annet Peter alionekana mwenye huzuni kubwa.
 Washiriki wakiwa na huzuni kutokana na wenzao kuaga mashindano.Picha zote na Josephat Lukaza wa Proin Promotions, Dar Es Salaam.
Na Josephat Lukaza - Proin Promotions Limited - Dar Es Salaam
Ni wiki ya Pili sasa ya mchujo katika Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) ambapo washiriki wengine wawili wamechomwa na Jua la Utosi na hatimaye kuaga shindano. Mchujo huo ni muendelezo wa Mchujo ambao kila wiki washiriki wawili watachomwa na jua la utosi na hatimaye kupelekea kuaga shindano la TMT.

Mpaka sasa Washiriki wanne tayari wameshayaaga mashindano na kupelekea washiriki 16 kubakia katika mchujo unaofuata.

Mpaka sasa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) limekua ni shindano lililoteka hisia za watanzania wengi waliopo ndani na nje ya Nchi kutokana na ubora, Uhalisia na Ubunifu wa hali juu kutoka kwa Waandaaji na waendeshaji pamoja na washiriki kuonyesha Vipaji vyao.

Ili kuweza kumnusuru mshiriki wako asichomwe na Jua la Utosi unachotakiwa ni kumpigia kura kadri uwezavyo ili kumfanya abaki ndani ya Nyumba ya TMT.

Mara baada ya washiriki wa wiki hii kuondolewa katika shindano hali imezidi kuwa ni simanzi kwa washiriki kutokana na kutokujua ni zamu ya nani kutoka wiki ijayo.

Washiriki waliotoka wiki hii ni Kareb John ambae alikua mmoja kati ya Washindi watatu kutoka kanda ya Kaskazini Mkoani Arusha huku Mshiriki Malima Deogratius akiwa ni Mshindi kutoka KAnda ya Pwani Mkoani Dar Es Salaam.

Ili kuweza kumnusuru mshiriki umpendae unachotakiwa kufanya ni Kuandika neno "TMT" ikifuatiwa na namba ya Mshiriki halafu unatuma kwenda namba 15678. Mfano TMT00 tuma kwenda 15678. Piga kura kadri uwezavyo ili kumnusuru mshiriki wako kutochomwa na Jua na Utosi wiki ijayo.

Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) ni shindano lililobuniwa na Kampuni ya Proin Promotions Limited ambayo inahusika na utengenezaji, Usambazaji na Uuzaji wa filamu za Kitanzania huku ikiwa na malengo pia ya Kuibua vipaji vya Kuigiza na Mpira wa Miguu kwa Wanawake. Shindano hili Pia linaendeshwa na Kusimamiwa pia na Kampuni bora ya Usambazaji wa Filamu nchini ya Proin Promotions Limited

Huzuni na Simanzi zaendelea kutawala ndani ya Nyumba ya TMT kwa washiriki hao wawili kuondoka lakini Pia Hofu Yaendelea Kutanda ndani ya Nyumba ya TMT kwa washiriki kwa kutokujua ni zamu ya nani sasa kuchomwa na jua la utosi litakalompelekea kuaga shindano kwa wiki ijayo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate