EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 18, 2014

MTOTO MIAKA 12 AELEZA ALIVYOFUNDISHWA UCHAWI


MTOTO mmoja mkazi wa Kimara Salanga, jijini Dar es Salaam (jina limehifadhiwa) mwenye umri wa miaka 12 hivi karibuni aliibuka na kutoa madai mazito, akimtuhumu baba yake mkubwa kuwa alimfundisha uchawi, Ijumaa lina mkasa kamili.
Mtoto (kulia jina limehifadhiwa) mwenye umri wa miaka 12 anayemtuhumu baba yake kumfundisha uchawi.

Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni, mtoto huyo alisema alianza kufundishwa tabia hiyo mbaya na baba yake mkubwa wakati huo akiwa na umri wa miaka mitano jijini Mbeya, kwa kumwelekeza namna ya kuroga na kuua watu.
Katika mojawapo ya matukio makubwa aliyodai kuwahi kuyafanya ni pamoja na kutengeneza ajali ya boti iliyotokea Nungwi mapema mwaka huu ambapo yeye na wenzake walitumwa na baba yake huyo kutega mambo yao huku wengine wakipanda kwenye chombo hicho ili kuongeza uzito uliosababisha boti hiyo kuzama na kuua watu kibao.
“Tuligandisha maji na kuweka sindano ambazo zilitoboa na baada ya watu kufa tulichukua nyama na damu kwa ajili ya kula na kunywa. Kwa hiyo nimeua na kula nyama za watu.
Baadhi ya tunguli za uchawi zilizokuwa zikitumiwa na mtoto huyo.
“Pia niliwahi kutumwa kwa msichana ambaye nilimnyunyizia dawa, nikamkalia na kumkaba shingoni mpaka akafa, nikamchukua na kumpeleka kwa baba mkubwa, pale kitandani niliacha gogo ambalo lina sura yake, kule tulimla na kunywa damu yake sisi na wachawi wenzetu.
“Baada ya kufanya matukio hayo mazito, baadhi ya wananchi waliponigundua kuwa ni mchawi, walienda kunishtaki kwa mama yangu mzazi, wakimwambia asiponihamisha wataniua.
“Kwa hali hiyo, huyu mjomba wangu akanileta Dar kwa ajili ya kufanyiwa maombi, lakini siku ya kwanza tu baada ya kufika, wakati nakwenda kuchota maji nilikutana na mmoja (jina limehifadhiwa) aliyeniambia kumbe mimi ni kijana wa kazi, alinitambua kutokana na nyota tunayobandikwa kwenye paji la uso baada ya kujiunga na uchawi ambayo ukikutana na mwenzako mnatambuana.
“Baada ya kuniambia hivyo, usiku wake nikiwa nimelala, baba mkubwa alikuja kichawi na kunichukuwa na kunipeleka kwa yule mzee ambaye ndiye mkuu wa wachawi wa eneo hili, akanikabidhi kwake na mikoba yangu ya kichawi na hapo ndipo nikaendelea na kazi kwa upande wa huku Dar nikishirikiana na wachawi wengine.
“Kazi yetu mara nyingi ni kuloga, kuua na kunyunyizia dawa kwenye makaburi, yakifunguka tunachukuwa nyama za watu na mafuvu na kuyapeleka nyumbani kwa yule mkuu wa wachawi wa eneo hili tunapokutania.
“Hapa nyumbani kwa mjomba niliweka dawa kwenye ukingo wa nyumba ili wasimalizie kujenga na kumloga mkewe ambaye tulimtupia vidonda vya tumbo, nilitaka kumuua lakini maombi yalimsaidia,” anasimulia kijana huyo.
ATINGISHA KIJIJI CHA SALANGA
Kwa mujibu wa shangazi yake aliyefahamika kwa jina la Lucy, baada ya kufanyiwa maombi kanisani kwa Mwingira, mtoto huyo alikiri kuachana na uchawi lakini alikuja kugundua bado anaendelea kutokana na kufanya maombi ya kufunga ambapo aliona katika maono kuna dawa ameweka kwenye nguo zake alizokuwa akipenda kuzivaa kila siku.
Alipobanwa kwa vitisho ndipo aliwataja wachawi wenzake na kuongeza kuwa kila alipokuwa akitoka kwenye maombi, anakutana na wachawi wanamvisha uchawi tena na ule wa tumboni aliolishwa bado unaendelea kufanya kazi.
WATINGA KWA MJUMBE WA SERIKALI ZA MITAA
Baada ya kueleza mambo hayo mazito waliamua kutinga kwa mjumbe ambaye baada ya kuwasikiliza aliitisha kikao cha pamoja na yule mzee ambapo mtoto huyo alieleza kinagaubaga mbele ya wananchi mambo wanayofanya wakiwa na mzee huyo lakini alikataa na kuapa kwa kutumia msahafu kuwa anasingiziwa na kwamba hajawahi kufanya mambo hayo.
NYUMBANI KWA MZEE ANAYEDAIWA MCHAWI
Mapaparazi wetu walitinga nyumbani kwa mzee huyo ili azungumzie suala hilo lakini jitihada ziligonga mwamba baada ya kumkosa ambapo mkewe anayedaiwa  kushirikiana naye kwenye mambo hayo, aliyejitambulisha kama mama Isha, alisema;
“Ni kweli huyo mtoto alieleza mambo hayo kwa mjumbe lakini naapa kwa jina la Mwenyezi Mungu, mimi na mume wangu siyo wachawi, hayo ni maneno ya uzushi tu, watu wa kijiji hiki wanatuonea wivu kwa sababu tuna maendeleo kwani hawapendi mtu awe na mafanikio,” alisema.
CHANZO GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate