EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, July 25, 2014

SHEHE AWAVAA WEMA, DIDA!


CHANZO NI GPL
Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum (pichani kushoto), amewavaa baadhi ya mastaa Waislamu wa Kibongo wenye kaunta zenye pombe majumbani mwao hasa kwa kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani huku akiwataka waondoe mara moja kwani ujana unawasumbua, Ijumaa lina ripoti kamili.
Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Alhad Mussa Salum
WAMO DIDA, WEMA & DIAMOND
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba baadhi ya mastaa Waislamu wenye kaunta zenye pombe majumbani mwao kuwa ni pamoja na Mtangazaji wa Radio Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’, staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

Akizungumza na Ijumaa mapema wiki hii jijini Dar es Salaam, Shehe Salum alisema kwamba, kwanza ameshtushwa na habari ya hao wanaojiita mastaa kuwa na kaunta za pombe majumbani kwao kwani ni habari ngeni masikioni mwake na kusema kuwa kwa semina wanayoipata mwezi huu hawatakiwi kutenda maovu.
Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
WANAPASWA KUOMBA DUA
Alisema kuwa mastaa hao wanapaswa kuutumia Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kusoma Quran, kuomba dua na kuacha maovu yote.
“Hao mastaa wenye kaunta wanatakiwa kuacha na kuondoa kabisa kwani Ramadhani imeletwa kwetu kama semina na hatutakiwi ikiisha turejee kule tulipokuwa.
“Mafunzo ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani maana yake tujifunze na tuachane na kule tulikotoka, hivi kwa nini wasijiulize mastaa wenzao wako wapi kwa mfano Sharo (mchekeshaji Sharomilionea) na wengine waliotangulia mbele ya haki?
WANAKULA UJANA?
“Wasijidanganye na ujana walio nao, wakikutwa na mauti, mbele ya haki watasema nini?
“Nawaasa kutorudi nyuma na kujifunza kwelikweli namna ya kuishika dini na nguzo zake,” alisema shehe huyo.
Baa ya ndani ya Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
SWAUMU ZAO VIPI?
Shehe mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake anayeswalisha katika msikiti uliopo Sinza jijini Dar alisema:
“Kiukweli kabisa pombe ni haramu na hatutakiwi  kuikaribia hata kidogo. Hawa ambao wamefikia hatua ya kuwa na kaunta za pombe majumbani kwao, wanakosea sana.
“Kwa mfano mwezi huu mtukufu kama wanafunga, si kwamba hawapati thawabu, wanapata ila kwenye kuikaribia pombe, watakuwa wanapata dhambi.
“Kwa hiyo unaweza kuwa umefunga lakini ukashangaa mpaka mwezi umeisha thawabu zako zimepungua kutokana na mambo mengine yanayokufanya upate dhambi.”
Mtangazaji wa Radio Times FM, Hadija Shaibu ‘Dida’,
DIDA ANASEMAJE?
Baada ya Shehe Salum kuwavaa mastaa hao, gazeti hili lilimsaka mmoja baada ya mwingine.
Alipopatikana, Dida ambaye ni binti wa Kiislamu mwenye kaunta ya pombe nyumbani kwake, Mwananyama, Dar alikuwa na haya ya kusema:
“Ni kweli mimi nina kaunta ndani kwangu lakini kwa mwezi huu hata mimi naichukia sana pombe na sipendi kabisa kuiona pamoja na kwamba sijui sana sheria za dini japo ni muhimu kuzijua nguzo zake.
“Hata mimi kama binti wa Kiislamu kwa mwezi huu mtukufu sinywi pombe na hiyo kaunta ni kwa ajili ya wageni wangu wanaonitembelea.”
Staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’
NYUMBANI KWA DIAMOND
Wiki mbili zilizopita ishu hiyo ilitibua futari nyumbani kwa Diamond maeneo ya Sinza-Mori, Dar hivyo kulazimika kuondoa pombe kali zilizokuwa zimejazwa kwenye kaunta.
WEMA VIPI?
Kwa upande wake Wema ambaye ukiingia kwake kitu cha kwanza unakutana na kaunta ya pombe na vinywaji vingine alipotafutwa ili kuzungumzia ishu hiyo, simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate