EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 23, 2014

Siri utupaji viungo vya maiti yabainika



 Makamu Mkuu wa Chuo cha International Medical and Technological University (IMTU), Profesa PV Prabhak Rao (mwenye koti la blue)  na viongozi wengine wakisindikizwa na polisi kuingia kwenye Kituo cha Oysterbay, Dar es Salaam jana, kwa ajili ya mahojiano kuhusiana na upatikanaji wa viungo vya binadamu eneo la Mpigi Bunju. Picha na Rafael Lubava

Dar es Salaam. 
Wakati ikibainika kuwa viungo vya miili ya binadamu vilivyookotwa juzi katika Bonde la Mto Mpiji nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam vilitoka katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU), jana Jeshi la Polisi liliwatia nguvuni watumishi wanane wa chuo hicho kuhusiana na sakata hilo.

Kukamatwa kwa watumishi hao kumeelezwa na Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova kuwa ni baada ya uchunguzi wa awali kubaini kuwa viungo hivyo kwa mara ya mwisho vilikuwa katika maabara ya IMTU.

Alisema tukio hilo lilitokea juzi jioni eneo la Bonde la Mbweni Mpiji ambako iligundulika mifuko ya plastiki 85 yenye mabaki ya viungo vya binadamu.

Kutokana na tukio hilo, Polisi imeunda jopo la wapelelezi saba likiongozwa na Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalumu, Jafari Mohamed kusaidiana na daktari wa jeshi hilo kufanya uchunguzi wa miili hiyo.

“Katika uchunguzi wetu tulibaini kuwa hivyo viungo vya binadamu vilitolewa katika Chuo cha IMTU na kusindikizwa na mfanyakazi wa ngazi ya juu kwa ajili ya  kutupwa eneo la Bonde la Mbweni Mpiji,” alisema Kova.

Alisema mifuko hiyo ilikuwa myeusi ikiwa na viungo vya aina mbalimbali vikiwamo vichwa, miguu, mikono, moyo, mapafu, vifua na mifupa ya aina mbalimbali.

“Viungo hivyo havikuwa na harufu wala uvundo wa aina yoyote na vilionekana vimekaushwa na kukakamaa,” alisema.

Alisema katika eneo hilo walikuta vifaa vinavyotumika hospitali kama glovu, nguo maalumu (apron) 20 na karatasi mbili zenye maswali ya kujibu.

Kova alisema viungo hivyo vilichukuliwa na kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).

Alisema jeshi hilo limefungua jalada la uchunguzi ili kujua sheria gani imevunjwa na kwa nini viungo hivyo vilitupwa hapo na kwa nini wasitumie utaratibu mzuri wa kuhifadhi na kwamba endapo kuna makosa ya kisheria, hatua zitachukuliwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Muhimbili wapokea mabaki

Meneja Uhusiano wa MNH, Aminiel Aligaesha alisema jana kuwa hospitali hiyo imepokea vifurushi 40 vyenye mabaki ya miili ya binadamu na kuhifadhiwa wakisubiri maelekezo ya polisi... “Hili ni suala la polisi, ninachoweza kusema ni kweli tumepokea vifurushi hivyo jana (juzi) usiku.”

IMTU yakiri kuhusika

Wakati Kova akisema hayo, uongozi wa IMTU ulikiri kuhusika na mabaki ya miili hiyo yaliyotupwa katika mto huo usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita.

Naibu Makamu Mkuu wa chuo hicho, Dk Fariji Mtango alisema jana kwamba anaamini miili hiyo inaweza kuwa ni ile iliyotoka katika chuo hicho, ambayo imekuwa ikifanyiwa mazoezi na wanafunzi kwa kuwa walihitaji kuiteketeza na walishatoa agizo hilo.

Alisema walitoa agizo kwamba mabaki hayo yapelekwe Muhimbili kwa mujibu wa utaratibu wao kwa kuwa hayakuwa na matumizi tena, kwa kuwa ndiyo sehemu yenye uwezo wa kuyateketeza na kutoa jukumu hilo kwa mmoja wa wakufunzi wa chuo hicho ambaye jana alikuwa safarini.

“Sasa zaidi hatujui kilichoendelea lakini tulipoangalia jana (Jumatatu) tulikuta sehemu yalipohifadhiwa imesafishwa, hivyo inawezekana ni sehemu ya vile vilivyoondolewa hapa. Hatukutarajia kwamba vingetupwa katika eneo lisilokuwa sahihi kama ilivyofanyika,” alisema.

Dk Mtango alisema hiyo ilikuwa moja ya hatua za kupisha wakaguzi ambao walitarajiwa kukuta maeneo yote ya kufundishia yakiwa katika hali ya usafi na unadhifu.

“Hawa wakaguzi wanapokuja wanatakiwa waone vitu vyote vikiwa sawa. Hata kama wangeona hayo mabaki ya miili ya binadamu isingekuwa tatizo, bahati nzuri wamekuja jana na wamefanya kazi yao vizuri,” alisema.

Muda mfupi baada ya kutolewa kauli hiyo, viongozi tisa wa chuo hicho na walinzi wawili walikamatwa mnamo saa 7.30 mchana na kupelekwa katika Kituo cha Polisi Oysterbay ambako wanashikiliwa, lakini baadaye Kova alisema waliokamatwa ni wanane.

Jana mchana eneo la chuo cha IMTU lilikuwa chini ya ulinzi mkali wa polisi waliotanda kuanzia getini, mapokezi na kwenye bustani za chuo hicho na wengine waliovalia sare maarufu kama ‘tigo’ ambao walikuwa wakishika doria mbele ya chuo hicho.

Hatua kuchukuliwa

Dk Mtango alisema uongozi wa chuo hicho umeshtushwa na kutupwa kwa mabaki hayo katika utaratibu usiokubalika na utafanya uchunguzi na kuchukua hatua kwa wote waliohusika.

“Tunaanza na huyu ambaye tulimpa hili jukumu. Yeye ndiye aliyetakiwa kusimamia na anaujua wazi utaratibu wetu. Kwa sasa hajafika hapa na hata simu yake haipatikani. Tunaarifiwa kwamba amekwenda Zanzibar,” alisema.

Jinsi ilivyotokea

Juzi jioni, ilitokea taharuki baada ya wananchi kubaini viungo hivyo na taarifa kuanza kusambaa katika mitandao ya kijamii na baadaye vyombo vya habari na hadi jana mjadala kuhusu suala hilo ulikuwa mzito na wananchi wakihoji miili hiyo ni ya watu gani, imetoka wapi na imetupwa na watu gani.

Shuhuda wa tukio hilo, Mariam Nkumba alisema mara ya kwanza aliona mifuko yenye viungo hivyo Jumapili alipokwenda kuponda kokoto katika eneo hilo lakini hakubaini kulikuwa na nini.

Siku hiyo, Nkumba alisema aliondoka katika eneo hilo saa 12 jioni bila kujua nini kilikuwa ndani ya mifuko hiyo na siku iliyofuata (Jumatatu), alikwenda kuchukua mfuko mmoja ili ahifadhie kokoto zake, ndipo aliposhtuka kuona viungo vya binadamu.

“Mifuko ilikuwa mingi kweli, yote ilikuwa imejaa viungo vya binadamu. Mpaka sasa sijala na sina hamu ya kula. Ukiiona ile miili huwezi kula chakula,” alisema.

Mfanyakazi wa Kampuni ya Ujenzi ya Skol iliyopo karibu na eneo hilo, Supery Kaijunga alisema mara alipopata taarifa kutoka kwa Nkumba alianza kutoa taarifa kwa wananchi wengine ili kwa pamoja wajue la kufanya.

Baadaye walitoa taarifa polisi ambao walifika saa mbili usiku na kukusanya mabaki yote na kuondoka nayo.

Hata hivyo, Kaijunga alieleza wasiwasi wake kuhusu wingi wa miili hiyo na kuhoji walikuwa watu gani na walitoka maeneo gani.

“Tukio hili siyo la kawaida na halijawahi kutokea huku kwetu. Tunakuwa na wasiwasi sana labda nasi maisha yetu yatachukuliwa kama hawa; polisi wafanye uchunguzi wa kina kubaini ukweli wake,” alisema Kaijunga.
Imeandikwa na Andrew Msechu, Peter Elias na Pamela Chilongola wa Mwananchi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate