EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 23, 2014

TAMASHA LA MATUMAINI 2014 BURUDANI MWANZO MWISHO


HAPATOSHI! Mastaa wanaokimbiza katika anga la muziki wa Bongo Fleva, wanatarajia kuchuana vilivyo kulipamba Tamasha la Usiku wa Matumaini katika Uwanja wa Taifa, Agosti 8, mwaka huu.
Diva wa muziki kutoka Nigeria ambaye anatamba na wimbo wa Johnny, Yemi Alade.
Akizungumza na Risasi Vibes, mratibu wa tamasha hilo ambalo linafanyika kwa awamu  tatu mwaka huu, Luqman Maloto aliianika listi ya mastaa hao huku akiahidi kuwa itazidi kuongezeka kadri siku zinavyozidi kusonga.

“Mpaka sasa kila kitu kinakwenda sawa, zimesalia wiki mbili tu na naamini wale mashabiki wa muziki wa Bongo Fleva watapata kile wanachokihitaji siku hiyo kutokana na mastaa watakaokuwepo kukamua mwanzo mwisho, miongoni mwao ni pamoja na Meninah, R.O.M.A, Shilole, Madee, Juma Nature na kundi zima la TMK wanaume Halisi na wengine kibao ambao listi kamili itaendelea kutoka katika magazeti pendwa.
Akimzungumzia mkali wa Hip Hop, Ibrahim Mussa ‘R.O.M.A Mkatoliki’, Maloto alisema kuwa rapa huyo atakuwepo kuwainua mashabiki wote wanaopenda muziki wa Bongo Fleva.
“Ataliamsha jukwaa kwa kupiga nyimbo ambazo kwa namna moja zimetokea kupendwa na mashabiki wengi wa muziki wa kizazi kipya kama Mechi za Ugenini, Tanzania, Mechi na hii ya sasa hivi Karibu Kwenye Karamu (K.K.K) na nyingine kibao ambazo zitakuwa kama sapraizi kwa mashabiki.
 Zuwena Mohamed ‘Shilole’ au 'Shishi Baby'.
Maloto aliongeza kuwa Rais wa Manzese Hamad Ally ‘Madee’ atakuwepo kuhakikisha Bongo Fleva inalitawala jukwaa kwa kuwachezesha mashabiki kwa kupiga nyimbo zake zote kali kwa staili tofauti.
“Atawadhihirishia mashabiki kwa nini anaitwa Rais wa Manzese. Mashabiki wategemee kusikia na kucheza siku hiyo nyimbo zote kali kama Pombe yangu, Niskize, Hip Hop Haiuzi, Tema Mate Tuwachape na nyingine kibao ambazo zitaacha gumzo siku hiyo.”
Kuhusu Meninah ambaye amekuwa akifanya maajabu jukwaani katika shoo zote anazopiga kutokana na uwezo wake wa kuimba na kucheza kwa kulitawala jukwaa, Maloto alisema atakamua mbaya.
“Kuonesha kuwa mwaka huu ni wa mabadiliko kwa mara ya kwanza katika Tamasha la Matumaini mashabiki watamuona Meninah akipafomu nyimbo zake kali kama Shaghala Baghala, Kacopy Kapaste, Dream Tonight na nyingine kibao ambazo zitakonga nyoyo za mashabiki wote watakaofika siku hiyo.”
Ally kiba
SHILOLE
Akimzungumzia diva wa muziki wa mduara nchini, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, Maloto alisema mashabiki wategemee ushindani mkubwa siku hiyo kwani mwanadada Shilole ataungana na Meninah katika kuhakikisha wanamfunika diva wa muziki kutoka Nigeria ambaye anatamba na wimbo wa Johnny, Yemi Alade.
“Sidhani kama Shilole atakubali kufunikwa kirahisi na Yemi Alade kutoka Nigeria. Atahakikisha mashabiki wake wote anawapa shoo ya kufa mtu kwa kuimba nyimbo zake zote kali zinazotamba kama Chuna Buzi, Paka la Baa, Lawama, pamoja na huu mpya wa Namchukua huku akifanya mikogo ya maana jukwaani.”
Usiku wa Matumaini umedhaminiwa na Vodacom, E.FM, Pepsi, Clouds FM, Azam TV, Times FM pamoja na SYCORP.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate