EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 14, 2014

TAMASHA LA MATUMAINI 2014: STAA WA JOHNNY... EEE! KUTOKA NIGERIA NAYE NDANI

Yemi Alade.
IM looking for my Johnny
Where is my Johnny...
Johnny oooh
Do you know Johnny...question
I'm looking for my Johnny.
Kiitikio hicho ndiyo habari ya mjini kwa sasa na good news ni kwamba staa wa wimbo huo, Yemi Alade wa Nigeria anadondoka Bongo kwa mara ya kwanza kuungana na listi ndefu ya wasanii wa nyumbani kulipamba Tamasha la Usiku wa Matumaini, Agosti 8, mwaka huu (Nanenane).
Staa wa Bongo Fleva, Ali Kiba atakuwepo katika Tamasha la Matumanaini 2014.

MJUE ZAIDI
Mwanadafada huyu ambaye alizaliwa Machi 13, 1989, anauweza muziki na kuthibitisha hilo alianzia kanisani akiwa mwanakwaya. Kukubalika kwake kulianza mwaka 2009 aliposhinda katika onesho la vipaji lililojulikana kama Peak Talent.
Wimbo wake wa kwanza kuachiwa ulikuwa Fimisile aliomshirikisha eLDee na baada ya kuuachia, alijizolea mashabiki wengi katika kipindi kifupi.
Mkali wa Pombe Yangu, Madee naye ndani.
Julai 2012, Yemi aliachia video ya wimbo mwingine uitwao Ghendhenlove.
Mpaka sasa ameshapiga kolabo na wanamuziki wakubwa wakiwemo Dipp, Ice Prince, eLDee, M.I, Sauce Kid, Shank, Sir Shina Peters, Waje, Wizkid, Yemi Sax na kufanya kazi na maprodyuza wakubwa wakiwemo OJB Jezreel, eLDee, E. Kelly, IBK, Major One, Sizzle Pro, DJ Klem, Bigfoot, Shadybizniz, Dtunes, Garth, na Flip Tyce.
Mwanamuziki wa Hip Hop, Roma Mkatoliki naye atashusha burudani ndani ya Tamasha la Matumaini 2014.
Kama hiyo haitoshi, Yemi ana mkataba na Kampuni ya Effyzzie Music Group na ndiyo waliomuwezesha kutoa albamu ya Johnny aliyoitengeneza chini ya Selebobo.
SHOO YA MATUMAINI
Mkali huyo kutoka Jimbo la Abia pande za Nigeria, ameahidi kupiga shoo kali ambayo itafuta historia ya baadhi ya wasanii wa nchini kwao waliowahi kukanyaga ardhi ya Jakaya (Bongo).
Atazipiga ngoma zake kali zikiwemo Tangerine (mpya) na Johhny ambazo zinabamba kutokana na staili yake ya kuimba na kucheza sambamba na mashabiki jukwaani.
MASTAA WA BONGO
Listi ya mastaa kutoka Bongo itaongozwa na Ali Kiba, R.O.M.A, Madee, Juma Nature (na kundi zima la Wanaume Halisi) na wengine kibao ambao watatangazwa hivi karibuni.
Juma Nature atakuwepo kutoa shangwe kwa wapenzi wa Tamasha la Matumaini Agosti 8, 2014.
TUJIKUMBUSHE MWAKA JANA
Mwaka jana tamasha hilo lilifanyika Julai 7 (Sikukuu ya Sabasaba) ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete. Mwaka huu atakuwa nani? Endelea kufuatilia magazeti Pendwa yatakujuza.
Burudani ya mwaka jana ilikuwa ni asilimia mia kwani mbali na michezo mbalimbali kulipamba tamasha hilo kama mechi wa wabunge wa Simba na Yanga, Bongo Fleva na Bongo Movie, staa kutoka Kenya, Jackson Makini ‘Prezzo’ alitimba uwanjani na kuchuana vikali na Nasibu Abdul ‘Diamond’ na kusababisha burudani ya kutosha.
MWAKA HUU SASA
Ukiachana na mkali huyo kutoka Nigeria, katika upande wa mpira wa miguu, wabunge wa Simba watakipiga na wenzao wa Yanga bila kusahau mpambano mkali wa ngumi kati ya mabondia wanaotisha kwa sasa, Mada Maugo na Thomas Mashali. Tamasha hili linawajia kwa udhamini wa Vodacom, Pepsi, Azam Tv, E.FM na Times FM.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate