EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 30, 2014

JIDE, DOGODOGO GUMZO MJINI! DOGO ANASWA NA MKOKO WAKE

Na Musa Mateja
OHOOO! Siku chache baada ya ndoa ya Legendary wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ na mtangazaji mahiri nchini, Gardner Gabriel Habash ‘G Habash’ kudaiwa kuvunjika, gumzo limeibuka kufuatia kunaswa kwa picha za Jide na kijana mmoja (dogodogo) aliyetajwa kwa jina la Meddy Ahmed ‘Mtoto wa Vitoto’, Risasi Jumamosi linakupa kinaga ubaga.
Legendary wa Bongo Fleva, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ akishow love na Meddy Ahmed ‘Mtoto wa Vitoto’.

TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Mtoto wa Vitoto huyo amekuwa na urafiki uliotukuka na Jide kwa muda mrefu kabla na baada ya mtafaruku wa ndoa ya Jide na mumewe Gardner hivyo kudaiwa kuwa ndiyo faraja ya mawazo ya mwanamuziki huyo hususan kipindi hiki cha changamoto ya mgogoro wa ndoa yake.
Chanzo hicho kilizidi kumwaga data kuwa, ukaribu wa Jide na bwa’mdogo huyo ulipitiliza kiasi cha watu wa karibu na staa huyo kuanza kuhisi huenda wana uhusiano usiofaa.
“Ukaribu wao ulipitiliza hadi kila mtu wa karibu na Jide akautilia shaka, isitoshe kama unavyojua, Jide si mtu wa kuweka mambo yake hadharani. Mbaya zaidi Jide amekuwa akimposti dogo huyo kwenye mitandao yake ya kijamii,” kilisema chanzo hicho.
Meddy Ahmed ‘Mtoto wa Vitoto’ akiwa kwenye ndinga ya 'Jide'.
APEWA NAFASI YA TATU
Wakati paparazi wetu akiendelea kukusanya data kuhusiana na ishu hiyo, chanzo hicho kilizidi kushibisha maelezo yake kwa kusema Jide amekuwa akimwandika nambari tatu dogo huyo kwenye mitandao ya kijamii ambapo baadhi ya watu eti wanatafsiri kuwa, maana yake ni kwanza mumewe (Gardner), ya pili yeye (Jide) na ya tatu ni dogo huyo.
“Dogo yuko sawa na Jide maana ukitaka kuamini fuatilieni kwa ukaribu mtawaona tu hata katika mitoko ya Jaydee (Jide). Kuna picha kibao zipo kwenye akaunti yake, dogo anaonekana akiwa kwenye ndinga (gari) la Jide ingawa dogo yuko makini kweli na suala hilo, nafikiri wamewekeana mikakati ya kuwa wa siri,” kilisema chanzo hicho.
Meddy Ahmed ‘Mtoto wa Vitoto’ akipozi nyuma ya ndinga hiyo aina ya Range Rover evoque.
PICHA ZATUA RISASI
Baada ya paparazi wetu kupewa mchongo huo, alianza kuzisaka picha hizo kupitia vyanzo vyake mbalimbali na kufanikiwa kuzidaka zikimuonesha bwa’mdogo huyo akijiachia juu ya ndinga inayodaiwa ni ya Jide katika pozi tofautitofauti.
Kama hiyo haitoshi, kupitia akaunti ya Jide ya Instagram, zilionekana picha tofauti za dogo huyo, ikiwemo ile ambayo aliiunganisha picha tatu tofauti, mbili za kwake na moja waliyokuwa ‘klozdi’ na Mtoto wa Vitoto.
JIDE ALIPOTAFUTWA!
Katika kutaka kujua ukweli wa ukaribu wa wawili hao na kufuatilia mwenendo mzima wa viwanja vyao vya starehe, paparazi wetu alimvutia waya Jide lakini simu yake haikupatikana hewani kwa siku tatu mfululizo.
‘Jide’ na mtangazaji mahiri nchini, Gardner Gabriel Habash ‘G Habash’ wakati wakiwa pamoja.
DOGODOGO SASA
Baada ya Jide kutopatikana hewani, Jumatano iliyopita paparazi wetu alimtwangia simu Mtoto wa Vitoto ili kumsikia anauzungumziaje ukaribu wake na sista huyo ambapo baada ya kusomewa mkasa mzima, dogo alikata simu kwa madai kuwa sehemu aliyokuwa siku hiyo haikuwa nzuri na kuahidi kumpigia paparazi wetu baadaye lakini hakufanya hivyo hadi kesho yake (Alhamisi) alipopigiwa tena na gazeti hili na kupokea.
ADAI NI MARAFIKI
Huku akiashiria sauti ya kutojiamini, dogo huyo alisema yeye na Jide ni marafiki wakubwa katika mazingira ya kawaida, pia  ni shabiki wake kama walivyo wengine ila ishu ya picha mtu yeyote anaweza kupiga.
Kuhusu kuendesha gari linalodaiwa ni la Jide, dogo alisema hajawahi ila ameshapiga nalo picha na mtu yeyote anaweza kufanya hivyo kama ana uhusiano mzuri na mwanamuziki huyo.
“Jide ni rafiki yangu na mimi ni shabiki wake wa kawaida. Kwa hiyo hilo siyo tatizo lakini pia kuhusu gari mimi sijawahi kuendesha gari la Jide lakini nimewahi kupiga nalo picha kweli kama shabiki mwingine na hakuna shida, ila siyo wapenzi, ni marafiki tu,” alisema Mtoto wa Vitoto.
ATUMA UJUMBE WA MASIHARA
Baada ya kuzungumza hayo, Mtoto wa Vitoto alikata simu na baada ya dakika tatu alituma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) kwenye simu ya paparazi wetu uliosomeka hivi: “Acha kunizingua mwana.”
Paparazi wetu alipompigia simu kwa mara nyingine kutaka kujua alikuwa na maana gani, dogo huyo hakupokea simu na hata alipoandikiwa SMS kwamba atoe ufafanuzi kuhusu ujumbe wake huo, hakujibu chochote hadi gazeti hili linakwenda mitamboni.
MTOTO WA VITOTO NI NANI?
Mtoto wa Vitoto ni kijana wa mjini tu, si Mbongo Fleva wala si Mbongo Muvi ila inadaiwa kwa sasa anafanya shughuli zake mkoani Morogoro. Amewahi kuishi Magomeni, Dar ambapo kwa sasa anadaiwa kuhamia Kinondoni, Dar. Ana asili ya Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate