EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 19, 2014

DOKII AMPA ASKARI RUSHWA YA BUSU

Stori: Sifael Paul/Global Publishers
MAKUBWA, madogo yana nafuu! Mwigizaji wa kitambo na mwimbaji wa muziki wa Kizazi Kipya, Ummy Wenslaus 'Dokii' anadaiwa kutoa kali ya karne baada ya kumpa askari wa jiji rushwa ya busu, Ijumaa lina mkanda kamili.
Mwigizaji wa kitambo na mwimbaji wa muziki wa Kizazi Kipya, Ummy Wenslaus 'Dokii' akiomba ruksa ya kusepa na gari kutoka kwa askari wa jiji (city parking).
Tukio hilo ambalo gazeti hili lina picha za mnato na video lilijiri kwenye Makutano ya Mtaa wa Narung’ombe na Swahili, Kariakoo jijini Dar, asubuhi ya saa 4:00, Septemba 15, mwaka huu.
Kwa mujibu wa ‘shushushu’ wetu, Dokii alipaki ‘vibaya’ gari alilokuwa nalo aina ya Toyoya Noah la rangi nyeusi ambapo alifuatwa na kuambiwa kwamba sehemu aliyopaki hairuhusiwi.
Ilisemekana kwamba alitumia ‘ustaa’ wake kuwapuuza akaingia kwenye maduka na kuendelea na ‘shopping’ zake.Ilidaiwa kwamba aliporudi na kutaka kuondoka, alikuta mkoko huo umefungwa mnyororo na vyuma kwenye tairi la nyuma na askari wa jiji (city parking) hivyo akashindwa kutimua.
'Dokii' akitoa rushwa ya busu kumlainisha 'askari wa city'.
Ilielezwa kwamba baadaye alifuatwa na mkuu wa askari hao almaarufu kwa jina la Masai ambaye alimwambia kuwa alitakiwa kutoa faini ya shilingi elfu hamsini.
Iliendelea kudaiwa kwamba huku akidhani watu hawamjui alilianzisha na askari hao na kuanza kuzozana.
Muda mfupi baadaye ilijitokeza kadamnasi ambayo ilikuwa ikimzomea ndipo akakimbilia dukani kwa mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Chid.
'Dokii' akitoa namba ya simu kumlainisha askari huyo.
Ilidaiwa kwamba mwanaume huyo alimpatia msanii huyo shilingi elfu tano ili awapoze askari hao huku akimuombea wamfungulie gari aondoke lakini jamaa hao waliikataa.
Ilielezwa kwamba baada ya kuomba sana askari hao walikubali kumwachia baada ya kummwagia kiongozi wao mabusu ya kimahaba hadharani, kisa tu hakuwa na fedha ya kulipa faini.

Ilidaiwa kwamba baada ya kumlainisha jamaa huyo kwa mabusu motomoto na kufutiwa shitaka, aliachiwa huru bila kutoa chochote huku askari aliyeonjeshwa ‘utamu’ akibaki na mfadhaiko huku akiomba namba ya simu.
Askari wa 'city' akimruhusu 'Dokii' kuondoka eneo la tukio  mara baada kuchukua namba ya simu.
Ilisemekana kwamba ili kuua msala, msanii huyo alimpatia namba ya simu kisha akatoka nduki.
Ni rushwa? Kutoa kitu ili kununua haki kama alivyofanya Dokii ya kutoa busu ili aachiwe, nayo ni rushwa pia.Jitihada za kumpata Dokii ili kuzungumzia mkasa huo hazikuzaa matunda kufuatia simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa hivyo jitihada zinaendelea. Stay tune!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate