Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan
IMEVUJA! Kuvunjika kwa Kundi la Bongo Movie Unity kumedaiwa kuwa ni laana ya aliyekuwa memba hai wa kundi hilo, marehemu Steven Kanumba kutokana na kumnyanyapaa enzi za uhai wake, Ijumaa linakupa mchapo kamili.
IMEVUJA! Kuvunjika kwa Kundi la Bongo Movie Unity kumedaiwa kuwa ni laana ya aliyekuwa memba hai wa kundi hilo, marehemu Steven Kanumba kutokana na kumnyanyapaa enzi za uhai wake, Ijumaa linakupa mchapo kamili.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Kanumba alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa kundi hilo lakini kabla hajafa, yaliibuka majungu ambayo yalimsababisha ajiengue na kususia kundi hilo huku akiwa na kinyongo moyoni.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Kanumba alikuwa ni miongoni mwa waasisi wa kundi hilo lakini kabla hajafa, yaliibuka majungu ambayo yalimsababisha ajiengue na kususia kundi hilo huku akiwa na kinyongo moyoni.
“Kanumba hakufurahishwa na majungu yaliyokuwa yakiendelea ndani ya
klabu dhidi yake, akajiapiza kwamba hatakaa akashiriki masuala ya kundi
hilo hadi pale wahusika watakapojisafisha.
“Wakati sisi tukipanga yetu, Mungu naye anapanga yake. Kanumba alifariki wakati ambao wasanii waliomsukia majungu hayo hawajajisafisha, kama si kumuomba msamaha,” kilisema chanzo.
“Wakati sisi tukipanga yetu, Mungu naye anapanga yake. Kanumba alifariki wakati ambao wasanii waliomsukia majungu hayo hawajajisafisha, kama si kumuomba msamaha,” kilisema chanzo.
KATIBU ASAKWA
Baada ya kunyaka maelezo hayo ya chanzo chetu, mapaparazi wetu walianza kuwatafuta waliokuwa viongozi wa klabu hiyo na kufanikiwa kumpata aliyekuwa katibu msaidizi, Devotha Mbaga, ambaye alikiri kwamba klabu hiyo ina laana ya Kanumba.
Baada ya kunyaka maelezo hayo ya chanzo chetu, mapaparazi wetu walianza kuwatafuta waliokuwa viongozi wa klabu hiyo na kufanikiwa kumpata aliyekuwa katibu msaidizi, Devotha Mbaga, ambaye alikiri kwamba klabu hiyo ina laana ya Kanumba.
HUYU HAPA DEVOTHA
Akizungumza kwa hisia kali maeneo ya nyumbani kwake Kigamboni, jijini Dar, Devotha alisema mgogoro unaoendelea ndani ya kundi hilo ambalo linapumulia mashine baada mwenyekiti wao, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na katibu wake, William Mtitu kujiuzulu ni laana ya Kanumba hivyo wanatakiwa kuomba radhi kaburini kwake.
Akizungumza kwa hisia kali maeneo ya nyumbani kwake Kigamboni, jijini Dar, Devotha alisema mgogoro unaoendelea ndani ya kundi hilo ambalo linapumulia mashine baada mwenyekiti wao, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na katibu wake, William Mtitu kujiuzulu ni laana ya Kanumba hivyo wanatakiwa kuomba radhi kaburini kwake.
Alisema enzi za uhai wa Kanumba baadhi ya wasanii ambao wanagombana
chini kwa chini kwa sasa ndani ya kundi hilo (majina yapo),
walimnyanyapaa na walikuwa wakimchukia na kufikia hatua ya kuwakataza
wanachama wote kutoshiriki kwenye filamu zake.
“Ukweli baadhi ya wasanii hasa hao viongozi wanatakiwa kutambua
makosa waliyomfanyia Kanumba enzi za uhai wake na wamuomba msamaha kwani
walimkosea sana na wakishaomba, naamini Bongo Movie itasimama lakini
wasipofanya hivyo hiyo laana itaendelea kuwatesa na watapigana kila
siku.
“Yaani kuna wakati hadi huwa nafikia hatua ya kusema bora Kanumba
alikufa mapema yawezekana Mungu alikuwa na kusudi lake maana angeaibika
na angeonekana ni mtu asiyefaa katika jamii kutokana na mikakati ambayo
wasanii wenzake walikuwa wameipanga,” alisema Devotha.
KUMBE WALIWAHI KUKAA KIKAO
Kama hiyo haitoshi, katika aya nyingine, Devotha alisema kuna wakati waliwahi kuweka kikao cha kusameheana kilichoandaliwa na Ridhiwan Kikwete ambaye sasa ni Mbunge wa Chalinze kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) lakini mambo bado yakawa ‘shagala baghala’.
Kama hiyo haitoshi, katika aya nyingine, Devotha alisema kuna wakati waliwahi kuweka kikao cha kusameheana kilichoandaliwa na Ridhiwan Kikwete ambaye sasa ni Mbunge wa Chalinze kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) lakini mambo bado yakawa ‘shagala baghala’.
“Nakumbuka kwenye kikao kimoja ambacho aliitisha Ridhiwan Kikwete kwa
ajili ya wasanii na kusema kama kuna mtu amemkosea mwenzake wasameheane
baada ya kuongea na sisi na kuondoka, watu walianza kuongea maneno
mabaya ya kashfa na hapo ndipo walipopanga mikakati ya kumchafua na
kutofanya kazi na Kanumba lakini baada ya siku chache alifariki.
“Hao wanaogombana sasa hivi ndiyo walikuwa vinara katika kumnyanyapaa
Kanumba na ndiyo haohao siku ya mazishi yake ndiyo waliobeba jeneza,
msalaba na kuvaa suti wakati walikuwa hawako naye vizuri, unajua roho
huwa haifi kwa hiyo wanatakiwa kuomba msamaha ili wawe na amani,”
alisema Devotha.
NI LAANA NZITO?
Kwenye mazungumzo hayo na waandishi wetu, Devotha aliendelea kutiririka kuwa kutokana Kanumba kufariki dunia akiwa na kitu moyoni kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna kitu alikizungumza muda mchache kabla hajafariki au kuwa na kinyongo na Bongo Movie hivyo wasanii hao wanatakiwa kwenda kuomba msamaha kaburini kwake ili kundi hilo lisimame tena.
Kwenye mazungumzo hayo na waandishi wetu, Devotha aliendelea kutiririka kuwa kutokana Kanumba kufariki dunia akiwa na kitu moyoni kuna uwezekano mkubwa kwamba kuna kitu alikizungumza muda mchache kabla hajafariki au kuwa na kinyongo na Bongo Movie hivyo wasanii hao wanatakiwa kwenda kuomba msamaha kaburini kwake ili kundi hilo lisimame tena.
WAOMBA RADHI KIMYAKIMYA
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba kuna baadhi ya wasanii wamedaiwa kuanza kwenda kaburini hapo kimyakimya na kuomba radhi ili kundi lao lirudi kwenye mstari kama lilivyokuwa enzi za marehemu Kanumba.
Uchunguzi wa gazeti hili umebaini kwamba kuna baadhi ya wasanii wamedaiwa kuanza kwenda kaburini hapo kimyakimya na kuomba radhi ili kundi lao lirudi kwenye mstari kama lilivyokuwa enzi za marehemu Kanumba.
“Tumeona hali ni mbaya bora twende vinginevyo mambo yataharibika
zaidi ya hapa,” alisema msanii mwenye taito kubwa ndani ya Bongo Movie
kwa sharti la kustiriwa jina.
WENGINE KUOMBA RADHI
Ijumaa lilizungumza na baadhi ya wasanii kwa sharti la kutotaja majina yao ambao walikiri kwamba mambo hayaendi sawa kutokana na laana ya Kanumba hivyo wako mbioni kwenda kuomba msamaha katika kaburi lake wakiamini uliokufa ni mwili roho ingali hai.
Ijumaa lilizungumza na baadhi ya wasanii kwa sharti la kutotaja majina yao ambao walikiri kwamba mambo hayaendi sawa kutokana na laana ya Kanumba hivyo wako mbioni kwenda kuomba msamaha katika kaburi lake wakiamini uliokufa ni mwili roho ingali hai.
KUMBUKUMBU
Marehemu Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 nyumbani kwake, Sinza-Vatcan akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Elizabeth Michael ‘Lulu’. Alizikwa katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
Marehemu Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 nyumbani kwake, Sinza-Vatcan akiwa na aliyekuwa mpenzi wake, Elizabeth Michael ‘Lulu’. Alizikwa katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar.
No comments:
Post a Comment