EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, September 6, 2014

LUNDENGA, MISS TANGA WAZICHAPA


Na Deogratius Mongela
KW/RB/8441/2014 imemshikilia Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga kwa madai ya kuzichapa na Miss Tanga 1997, Mona Faraja ambaye pia ni mke wake na kumsababishia majeraha, Risasi Jumamosi lina ‘full’ stori.
Miss Tanga 1997, Mona Faraja anayedaiwa kujeruhiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga.
Ishu hiyo iliyonyakwa laivu na majirani ilijiri usiku wa Jumatano iliyopita maeneo ya Mbezi Beach jijini Dar, nyumbani kwa Lundenga wakati wawili hao walipokuwa wamepumzika baada ya mihangaiko ya mchana kutwa.Kwa mujibu wa mtoa habari wetu, wakiwa wanabadilishana mawazo, mara simu ya Lundenga iliita na ndiyo chanzo cha mtafaruku, upi huo?

TUJINGE NA CHANZO
Mtoa habari wetu alisema kuwa, tatizo lilikolea mara baada ya simu hiyo kuita mfululizo kwa namba ngeni iliyodaiwa kuwa ni ya ‘kichenchede’ cha pembeni huku bosi huyo akiwa hana mpango wa kuipokea.

Hashimu Lundenga akiwa katika kituo cha poisi cha Kawe.
“Mke wa Lundenga alikuwa na shauku ya kujua nani anayepiga simu ya mumewe muda huo na kwa nini mumewe haipokei lakini wakati akiendelea kujiuliza ndipo ikaingia meseji ambapo inadaiwa Lundenga alikwenda ‘fasta’ kwenye inbox na kuifutilia kwa mbali.
“Kitendo cha kufuta SMS hiyo nacho  kilitibua kabisa hali ya hewa, Mona akataka kujua kwa nini mumewe alikuwa hataki kupokea simu na SMS iliyoingia ilitoka wapi?
“Mona akawa mkali baada ya kuona haridhishwi na majibu ya mumewe ndipo alipoanza kutoa maneno yenye shutuma kwa mzee mzima ambapo naye uvumilivu ulimshinda kama binadamu wengine, wakaanza kutwangana,” kilisema chanzo hicho.

MKE AWAHI POLISI
Chanzo hakikuwa tayari kuweka ‘fullstop’, kiliendelea kumwaga mchele kwenye kuku wengi kuwa, baada ya mke kuona anazidiwa kwa kushushiwa makonde mazito yaliyomvimbisha uso, usiku huohuo  alikimbilia Kituo cha Polisi Kawe, Dar kumripoti mumewe.
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga.
POLISI WAMKAMATA LUNDENGA
Mara baada ya mke kumaliza malalamiko yake kituoni hapo, saa chache baadaye polisi walifika nyumbani wakiwa na difenda ambapo walimchukua mlalamikiwa huyo hadi kituoni kujibu madai hayo.
“Polisi hawakuwa na maneno mengi, walipofika nyumbani walimkamata Lundenga na kwenda kumlaza kituoni kwa ajili ya hatua nyingine za kisheria,” kilisema chanzo.

MAJIRANI WANENA
Baadhi ya majirani waliolitambua sakata hilo walionesha kushangazwa huku wakimhurumia Mona ambaye alikuwa ameumia usoni, hususan mzunguko wote wa jicho la kushoto.

MKE AINGIWA NA HURUMA
Wakati gazeti hili likiwa katika hatua za mwisho kuelekea mitamboni, Mona alidaiwa kuingiwa na huruma kwa kitendo cha kumlaza mumewe kituoni hivyo alikwenda kwa lengo la kumfutia mashitaka.

Hashimu Lundenga akiwa na Miss Tanga 1997, Mona Faraja.
“Mke alimuonea huruma mumewe licha ya kupewa kipondo maana wamedumu kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 10 sasa, si mchezo. Alikwenda Kawe kufuta kesi lakini polisi wakamkomalia kwamba ishu lazima ifike mahakamani,” kilisema chanzo.
Mwandishi wetu alifika kituoni hapo na kukuta polisi na Mona wakiendelea na mazungumzo lakini hadi tunakwenda mitamboni, Lundenga alikuwa bado anashikiliwa kituoni hapo.
MKE WA LUNDENGA
Juzi, Risasi Jumamosi lilimpigia simu Mona kwa lengo la kutaka kumsikia anasemaje kuhusu madai hayo, lakini baada ya maelezo marefu ya mwandishi, alikata simu na baadaye kuizima kabisa!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate