EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 2, 2014

MAMA MCHUNGAJI AJIFUNGUA HIRIZI!

Stori: Shani Ramadhani na Rhoda Josiah
NI maajabu ya dunia! Mke wa Mchungaji wa Kanisa la EAGT ‘Bonde la Baraka’ lililopo Kata ya Kerege Manofu, Bagamoyo mkoani Pwani, Boniface Onesmo Mahera (38) (pichani), Bentha Seth (27) baada ya kubeba mimba kwa miezi tisa  hatimaye amejifungua hirizi, gazeti la kijamii, Uwazi lina mkasa wote.
Mke wa Mchungaji wa Kanisa la EAGT ‘Bonde la Baraka’,  Bentha Seth aliyejifungua hirizi.
Akizungumza na waandishi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita nyumbani kwake, mchungaji huyo alisema mbali na mkewe kujifungua hirizi, pia alitoa mawe mawili, mkaa usiotumika na kitambaa chekundu chenye ukumbwa wa ‘hendkachifu’.

NI MIMBA YA TATU KUTOKA KIMAAJABU
Akisimulia mkasa huo, mchungaji huyo alisema kuwa, awali mkewe alikuwa akipata ujauzito lakini ukifikisha miezi mitatu hutoka.“Tangu mwaka 2009 zimeshatoka mimba tatu kimaajabu. Alikuwa akishika ujauzito, ukifikisha miezi mitatu  unatoka akienda kujisaidia, hali ilikuwa mbaya sana kiasi kwamba tulikuwa tunafanya maombi kila mara na wakati huo wote mimi nilikuwa bado sijasimikwa kuwa mchungaji,” alisema mchungaji huyo.
Hirizi, mawe mawili, mkaa na kitambaa chekundu vinavyo daiwa kutoka tumboni mwa Bentha Seth .
UJAUZITO TAYARI
Akisimulia kilichotokea siku ya tukio, mchungaji huyo alisema mimba hiyo iliyozaa ‘mtoto hirizi’ iliingia Desemba mwaka jana na tangu ilipokuwa na mwezi mmoja walikuwa wakienda kliniki kupima.
“Ikiwa na mwezi mmoja tulikwenda kliniki kupima. Vipimo vilikuwa vikitoa majibu tofauti, mara hana mimba, mara mimba imetunga nje ya mfuko wa uzazi au kugoma kabisa kutoa majibu yoyote. Kwa kweli mke wangu amepitia majaribu mengi.
AOMBA NA KUFUNGA SIKU KUMI
“Basi, tukawa tunaendelea hivyohivyo huku tukiomba na kufunga kwa siku kumi kwa maombi maalum kwa mke wangu na wanawake wengine waliokuwa hawashiki ujauzito. Hatimaye tukamaliza na kusubiria mtoto atakayezaliwa,” alisema mtumishi huyo wa Mungu.
Mchungaji wa Kanisa la EAGT ‘Bonde la Baraka’, Boniface Onesmo Mahera (38).
MAAJABU YAANZA
Baba mchungaji akaendelea kusema kuwa, mimba ilipofikisha miezi sita, mkewe akaanza kupata mauzauza, alianza kutokwa na haja ndogo kila wakati kama vile kuna mtu alikuwa akimmwagia maji.
“Kama hilo halitoshi kila ilipofika saa nane mchana alikuwa akichapwa viboko na mtu asiyemwona jambo lililowapa wakati mgumu zaidi.
AUZA NYUMBA, VIWANJA KUMTIBU MKEWE
Mchungaji huyo alisema baada ya kuyaona hayo aliamua kuuza mashamba na viwanja alivyokuwa navyo sanjari na nyumba aliyojenga Kigoma ili akamtibie mkewe kwa kuamini kuwa  alikuwa akisumbuliwa na Ugonjwa wa Fistula.
Mchungaji akiwa amezungukwa na majirani walioshudia mkasa huo.
Alisema alimpeleka Hospitali ya Comprehensive Community Based Rehabilitation in Tanzania (CCBRT), Msasani jijini Dar ambapo vipimo vilionesha hakuwa na ugonjwa wowote, wakarudi nyumbani na kuendelea na maombi.“Nimeishapoteza karibu shilingi milioni nane kwa ajili kumtibia mke wangu na sasa hivi sina fedha tena na matatizo bado yanaendelea kuikumba ndoa yangu kila kukicha, nina imani shetani aliyeikumba nyumba yangu ataiachia kwa uwezo wa damu ya Yesu,” alisema.
SIKU YA TUKIO, SAUTI YA CHURA KWANZA
Hatimaye siku za mama mchungaji kujifungua ziliwadia, Agosti 19, mwaka huu asubuhi, mwanamke huyo alianza kwa kusikia sauti ya chura ikitokea tumboni ndipo saa tatu usiku alishikwa na uchungu huku mumewe akiwa na shilingi 1,500 tu mfukoni pesa ambayo haikuwa ikitosha hata usafiri wa kwenda hospitali.
Cheti cha ndoa baina ya Bentha Seth na mchungaji huyo.
“Nilifanya maombi mazito na kumtayarishia mkewe wangu sehemu ambayo atajifungulia hapahapa nyumbani, cha ajabu muda wa kujifungua nikashangaa kumwona anatoa haja ndogo kama ujazo wa lita kumi. Nikiwa naendelea kufanya maombi tumbo lilijaa na kupungua, ilibidi nimfunge kitambaa na mpira wa tairi la baiskeli ili tumbo lipungue.
“Kwa hatua aliyokuwa amefikia mke wangu  nilijua anaaga dunia kwa sababu niliisha kinga ndoo nne zilizokuwa zimejaa haja ndogo na hakukuwa na hata tone moja la damu.
“Ilipotimu saa sita usiku mke wangu akaanza kulalamika huku akisema anakufa, mara nikaona kitu kimechomoza, akasema nisaidie basi, nilipochungulia nikaona uzi, nikapeleka mkono kuuvuta, ikawa kama tunavutana lakini nilifanikiwa kuvuta ndiyo nikatoa hirizi lakini sikumwambia nilichokiona na muda huohuo yeye alipoteza fahamu.
“Kwa sababu ilikuwa kitu cha ajabu sana kwangu, nilitoka kwenda kuwaita majirani zangu ili waje washuhudie kilichotokea kwa mke wangu. Walikuja na kumkuta bado amepoteza fahamu.
“Alipokuja kuzinduka alianza kunidai mtoto ikabidi nimwambie ukweli mbele ya majirani. Niliichukua ile hirizi nikaifungua nikakuta ndani kuna kitambaa chekundu, mawe, mkaa na manyoya, nikaviombea na kuvichoma moto.
“Haya yote naona ni majaribu ya shetani tu na ninasema hili ni jaribu lake la mwisho haitatokea tena na kama ikitokea basi nitamteketeza huyo shetani kwa maombi,” alisema mchungaji huyo.
MAMA MCHUNGAJI SASA
Kwa upande wake, mama mchungaji huyo alisema anamshukuru Mungu kwa majaribu yote aliyopitia na kuamini ni sehemu ya maisha lakini kubwa ni uzima alionao mpaka sasa.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate