EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, September 12, 2014

PEPO WA AJALI NI AHUYU HAPA

Stori: Ojuku Abraham HAKUNA lugha nyingine ya kusema zaidi ya kuainisha kuwa pepo wa ajali za barabarani zinazoua mamia ya watu ni uzembe wa kutisha unaofanywa na madereva katika uendeshaji magari bila utii wa sheria.                          Basi la Mtei Express likiovateki wakati kuna magari mawili yanakuja kwa mbele.
Uchunguzi wa Gazeti la Ijumaa uliofanywa hivi karibuni katika maeneo mbalimbali nchini umebaini kuwa, mbali na mwendo kasi unaotajwa mara kwa mara kuwa unachangia ajali, suala la kutozingatia sheria za usalama barabarani ni hatari zaidi.

Picha za magari ya abiria yaendayo mikoani zilizotumika ukurasa wa nyuma wa gazeti hili ni kielelezo tosha kuwa madereva wengi hawajui sheria za usalama barabarani au wanazivunja makusudi jambo ambalo husababisha kutokea kwa ajali nyingi za magari kugongana uso kwa uso.
Mabasi manne yakiovateki lori kwa wakati mmoja.
Katika ajali kubwa na mbaya iliyotokea wiki iliyopita mjini Musoma na kuua zaidi ya watu 40, ilitokana na mabasi mawili ya J4 na Mwanza Coach kugongana uso kwa uso katikati ya daraja; kukosa umakini kwa madereva ni chanzo.
Uamuzi wa kizembe kama huo na ule unaonekana katika picha zilizobeba habari hii ambapo madereva wa magari husika wanaonekana ‘kuovateki’ kinyume cha muongozo wa uendeshaji.Sheria zinamkataza dereva kulipita gari jingine kwenye mlima, mteremko mkali na  mahali penye kona, lakini kwa mshangao madereva wengi wamekuwa hawazingatii hilo.
Basi likiovateki wakati mbele kuna kona.
“Ukisafiri hasa kwenye barabara kubwa kuna alama zinazokuongoza, lazima dereva uzifuate, lakini madereva wetu hawafanyi hivyo, inawezekana hawajui sheria au wanapuuza kwa sababu adhabu zetu ni nyepesi tofauti na nchi nyingine kama Rwanda,” alisema Mohammed Mpinga, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini katika mahojiano na gazeti hili hivi karibuni.
Hata hivyo, mbali na uvunjifu huo wa sheria, uchunguzi wetu umebaini kwamba madereva wengi wamekuwa wakiendesha magari huku wakiwa wamelewa pombe na hivyo kuwafanya wakose umakini.
Mbali na ulevi baadhi ya madereva wa mabasi yaendayo mkoani wamekuwa wakiendesha kwa mashindano ya kuwahi kufika waendeko ili wasifiwe na abiria kuwa wamewawahisha jambo ambalo mwishowe kuwahi huko huwatokea puani na kuwasababishia ajali.Taarifa ya polisi inaonesha kwamba kwa mwaka jana pekee kulikuwa na ajali 23,842, kati ya hizo ni za mabasi 931, zilizoua watu 313.
Gazeti hili linampongeza Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe kwa hatua anazochukua kuyafungia makampuni ambayo mabasi yake hupata ajali za kizembe na kwamba tunatoa mwito kwa polisi wa usalama barabarani kusimamia sheria ipasavyo ili pepo wa ajali atoweke nchini.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate