EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, September 10, 2014

UKIFANYA KAMA HUJALI, HUTASUMBUKA!

KUNA kelele nyingi sana kutoka kwa akina mama, wakilia kutendwa na wenza wao. Nimewahi kukutana nao wengi sana, wakilalamika na ukijaribu tu kuwagusia kuhusu nia yako ya kutaka urafiki nao, utawasikia: “Weee, tena sitaki hata kumsikia mtu anaitwa mwanaume.”
Na unapotaka kujua kulikoni, atakupa simulizi ndefu juu ya uhusiano wake wa kimapenzi ulivyokatishwa ghafla na mwenza wake kutokana na sababu mbalimbali, lakini kubwa huwa ni kukosa uaminifu.
Ninataka kuwapa siri, siyo tu wanawake, bali hata wanaume.Wakati mwingine tunajiumiza mioyo yetu sisi wenyewe, kwa sababu tunatumia muda mwingi kujipa mawazo ambayo yanatuondolea furaha tunayopaswa kuwa nayo kwa muda mwingi.
Kufikiri sana kuhusu mwenza wako ni ugonjwa ambao mwenye uwezo wa kuutibu siyo mwingine zaidi yako. Na ugonjwa huo unatokana na kosa ambalo wewe ulilifanya siku ile ya kwanza ulipoamua kuanzisha uhusiano wa kimapenzi naye.


Kuna wanawake wanasema wanaume ni waongo sana, kwamba watakudanganya kwa maneno matamu, lakini wakishakupata wanabadilika. Huwa napinga sana msemo huu, siyo kwa sababu mimi ni mwanaume, bali kwa sababu hayana ukweli wowote.
Wanaume siyo waongo isipokuwa hivi ndivyo tulivyoumbwa. Mungu alimfanya mwanaume ampate mwanamke kwa vishawishi, ndiyo maana wanaojaribu kutumia nguvu sheria inawakabili. Vishawishi hivi viliumbwa, tatizo huwa jinsi gani mwanamke anavyovipokea!Hata wewe mdada, mwanaume anapokusimamisha njiani, anapoanza kukusemesha mkiwa garini au popote pale, unajua kabisa huyu sasa anaanza kubwaga sera, unajua kabisa atakushawishi ili ukubaliane naye hatimaye uwe wake.
Kwa maana hiyo, wakati unamsikiliza, akilini mwako unajua kama anafanana na anachokisema au la. Ndiyo, kuna watu wanafanana na wengine hawafanani kabisa. Kwa mfano, mtu atakuambiaje atakununulia gari wakati mmekutana kwenye daladala?
Maana yangu ni kuwa unaweza kumkubali mwanaume siyo kwa sababu ya kuamini anachokisema, bali kwa vile tu, wewe mwenyewe umevutiwa naye pia. Kwani uongo, hata wanawake nao si wanapenda kama wanaume walivyo?
Siku ya kwanza ya kumsikiliza, unakuwa pia umeshamuelewa. Unapomkubali, maana yake ni kuwa uko tayari kwa lolote, hasa baya. Niwape angalizo, mara zote fikiria sana kuhusu kutendwa kuliko mazuri, kwa sababu ukishajiweka tayari kiakili kwa jambo hilo kutokea wakati wowote, wala hutapata taabu.
Na tena, namna nzuri ya kujiweka mbali na stress za kutendwa, wewe ni kujifanya kutojali. Ukiona siku hizi amebadilika, kama alikuwa mtu wa kukupigia simu kila saa na sasa anapiga mara mbili au tatu tu kwa siku, uchune!
Ukiona labda amepunguza mashamsham, muulize maana huenda kweli umemkera, lakini akijifanya kutingisha kichwa na kuendelea na shughuli zake, achana naye.
Amini nakuambia, atakapokuona huna presha, mwenyewe atajishtukia, atajiuliza, mbona huyu siku hizi kama hana habari vile, ana mtu nini? Utashangaa kuona yeye ndiyo anakuja kwako na kulalamika kuwa siku hizi umebadilika!
Lakini nirudie tena kuwaasa, kuweni waangalifu sana siku ya kwanza mnayokata shauri la kushiriki mapenzi na mtu, ndiyo siku inayoshikilia matumaini yako ya baadaye, ni bora kusubiri kuliko kuharakia karaha!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate