EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, October 21, 2014

ALIYEUAWA NA KOMANDOO WA JWTZ MSIBA WAKE WAZIZIMA

Stori: Makongoro Oging’na Haruni Sanchawa
INAUMA sana! Baadhi ya ndugu waliokuwa wakiuaga mwili wa Aron Kihundwa (28) kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar walijikuta wakidondoka na kuzimia kufuatia uchungu wa kumpoteza mpendwa wao huyo aliyedaiwa kuuawa na Komandoo wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Octavian Mgowele.
Aron Kihundwa akiwa mahututi hospitali kabla ya kifo chake.
Tukio hilo lilijiri wiki iliyopita na kumfanya Mchungaji  Elaina Msuya wa Kanisa la KKKT aliyekuwa akiongoza misa ya kumuombea marehemu huyo, kuingilia kati na kusema mwili usiendelee kuagwa ili kuzuia watu kuzidi kuzimia.
Komandoo Octavian Mgowele mwenye cheo cha Luteni wa Kikosi cha 94 KJ Ngerengere, Morogoro, Oktoba 13, mwaka huu alidaiwa kumuua Aron kwa kumpiga kipigo kibaya.Tukio hilo lilidaiwa kutokea kwenye baa iitwayo Mbondela iliyopo Yombo - Buza maeneo ya Kipera, jijini Dar kwa madai kwamba alikuwa akimbughudhi mke wa komandoo huyo.
Taarifa toka kwa mtu aliyekwepo kwenye baa hiyo zinasema siku hiyo mjeshi huyo alikaa meza moja na mkewe ambaye alitoka kufunga naye ndoa jana yake. Pia kwenye meza hiyo  alikaa Aron huku wakiendelea kunywa bia ambapo mnunuaji mkuu alikuwa komandoo.
Marehemu Aron Kihundwa enzi za uhai wake.
Ikadaiwa kuwa, kuna wakati komandoo alikwenda kaunta aliporudi alishangaa kumkuta mkewe amehama katika kiti alichomuacha.Chanzo hicho kikaendelea kusema komandoo huyo alimuuliza mkewe kisa cha kuhama kiti, naye akamjibu; si huyu rafiki yako ananisumbua.’
Wakati huo, marehemu alikuwa anauchapa usingizi kutokana na kulewa.
“Marehemu akiwa usingizini alishtukia komandoo akimwadhibu bila kujua sababu ni nini hadi akamjeruhi.

”Baada ya kumpiga sana hadi kumjeruhi tulimchukua marehemu na kumpeleka Kituo cha Polisi Chang’ombe (Dar) na kupewa PF3, tukamkimbiza Hospitali ya Temeke,  ilipofika saa kumi usiku wa kuamkia kesho yake alifariki dunia.
“Aron ni rafiki yake sana komandoo, hata siku ya ndoa yake, yeye ndiye aliyempambia gari la harusi na ukumbi. Siku ya tukio ilikuwa ni sherehe ya kuvunja kamati.
“Hatujajua ni kwa nini komandoo aliamua kumpiga Aron kiasi kile, mambo ya kuambiwa na mwanamke siyo ya kuyafanyia kazi kama haukushuhudia ama hauna uthibitisho,” alisema shuhuda huyo.
Marehemu Aron alizikwa Oktoba 18, mwaka huu kijijini kwao Kyengia Wilaya ya Siha mkoani Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate