EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, October 24, 2014

DIAMOND KUFUNGWA JELA MIAKA MITATU!

Na Musa Mateja
Kufuatia tukio la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuonekana jukwaani na sare zinazoaminika kuwa za Jeshi la Wananchi (JWTZ) kisha kukamatwa kwa kundi lake la Wasafi Classic Baby (WCB) na meneja wake, Babu Tale, kuna uwezekano wa jamaa huyo kufungwa jela miaka miwili au mitatu.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akisubiri zamu yake kupanda jukwaani.
Kwa mujibu wa chanzo chetu ndani ya jeshi la polisi, baada ya jeshi kutoa tamko kuwa ni kinyume cha sheria, juzi Diamond alitakiwa kwenda kujisalimisha polisi lakini hakufanya hivyo jambo lililosababisha wenzake kukamatwa na kuwekwa nyuma ya nondo za mahabusu ya Oysterbay, Kinondoni jijini Dar.

Ilisemekana kwamba baada ya Wasafi (madensa wa Diamond) kukamatwa, Babu Tale naye alifikishwa katika kituo hicho ambapo maafisa kadhaa wa jeshi la polisi walionekana katika eneo hilo wakiweka ulinzi mkali.

Madensa wa ‘Diamond Platnumz’ wa kundi la Wasafi Classic Baby (WCB) wakisindikiza shoo yake.
Chanzo hicho kilieleza kwamba, siku ya tukio Oktoba 21, mwaka huu, uongozi wa Diamond ulipewa muda wa kujieleza kabla ya saa 2:00 asubuhi lakini haukufanya hivyo ndipo hatua hiyo ikachukuliwa.
Hata hivyo, baadhi ya watu walikuwa wakihoji kwa nini jeshi la polisi lilimshikilia Babu Tale peke yake bila Diamond lakini vyanzo vilieleza kuwa mwanamuziki huyo huenda alikuwa safarini.
Diamond akiendelea kutoa burudani jukwaani.
Ilielezwa kwamba wanaomsaka Diamond na waliowakamata Wasafi ni wanajeshi wa Military Police (MP) ambao waliwabwaga jamaa hao kituoni hapo kisha kuendelea na mambo yao.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Dar, Camillus Wambura alisema bado hajawasiliana na kituo cha Oysterbay kuhusu suala hilo na hajapata taarifa kwa kuwa kesi hiyo inachunguzwa na iko chini ya Mkuu wa upelelezi wa Mkoa.
Akijibu kuhusu taarifa za uongozi wa Diamond na Diamond kupewa muda wa kujieleza, Kamanda Wambura alijibu:
Diamond Chege wakifanya yao.
“Uchunguzi unafanywa huko (Oysterbay). Kwa sasa hivi sina taarifa hiyo nina mambo mengi sana. Kwa hiyo kwa sasa hivi uchunguzi unafanywa chini ya Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa. Sijapata nafasi ya kujua wamefikia wapi katika uchunguzi wa suala hilo.”
Mapema wiki hii, Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) lilitoa taarifa kwa vyombo vya habari likipiga marufuku raia kuvaa sare za jeshi.
Kwa mujibu wa mwanajeshi wa JWTZ ambaye aliomba hifadhi ya jina kwa kuwa si msemaji wa jeshi hilo, taaluma yake ya sheria imemfanya kuchimba kwa undani suala hilo na kugundua kuwa endapo Diamond atapatikana na hatia atapigwa faini au kwenda jela miaka miwili au mitatu au vyote, yaani faini na kifungo.
Alisema kosa la Diamond ni kushindwa kutii wito kwani alitakiwa kuripoti mwenyewe polisi hivyo lazima atapanda mahakamani kujibu shitaka hilo na lile lenyewe la kutumia sare za jeshi hilo.Chanzo hicho kilidai kwamba si mara ya kwanza kwa jamaa huyo kuingia kwenye kashikashi kama hiyo kwani kuna kipindi alikwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ambapo alionekana na sare hizo stejini na akapewa onyo lakini safari hii amejiongeza tena kuonesha kuwa ni kichwa ngumu.
CREDIT:GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate