MSANII
 nyota wa muziki wa Bongo Flava nchini, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ 
huenda akaingia matatani baada ya juzi kupanda jukwaani kutumbuiza 
katika Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 akiwa amevaa sare ya Jeshi la 
Wananchi Tanzania (JWTZ), kinyume cha sheria.
Tangu
 msanii huyo afanye hivyo, mjadala umeibuka kwa wengi wao kujiuliza nini
 maana yake na kama alifanya hivyo kwa kibali maalumu au la, hasa 
ikizingatiwa ni hivi karibuni Jeshi hilo lilitoa onyo kwa wasanii na 
wengineo kutotumia mavazi hayo.
Mbali
 ya Diamond, hata vijana wake nao walishambulia jukwaa wakiwa katika 
mavazi hayo, akiwemo msanii aliyemshirikisha katika moja ya nyimbo zake,
 Ney wa Mitego.
Wakati
 shoo hiyo ikiendelea, baadhi ya mashabiki walianza kumzomea kila 
alipoimba kabla ya video kubwa ambazo zilikuwa mbele ya jukwaa hilo 
kuanza kuonyesha picha za mnato na video za mwanamuziki huyo akiwa 
amevaa mavazi hayo huku akiwa kama askari ‘anayekoki’ risasi katika 
katika bastora na baadaye katika bunduki ya kivita.
Kitendo
 hicho, kilionekama kuwakera zaidi maelfu ya wapenzi na mashabiki wa 
muziki waliokuwa wamejazana katika viwanja vya Leaders Club, huku kila 
mmoja akiwa na tafsiri yake.
Baada
 ya tukio hilo la juzi usiku, kitendo cha nyota huyo kuvalia mavazi hayo
 ya JWTZ, kimeibua mjadala hadi katika mitandao ya kijamii kuanzia jana 
asubuhi, ambapo picha za msanii huyo zikitumika kujenga hoja ya uhalali 
wa kufanya hivyo, huku vijana kadhaa wanaokutwa nazo mitaani wakiteswa 
vibaya na jeshi hilo.
Kwa
 upande wake Diamond, alitoa taarifa ndefu katika ukurasa wake wa 
Facebook na Instagram, akiishia kuelezea ni kwa nini alizomewa katika 
shoo hiyo.
Tanzania
 Daima ilipomtafuta Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camilius 
Wambura juu ya kitendo cha msanii huyo, alisema alikuwa hajui chochote 
na kuahidi kulifanyia kazi kama atapelekewa taarifa na wasaidizi wake.
Alipotafutwa
 Kaimu Msemaji wa JWTZ, Meja Joseph Msanja, simu yake iliita bila 
kupokelewa na alipotafutwa msaidizi wake, alikiri kupata taarifa na 
kujionea kupitia shoo hiyo, huku akisisitiza bosi wake anaweza 
kulizungumzia hilo.
Tukio
 hilo limefanyika ikiwa ni siku chache tu tangu kijana mmoja aliyekuwa 
amevalia mavazi ya kijeshi maeneo ya Kariakoo, jijini Dar es Salaam, 
kuvuliwa na kupewa adhabu ya kuogelea katika dimbwi la maji machafu 
yaliyotuama.
Aidha,
 msanii Gwamaka Kaihula ‘Crazy GK’ aliwahi kuhojiwa na Jeshi hilo kwa 
kutumia mavazi ya kijeshi katika kibao chake cha Simba wa Afrika, ambapo
 alijitetea pamoja na kuomba msamaha kwa kilichofanyika.
Kutokana
 na wimbi la watu mbalimbali hasa wasanii kuvalia mavazi yanayofanana na
 sare za jeshi hilo, hivi karibuni Kurugenzi ya Habari na Uhusiano Makao
 Makuu ya JWTZ, ilionya kama ifuatavyo:
ilifafanua taarifa hiyo.


No comments:
Post a Comment