EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 22, 2014

WEWE SIYO MZURI? NANI KAKUDANGANYA!

BINADAMU tumeumbwa kwa namna tofauti sana, ingawa kibaolojia, wote tuko sawa, bila kujali kama ni Wahindi, Waarabu, Wazungu, Waafrika, Wachina na makabila yote, siyo warefu, wafupi, wembamba wala wanene.
Tunatofautiana akili, uwezo wa kuelewa, uwezo wa kukabili changamoto na hata jinsi ya kuishi kwenye jamii inayotuzunguka. Kuna watu wengine hawaamini kama wao wako vile walivyo kwa sababu yao wenyewe, bali wanamsingizia Mungu.

Mungu alituumba wote tukiwa na akili, kinachotokea ni kujiongeza tu, kwa elimu ya darasani na hata ya mtaani, lakini ukifunua kichwa changu, utakuta kina kila kitu ambacho kipo kichwani mwa Steve Jobs, yule bilionea namba mbili duniani.
Ndivyo pia tulivyo hata katika maisha ya uswahilini. Unashangaa watoto wawili wa kiume wamezaliwa kwa wazazi walewale, lakini staili ya maisha yao ni tofauti kabisa, mmoja ni mpole na mtanashati, mwingine ni mtukutu asiyekamatika.
Kuna wengine kutokana na hali ya maisha yao, wanaamini kwamba wao ni wabaya kiasi kwamba hawawezi kupata wenza wenye maana. Hivi, hebu jaribu kufanya utafiti wako mwenyewe mdogo. Mchukulie msichana mwenye sura ya kawaida tu lakini anayeishi katika familia bora anavyokuwa.
Atatumia uwezo wa wazazi wake kufanya shopping ya maana na atajiremba sana kiasi kwamba ataonekana ni mrembo kuliko msichana kutoka familia iliyochoka ambaye ana uzuri wa asili, lakini uwezo wake duni kifedha, unamfanya ashindwe kujifanyia manjonjo.
Vivyo hivyo kwa wavulana, wapo wenye miili iliyopendwa na akina dada, lakini kutokana na ufukara wao, wanashindwa kujitokeza mbele ya wasichana wazuri kwa sababu hawawezi kusikilizwa, hasa katika kipindi hiki ambacho ni cha hapendwi mtu isipokuwa pochi.
Lakini mvulana mwenye sura isiyovutia, aliyetoka familia bora atavaa mavazi ya gharama yatakayomfanya aonekane handsome na wadada watamkimbilia, naye hakika atajiona ni mzuri.
Kitu tunachoweza kujifunza kutokana na hali hii ni kwamba siku hizi mapenzi hayaangalii sana wajihi wa mtu, bali hali yake.
Upande wowote ambao fedha inahusika, ndiyo ambao una nafasi kubwa ya kupata mapenzi yenye uhakika, wakati upande wa pili kidogo hali huwa siyo rahisi. Hapa ndipo baadhi yetu tunapokosa ujasiri hadi kujikuta tunakimbilia kwa binadamu wenzetu, tuliowapa jina la waganga na kuamini kuwa wanaweza kutusaidia kuwapata wenza!
Wapo ambao maisha yao ya kimapenzi yamewafanya wajione kama wenye mikosi, wamejikuta wakiamini kwamba wao ni wabaya na kwamba hawana bahati. Kama wewe ni mmoja wa watu hawa, safu hii ya leo itakuwa ni nzuri sana kwako.
Wapo baadhi ya ndugu zangu, wake kwa waume wamekuwa wakinipigia simu na kunieleza jinsi maisha yao ya kimapenzi yalivyotawaliwa na kile wanachosema kuwa ni mikosi, kwamba kila baada ya muda mfupi, wapenzi wao ama wanageuza njia au lolote ambalo huliweka penzi lao katika hali ya sintofahamu.
Kwanza ni lazima tufahamu kwamba katika mapenzi, hakunaga mtu mzuri wala mbaya.
Wengine wanajidanganya kwamba wao ni warembo kuliko wenzao. Hapana, mapenzi ni hisia. Kila mtu ana hisia na kwa maana hiyo, yeyote anaweza kumpata mwenza. Kinachotufanya tujione kuwa na mikosi ni kwamba achilia mbali matatizo yetu ya kibinadamu, lakini pia huenda wenza tunaowachagua, hawana hisia kwetu. Usidhani urembo wa sura na umbo ni kitu pekee kinachoweza kumfanya mtu avutiwe na wewe. Ni zaidi ya hapo.
Ndiyo maana hushangai kwa nini wenzetu wenye ulemavu, uwe wa viungo au ngozi, mbona na wenyewe wana watu wao? Kama mapenzi yangekuwa siyo hisia, hawa wasingepata wenzao kwa sababu watu wangeogopa ulemavu wao.
Kuna watu wana magonjwa yao, mtu mwingine anapenda matiti makubwa au madogo, akimuona mwanamke aliyenayo, hajali, hata kama hana miguu!
Ndiyo maana nimekwambia, acha kujiona mwenye mikosi, isipokuwa tambua bado hujampata mtu ambaye anaendana na wewe kwa hisia. Ni kujidanganya kumtafuta kwa waganga wa kienyeji!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate