EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 18, 2014

MUHIMBILI VIFO NJE NJE KISA DAWA HAKUNA

Stori: Haruni Sanchawa na Makongoro Oging’I NATISHA! Uhaba mkubwa wa madawa, ongezeko la ada ya kitanda na chakula katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, umesababisha watu wengi kupoteza maisha kufuatia wagonjwa kukosa huduma na hivyo kurejea majumbani mwao.
Baadhi ya wagonjwa wakiwa katika moja ya wodi za Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa baada ya Bohari Kuu ya Madawa (MSD) kusitisha kutoa dawa kwa hospitali hiyo kubwa ya serikali kufuatia deni kubwa, wagonjwa hasa wenye uwezo mdogo wamelazimika kuingia mitaani na kuombaomba kwa wasamaria wema ili waweze kunusuru hali zao.

Katika wodi ya wagonjwa wa moyo, walilalamikia bei kubwa ya matibabu inayowafanya wasio na uwezo na wasio na ndugu kuishi kwa kubahatisha. “Hali ni mbaya sana hapa, jana nimeshuhudia wagonjwa wenzetu wawili wanapoteza maisha kwa sababu hawahudumiwa tokea majuzi kwa vile hakuna dawa, na tunasikia hata huko katika mawodi mengine hali ni ya hatari kabisa,” alisema mgonjwa mmoja aliyeomba hifadhi ya jina lake.
Moja ya jengo la Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Katika wodi ya wazazi, kulikuwa na ukosefu wa vifaa tiba kama vile pampas na wagonjwa wengi walionekana kujirundika pamoja, huku familia zisizo na uwezo, inakuwa vigumu kupata huduma, hasa kwa mzazi aliyejifungua.
Hali ilikuwa hivyo pia katika majengo mengine, likiwemo lile la watoto, ambako wagonjwa walionekana kuwa ni wengi kuliko wauguzi, kwani wakati kwa wastani muuguzi mmoja anapaswa kuhudumia wagonjwa kati ya 5-8, hapo muuguzi mmoja alijikuta akihudumia hadi wagonjwa 60.
Hata duka la dawa lililo chini ya hospitali hiyo, nalo lilionekana kama urembo tu, kwani kila aliyeandikiwa, alilazimika kutoka nje kwenye maduka binafsi.
Mmoja ya wagonjwa wakiwa hospitalini hapo. 
Katika wodi ya Mwaisela ambayo ina wagonjwa mseto wakiwemo wa vinywa, uvimbe, ajali za moto na kadhalika, ukosefu wa dawa ulileta tishio kubwa, hasa kwa mlipuko wa magonjwa ya kuambukizwa.
Kwa wagonjwa waliotakiwa kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi, waliambiwa kurejea majumbani hadi hapo watakapoitwa kwa simu baada ya serikali kupata fedha.
Huduma ya maji pia ni tatizo lingine linalowakabili wagonjwa waliopo hospitalini hapo, kwani kwa wasiokuwa na uwezo wa kununua maji ya chupa, inawawia vigumu kuyapata kutoka Dawasco.
Vinginevyo wanapaswa kuyatumia yanayotoka katika kisima kilichopo hospitalini hapo, ambacho hata hivyo maji yake yanaelezwa kuwa na chumvi.
Wagonjwa wakinamama wakiwa katika moja ya wodi za Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Katika chumba cha kuhifadhia maiti, uchunguzi umebaini hali ni mbaya zaidi, kwani wafiwa hulazimika kwenda kununua wenyewe dawa kwa ajili ya kuwahifadhi maiti wao. Pia ndani ya chumba hicho, zipo maiti za muda mrefu zinazohusu Chuo cha Kitabibu cha IMTU ambazo zimehifadhiwa hapo na hivyo baadhi ya watu kuomba serikali kuruhusu kuteketezwa kwa miili hiyo.
Afisa uhusiano mkuu wa Hospitali hiyo, Emaniel Eligalesha alisema matatizo yote yanayohusu  hospitali hiyo yatashughulikiwa muda mfupi ujao.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dkt. Seif  rashid akifafanua jambo.
Kaimu Mkurugenzi wa MSD, Cosmas Mwaifwani alisema kutokana na deni kubwa la serikali, inakuwa vigumu kwao kukomboa kontena za dawa zilizokwama bandarini Dar es Salaam. “Hili tatizo la serikali kudai kodi kwa dawa zinazotolewa na wafadhili kutoka nje kunawakatisha tamaa, kwani kuna dawa zingine hazifai kutozwa kodi zikiwemo zile za waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi zikiwemo Kondom, hali hii inaweza kuwafanya wafadhili wasitishe kutoa misaada mbalimbali kwa vile ile inayotolewa haiwafikii wananchi kwa wakati,” alisema Mwaifwani na kuwafanya wagonjwa wengi kuondoka kwa vilio.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate