ALIYEKUWA mwakilishi wa Tanzania katika Big Brother Africa Hotshots, Irene Laveda wiki hii alikuja na kufanya mazungumzo katika chumba chetu cha habari.Katika mahojiano maalum, Irene alizungumza mambo mbalimbali kama alivyonukuliwa na Global tv online.
Kwa sasa msichana huyo amedhamiria kufanya kweli katika muziki na filamu ili kujiimarisha kisanaa. Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano hayo ambayo pia yanapatikana katika tovuti ya www.globaltvtz.com. ; Mwandishi: Safari yako kuelekea Big Brother Africa ilikuwaje?Laveda: Nilienda kwenye usaili kama watu wengine na tulikuwa wengi sana, wengine watangazaji maarufu, nilichaguliwa kutokana na kuwa na sifa zote.
Mwandishi: Vipi kuhusu video yako iliyonaswa ukijichua?
Laveda: Sijawahi kufanya hivyo wala kufanyia mtu mwingine, hapa kinaongelewa kitu ambacho hakijaonwa, mimi niko hapa wiki ya ngapi sijui, hizo video zinatafutwa hazijapatikana, sidhani kama kweli Big Brother watazuia kuonesha hizo clips, waliokuwa wananiongelea mimi wanatoka nchi zingine na alishaniona nina kipaji tokea siku ya kwanza, nilikuwa nina asilimia 85 na kiongozi na ukiwa kiongozi lazima utakuwa ‘nominated’.
La Veda akiwa na Saxaphone yake wakati akifanyiwa Exclusive Interview kwenye studio za Global TV Online jana.
Mwandishi: Je, kushiriki Big Brother ni udhalilishaji? Laveda: Huu ni mwaka wa tisa sasa mashindano haya yanafanyika na hayawezi kufanyika bila nchi husika kuruhusu, ingekuwa ni udhalilishaji yasingefanyika, maana tunapokwenda pale tunawakilisha nchi isipokuwa pale unakuwa kikazi na kutumia kipaji chako kwa sababu yale ni mashindano.
Mwandishi: Kuna changamoto gani Big Brother?
Laveda: Changamoto zipo, kuna vitu vingi watu wanakwambia kabla hujaingia, lakini ukiingia unakuta vitu tofauti kabisa.
La Veda akipozi na mama yake mzazi, Mecky Vedastous ndani ya studio za Global TV Online zilizopo ndani ya Global Publishers.
Mwandishi: Mtu anawezaje kupata nafasi ya kushiriki katika jumba hilo? Laveda: Mtu yeyote anayeamini ana vigezo anaweza kwenda, unafanya usaili kama watu wengine wamefanya zaidi ya mara moja na wakafauli mara ya tatu, mashindano hayana kanuni kwa hiyo nawasapoti vijana wote wanaotaka na wazazi wao wawasapoti kwa sababu hakuna kitu kibaya pale ili mradi uwe umezidi miaka 21 na unajitambua.
Mwandishi: Unamzungumziaje Miss Tanzania 2014 ambaye amevua taji kwa tuhuma za kudanganya umri?
Laveda: Nimekuwa ‘surprised’ sana, nimetoka ndiyo nikasikia Miss Tanzania yuko na furaha lakini sijaelewa kwa nini taji limechukuliwa kwa sababu ya umri wake, miaka 23 - 25 bado ni mdogo na ana sifa zote na Miss World, bado anaenda akiwa na umri hata miaka 26-27, pia ningependa kusema vyombo vya habari vya Tanzania vinatakiwa kupromoti zaidi uzalendo.
Mwandishi: Vipi kuhusu kufanya shoo yako ya Reality?
Laveda: Niko kwenye mpango huo lakini ni baadaye, kwa sasa nataka kufanya kazi zangu za muziki na filamu kwanza.
Mwandishi: Wewe ni mpenzi wa mpira wa miguu?
Laveda: Ndiyo. Mimi ni mpenzi wa Kombe la Dunia, Twiga na Taifa Stars zote nazipenda, nasapoti pia Yanga na Simba japo bado sijazijua vizuri lakini nje ya hapo naipenda timu ya Ghana, inajitahidi, nina matumaini na Tanzania tutafika kombe la dunia tukiweka juhudi.
No comments:
Post a Comment