EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, November 5, 2014

SITTI MTEMVU ATOWEKA

WAKATI suala la kudaiwa kudanganya umri likiwa bado ‘bichii’, taarifa zinadai kuwa mshindi wa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu ametoweka na hajulikani alipo, Risasi Mchanganyiko limechimbua stori kamili.
Mshindi wa Miss Tanzania 2014, Sitti Mtemvu.
Shughuli ya kumsaka mrembo huyo ili kujua undani wa sakata lake ilianzia Temeke ambako ilielezwa kuwa ndiko anakoishi.
Mapaparazi wetu walipofika katika nyumba waliyoelekezwa, walikuta imebadilishwa na kuwa Ofisi ya Vikoba ambapo mmoja wa wahudumu wa ofisi hiyo kwa sharti la kutoanika jina lake gazetini, aliwataka waandishi wetu kwenda Mbezi-Makonde akidai ndiko anakoishi kwa sasa.
“Hapa ilikuwa nyumba ya zamani lakini kwa sasa ni ofisi na Sitti hakai hapa, kama mnamtaka nendeni Mbezi-Makonde huko nasikia ndiko anakoishi,” alisema mtumishi huyo.
Mapaparazi wetu hawakuchoka, walifunga safari hadi Mbezi-Makonde ambapo walikuta nyumba yenye maduka yaliyoandikwa Mtemvu Foundation, wakaenda moja kwa moja katika saluni mojawapo iliyokuwa na bango lililosomeka Malisa huku likiwa na picha ya Sitti sambamba na namba za simu.
Sitti Mtemvu wakati wa kutwaa taji la Miss Tanzania 2014.

Dada mmoja aliyeonekana kufanana na Sitti alizidi kutibua hali ya hewa baada ya kusema Sitti amesafiri nje ya nchi pasipo kufafanua nchi gani.“Sitti amesafiri nje ya nchi, ila kama mnamtaka nafikiri nitawapa namba zake akirudi kati ya Jumatatu au Jumatano ya wiki ijayo (wiki hii),” alisema dada huyo pasipo kutaja jina lake.
Mmoja wa majirani wa mrembo huyo alihoji inawezekanaje mrembo huyo akasafiri nje ya nchi wakati suala lake la umri halijapata ufumbuzi?“Mh! Ataondokaje wakati bado ana majanga ya umri?” alihoji jirani huyo.
Aidha, mapaparazi wetu hawakutaka kuishia hapo, Jumapili iliyopita walitia timu Buza Kipera katika Kanisa la The Revelation Church la Nabii Yaspi Bendera ambalo ilielezwa kuwa Sitti anaabudu, ili kujiridhisha kama yupo, lakini pia hakuonekana huku waumini wakidai hawajamuona kwa siku za karibuni.Nabii Yaspi Bendera wa Kanisa la The Revelation Church.
“Hatumuoni siku hizi, ila alikuwa anakuja katika ibada ya peke yake kwa nabii saa kumi lakini siku za karibuni hatumuoni,” alisema muumini mmoja.Katika ibada inayoendeshwa kanisani hapo ambayo mapaparazi wetu walizama ‘kiintelijensia’, Nabii Yaspi alisikika akimkingia kifua Sitti kuwa alistahili ushindi na kumtabiria kufika mbali na hata kuwa Miss World huku akiwaonya wanaomfuatilia mrembo huyo.
“Mara ya kwanza nilimtabiria Sitti kushinda u-miss Tanzania na kweli akashinda, sasa wanatokea watu wakidai mara ana hipsi kubwa, ooh kadanganya umri, huu wote ni upepo tu na utapita.“Kama Sitti hatakengeuka kwenye imani yake atafika mbali zaidi na kushinda hata Miss World. Wale wote watakaoendelea kumfuatilia wataparalaizi,” alisema Nabii Yaspi.
Hadi mwishoni mwa wiki iliyopita, Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), walisema bado wanalifanyia uchunguzi suala la Ritta kudaiwa kufoji cheti cha kuzaliwa kutokana na baadhi ya nyaraka zake kuonesha amezaliwa mwaka 1989 huku yeye akidai amezaliwa 1991.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara akitafakari jambo.
Wakati RITA na BASATA wakiwa hawajatoa tamko lolote kufuatia uchunguzi waliodai wataufanya, gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Fenella Mukangara ili azungumzie sakata hilo.
“Waziri ni mtu mkubwa sana kuzungumzia suala kama hilo, watafute wasaidizi wangu pale wizarani watakuambia kinachoendelea. Naweza kutoa tamko halafu nikaonekana mtu wa ajabu, kumbe watu wanaendelea kulifanyia kazi, nenda kamuone Mkurugenzi wa Utamaduni atakusaidia,” alisema Waziri huyo alipozungumza nasi kwa njia ya simu.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate