EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, December 25, 2014

HUKU MKEWE AKISOTA GEREZANI MISS TZ AOLEWA NA MUME WA JACK PATRICK

Stori: Imelda Mtema DUNIA ina mambo! Wakati mkewe mwanamitindo Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ akiwa nyuma ya nondo kwa msala wa madawa ya kulevya ‘unga’ nchini China, mumewe, Abdulatif Fundikira ‘Tif’ amefunga ndoa ya siri na Miss Tanzania 2011, Salha Israel, Amani linakupa mchapo kamili.
Mume wa ‘Jack Patrick’, Abdulatif Fundikira ‘Tif’ akifunga ndoa ya siri na Miss Tanzania 2011, Salha Israel(liyeshika karatasi).
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, uhusiano wa Salha na Tif uliibuka na kushamiri mwaka jana baada ya Jack kukamatwa na unga huo.“Penzi lao liliibuka ghafla tu, jamaa naona ana ‘aleji’ na warembo wenye majina yao maana penzi lake na Jack lilipoyumba na kisha mrembo huyo kukamatwa na madawa ya kulevya nchini China, fasta akaanzisha uhusiano na Salha,” kilisema chanzo hicho.
UMAARUFU WA JACK UPOJE?
Jack ni mshiriki wa Miss Tanzania mwaka 2006 akitokea Miss Ilala lakini umaarufu wake ulizidi kukua baada ya kushiriki kama ‘video queen’ katika video mbalimbali za wasanii wa muziki wa Bongo Fleva ikiwemo video ya She Got Gwan ya marehemu Albert Mangwea.

Miss Tanzania 2011, Salha Israel akipozi.
VYANZO VINGINE
Hata hivyo, vyanzo vingine vimeeleza kuwa, Jack na mumewe walikuwa na mgogoro mzito kabla modo huyo hajakamatwa na madawa ya kulevya.“Walikuwa na mgogoro, ilifika wakati Jack alikuwa akidai talaka mahakamani lakini bahati mbaya kabla hajafanikiwa kupewa akaswekwa nyuma ya ndondo,” kilieleza chanzo hicho.


NDOA ILIVYOFUNGWA
Chanzo chetu kilichoshuhudia tukio hilo la siri kilieleza kuwa, Tif na Salha walifunga ndoa ya kiserikali Jumapili iliyopita Sinza-Mori jijini Dar, nyumbani kwa wazazi wa  Salha ambapo sherehe hiyo ilihudhuriwa na watu wachache ikisemekana ndugu wa pande zote mbili ndiyo walitawala zaidi.

“Kwenye hiyo ndoa hakukuwa na watu wengi, sanasana ndugu tena ilifungwa kwa siri sana, hawakupenda watu wengi wajue  kuhusiana na shughuli hiyo, hata wapiga picha walizuiwa kabisa kupiga picha katika simu zao,” kilisema chanzo hicho.
Mwanamitindo, Jacqueline Fitzpatrick Cliff ‘Jack Patrick’.
PICHA ZAPATIKANA
Katika kufukunyua uthibitisho wa taarifa hizo, mwanahabari wetu alifanikiwa kuzinasa picha za tukio hilo ambazo zinamuonesha Salha akiwa na Abdulatif pamoja na ndugu wachache wa pande zote mbili muda mfupi baada ya ndoa kufungwa.

JACK ATONYWA
Wakati mwanahabari wetu akizidi kuichimba habari hiyo juzi, alikutana ndugu wa Jack ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini. Alikiri kusikia ndoa hiyo na kuweka wazi kuwa taarifa zimemfikia Jack na kumfanya apate presha.

“Jack amepelekewa taarifa hizo Jumapili ileile, ameshtuka na presha ikampanda ingawa haikumchukua muda mrefu akarudi katika hali yake ya kawaida maana si unajua Jack na Salha ni marafiki!” alisema ndugu huyo.
‘Jack Patrick’ wakati akifunga ndoa na mumewe Abdulatif Fundikira ‘Tif’.
SALHA ANASEMAJE?
Amani lilimtafuta Salha kwa njia ya simu ili kujua anazungumziaje ndoa yake hiyo na Tof lakini simu yake haikuwa hewani muda mrefu.
Amani linaendelea kumtafuta, akipatikana atafunguka kwa kirefu zaidi.

TUJIKUMBUSHE
Tif na Jack walifunga ndoa Desemba 3, 2011 katika ufukwe wa Hoteli ya Coral, Masaki jijini Dar es Salaam. Ndoa hiyo ilifungwa na mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Hatibu Benard.

Mwaka mmoja baadaye, ndoa hiyo iliingia mdudu ambapo mzozo kwa wawili huo uliibuka kiasi cha kufikia hata Jack kushindwa kufika Gereza la Keko, Dar pale Tif alipotupwa mahabusu kwa madai ya kujihusisha na madawa ya kulevya. Mwishowe wawili hao walimwagana na Jack kupata msala na yeye wa kukutwa na madawa ya kulevya nchini China, Desemba mwaka jana ambako alihukumiwa kifungo cha miaka 7 jela.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate