EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, December 1, 2014

WANAWAKE WASUTANA KISA KUIBIANA BWANA

Stori: Dustan Shekidele, Morogoro
Makubwa! Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikiwa kwenye msukosuko wa fedha zilizochotwa ‘kihuni’ kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow, mwanaume mmoja, mtumishi wa wizara hiyo mkoani hapa almaarufu Kigogo wa Escrow, amesababisha wanawake wawili kusutana kwa matarumbeta na kukabana wakidaiwa kumgombea kwani ana fedha ‘chafu’.
Wakina mama, Tabu Mohamed na Mwajuma Chota  ( katikati ) wakisutana kwa kuibiana mabwana.
Tukio hilo la aina yake lilijiri wikiendi iliyopita katika Mtaa wa Karume mjini hapa ambapo wanawake hao, Tabu Mohamed na Mwajuma Chota walisababisha pakachimbika hadi polisi walipofika na kuokoa jahazi.
Awali ilifahamika kwamba wanawake hao walikuwa wakiishi pamoja maeneo ya Kikundi, Kata ya Sultan Area mkoani hapa. Kwa mujibu wa madai ya mashuhuda waliokuwa wamefunga mtaa huo, Tabu ndiye aliyeanza ‘kuchepuka’ na kigogo huyo ambaye ni mume wa mtu aliyemnunulia gari aina ya Toyota Opa.

Madai yaliendelea kushushwa kwamba, Mwajuma ambaye ni mke wa mtu alipoona mwenzake anakula vinono, naye akajiweka.
Bendi ilikodiwa na Tabu Mohamed ili kumsuta shosti yake Mwajuma Chota.
Habari za mtaani zilidai kuwa katika kujiweka, alifanikiwa kulamba mshiko wa shilingi elfu 80 kabla ya kushtukiwa na Tabu huku naye akitaka kuhongwa gari kama mwenzake.
Ilielezwa kwamba katika kufuatilia, Tabu aligundua kuwa Mwajuma anachepuka na ‘mshefa’ wake ndipo akapanga mashambulizi ya vita vya ardhini.
Kwa hasira, Tabu alishonesha sare za ‘madila’ na kununua mizinga ya pombe kali ambapo alienda kukodi matarumbeta na watu wa kusuta.
Wakubwa kwa watoto wakishuhudia vimbwanga vya wakinamama hao.
Ilisemekana kwamba kabla ya tukio, watu walipiga pombe kisha wakamfuata nyumbani kwao, Mtaa wa Karume na kulianzisha.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda ambalo liliwasili eneo la tukio ndani ya dakika sifuri juu ya tukio hilo, Mwajuma alifunguka: “Namshangaa Tabu kuja kunifanyia vurugu wakati na yeye ni mwizi tu. Huyo bwana ni mume wa mtu.”
Kwa upande wake, Tabu alidai Mwajuma ni shosti yake lakini alimtendea kitendo kibaya cha kutembea na bwana’ke.
Mmoja wa wamama hao, Tabu Mohamed  akichukuliwa na polisi kwa kumletea fujo mwenzake, Mwajuma Chota.
Alipobanwa zaidi hasa suala la kukodisha matarumbeta na kwamba mwanaume huyo ni mume wa mtu, Tabu alidai kwamba jamaa huyo alimkataza kuzungumza na wanahabari.
Baada ya kuipata ishu hiyo, gazeti hili liliwasiliana na mke wa kigogo huyo na kumuuliza kama ana habari kwamba kuna wanawake wanamgombea mumewe ndipo akapatwa na mshtuko na kuahidi kulifanyia kazi na kama ni kweli atafungasha virago.
Makamanda wa Polisi wakiimarisha ulinzi eneo la tukio.
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Mtaa wa Karume, Elly Mgota alithibitisha vurugu hizo kutokea kwenye mtaa wake ambapo sakata hilo lilitinga polisi baada ya Tabu kutiwa mbaroni kwa kosa la kumfanyia fujo mwenzake.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate