EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, January 24, 2015

BABA, MAMA DIAMOND HOI KITANDANI

Na Waandishi wetu/Risasi
HALI ni tete! Wazazi wa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kasim na Abdul Juma wako hoi vitandani wakikabiliwa na maradhi mbalimbali, Risasi Jumamosi lina taarifa kamili.
Mama wa mbongofleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sanura Kasim akiuguza ugonjwa,
MAMA DIAMOND
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha uhakika, mama Diamond hajiwezi kwa mwezi mmoja sasa akisumbuliwa na maradhi yenye kuashiria kupooza sehemu ya mwili na kushindwa kutembea. Anaugulia nyumbani kwake, Sinza ya Mori jijini Dar es Salaam.

YADAIWA KUWA SIRI
Habari zinadai kuwa, ugonjwa wa mama huyo umefanywa kuwa siri kwa watu wengine lakini bila kujulikana kisa cha usiri huo.
BABA DIAMOND
Chanzo hicho kilieleza kuwa, baba Diamond kwa muda mrefu usiorekodiwa siku, anasumbuliwa na maumivu makali ya miguu, naye kwa kiasi cha kushindwa kutembea.
“Yeye anaugulia mafichoni kwani ndugu zake wamemficha mahali pasipojulikana ili watu wasimwone. Inaaminika kuna mambo ya kishirikina ndani yake,” kilisema chanzo hicho bila kufafanua ushirikina wa vipi!
RISASI LATAKA UTHIBITISHO
Ili kupata mzani sawa wa madai hayo, Risasi Jumamosi liliingia mtaani kwa wahusika wote.
Bi. Sanura Kasim akiwa hoi kwa ugonjwa.
BREKI YA KWANZA
Katikati ya wiki hii, Risasi Jumamosi lilifika nyumbani kwa mama Diamond na kugonga geti kubwa. Msichana mmoja alitoka na kufungua geti.
Msichana: “Nikusaidie nini?”
Risasi Jumamosi: “Nimekuja kumwona mama Diamond, nasikia anaumwa sana.”
Msichana: (anafikiri kwa muda). “Mh! Ngoja nikuitie mtu mmoja uongee naye.”
Baada ya dakika mbili,mwanamke mmoja alifika getini na kukutana uso kwa uso na Risasi Jumamosi, ikawa hivi:
Mwanamke: “Eti unasemaje?”
Risasi Jumamosi: “Nimekuja kumjulia hali mama Diamond, tumesikia anaumwa.”
Mwanamke: (naye anafikiria kwa muda). “Hebu subiri kwanza.” (akaondoka).
BAADA YA DAKIKA MBILI TENA
Baada ya dakika mbili, msichana wa kwanza ndiye aliyerudi getini na kusema:
“Mama Diamond mbona hayupo, alitoka. Ni mzima na ameenda kwenye shughuli zake kama kawaida.”
Mbongofleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akiwaza jambo.
MASWALI
Risasi Jumamosi liliondoka na maswali kuhusu majibu ya msichana huyo.
Kama kweli haumwi na alikwenda kwenye shughuli zake kama kawaida, kwa nini jibu hilo lisipatikane awali? Kulikuwa na ulazima gani kwa msichana huyo kutojibu ametoka mpaka akaenda kumwita mwanamke ambaye naye alishindwa kusema na kurudi ndani kumtuma msichana huyo? Sababu wanayo wenyewe!

DAKTARI ASHAURI
Kwa mujibu wa daktari mtaalamu wa viungo, alishauri kuwa endapo mama Diamond amepooza ni vyema akapata tiba kwa wataalamu wa viungo mapema kwani tatizo linaweza kuongezeka.

BABA DIAMOND SASA
Risasi Jumamosi lilifunga safari hadi Magomeni ya Kagera, Dar ambako ni nyumbani kwa Baba Diamond.
Baada ya kugonga mlango, mwanamke mmoja alitoka. Baada ya Risasi Jumamosi kujieleza naye alijitambulisha kuwa ndiye mke wa sasa wa baba Diamond.
Risasi Jumamosi: “Tumesikia mzee Abdul, baba yake Diamond anaumwa sana. sasa nimekuja kumjulia hali.”
Mke: “Ni kweli Abdul anaumwa, anasumbuliwa na miguu lakini haugulii hapa.”
Risasi Jumamosi: “Anaugulia wapi? Kwani amelazwa?”
Mke: “Hajalazwa na anakougulia kwa kweli siwezi kupataja.”
Baba wa 'Diamond Platnumz', Abdul Juma.
WAPIGIWA SIMU
Juzi, Risasi Jumamosi liliwasaka wazazi hao kwa njia ya simu ili kuwasikia wanasemaje kuhusu madai ya kuumwa kwao.
Mama Diamond hakupatikana hewani, lakini baba Diamond alipopatikana alisema:
“Ni kweli naumwa bwana. Miguu inasumbua sana. Si unajua hili ni tatizo langu tangu mwaka jana?”
Risasi Jumamosi: “Nakumbuka. Sasa uko wapi nije kukupa pole?”
Baba Diamond: “Asante, usiwe na wasiwasi we endelea na shughuli zako tu, ila niombee maana kidogo hali inaanza kuonesha matumaini.”
Risasi Jumamosi: “Vipi Diamond ameshafika kukuona?
Baba Diamond: “Ah! Hapana, ila mdogo wake Mwajuma (Queen Darleen). Lakini Nasibu (Diamond) sijamwona.”
Risasi Jumamosi: “Pole sana, labda ana mambo mengi kwa sasa. Basi pole sana mzee wangu.”
Baba Diamond: “Haya nashukuru sana.”

DIAMOND MACHOZI TUPU
Kwa mujibu wa chanzo kilicho karibu na staa huyo, kutokana na hali aliyonayo mama yake, amekuwa akilia mwenyewe pindi akiwaza hatma ya mama yake ingawa simu yake alipopigiwa na mwanahabari wetu, hakupokea.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate