EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, January 24, 2015

HATIMAYE WAZIRI WA NISHATI NA MADINI, PROFESA SOSPITER MUHONGO AJIUZULU

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akiongea na wanahabari ofisini kwake leo.
Hatimaye Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospiter Muhongo amejiuzulu leo jijini Dar es Salaam.
Waziri Muhongo amechukua uamuzi huo leo ofisini kwake mbele ya waandishi wa habari.

Kujiuzulu kwa Muhongo kumetokana na maazimio ya Kamati ya Bunge  ya Hesabu za Serikali chini ya Mhe. Zitto Kabwe ilitokana na sakata la ufisadi wa Akaunti ya Escrow ambapo zaidi ya shilingi bilioni 306 zilichukuliwa kiholea Benki Kuu ya Tanzania na kusababisha mjadala mzito ndani na nje ya Bunge.

Ukaguzi maalum uliofanywa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)  na uchuguzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kwenye akaunti hiyo, ulifanywa na ripoti zikatolewa na bunge, likajadili na kufikia tamati kwamba kuna kodi ya umma iliibwa.
Kwa vile suala hili liligusa utendaji wa viongozi wa ngazi za juu serikalini pamoja na wanasiasa wengine,  bunge lilitaka kuyumba kutokana na kupendeleana licha ya ukweli kwamba fedha zilizochukuliwa ni nyingi sana .
Mhe. Muhongo alipokuwa Bungeni wakati wa sakata hilo
Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), chini ya Uenyekiti wa Zitto Kabwe ilipitia kwa ufasaha ukaguzi wa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali,(CAG)  na uchunguzi wa Takukuru wakatoa ripoti yao na uthibitisho wa kutosha kuwa kuna (aliyekuwa) Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema, Waziri wa Madini na Nishati, Profesa Sospiter Muhongo pamoja na watendaji wengine serikalini wamehusika kwa njia moja au nyingine na upotevu wa fedha hizo za Escrow ama kwa kukusudia ama kwa kutojua, kitu ambacho kilielezwa kuwa ni uzembe.
Rais Jakaya Kikwete alichukua uamuzi wa kumfuta kazi Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka  kutokana na madai kuwa alichotewa shilingi Bilioni 1.6  zilizotoka katika akaunti hiyo ya Escrow.
Mhe. Anna Tibaijuka
Rais Kikwete alisema Profesa Muhongo alikuwa amemuweka kiporo. Hata hivyo, Watanzania wengi wakati wa kikao cha bunge liliopita walishangazwa kuona baadhi ya wabunge kukaza misuli ya shingo zao na kutetea wizi ili wahusika wasiwajibishwe. Wengine walipingana na ripoti ya CAG.
Wakati wa kikao hicho cha Bunge aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema alidaiwa kutaka kumpiga Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila ambaye ndiye aliyeanzisha mjadala wa sakata hilo bungeni.
Aliyekuwa Mwanasheria wa Serikali, Jaji Werema
Vyombo vya habari vikatangaza kuwa kama siyo kuzuiwa na mawaziri, Jaji Werema angezua tafrani bungeni kutokana na kitendo chake cha kutaka kumpiga mbunge huyo  kutoka NCCR-Mageuzi, David Kafulila.
Ilidaiwa kuwa tafrani hiyo ilitokea baada ya Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Azzan Zungu kuahirisha kikao cha Bunge hadi jioni ya siku hiyo, ikiwa ni muda mfupi baada ya Werema na Kafulila kurushiana maneno bungeni baada ya jaji kuchukizwa na kitendo cha mbunge huyo kijana kumwita mwizi, akijibu mapigo baada ya mbunge huyo kuitwa tumbili (na mwanasheria mkuu huyo wa nchi).
Waliomzuia Jaji Werema asizipike baada ya kumzunguka inadaiwa ni baadhi ya mawaziri ambao walimsindikiza hadi nje ya Ukumbi wa Bunge.

Jaji Werema pia alituhumiwa kumtishia kifo Kafulila ambaye alilalamika bungeni. Ikadaiwa kuwa jaji huyo alimtolea maneno hayo ya vitisho mbunge huyo kwenye viunga vya bungeni mjini Dodoma baada ya bunge kuahirishwa.
Mhe. David Kafulila
Jaji Werema alinukuliwa na vyombo vya habari akidaiwa kumwambia Kafulila: "I will take your head, unless you apologize," ikimaanisha atamkata kichwa iwapo hatamwomba msamaha!

Kufuatia tishio hilo Kafulila akajihami kwa kuiandikia barua ya madai ya kutishiwa maisha ofisi ya spika wa bunge, huku nakala ya barua hiyo akiipeleka kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Ernest Mangu na nakala nyingine ameipeleka kwa kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma.
Hili ni tukio baya sana ambalo limeingia katika rekodi. Werema pia alijiuzulu kutokana na kashfa hiyo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate