EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 13, 2015

HAUSIGELI ASAKWA WIZI WA MTOTO

Stori: Shomari Binda, Mara/UWAZI MFANYAKAZI wa ndani anayefahamika kwa jina la Paulina Sobe anatafutwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kuhusika na wizi wa mtoto wa bosi wake, Diana Meshack, mwenye umri wa miaka miwili, huko Musoma mkoani Mara, tukio lililotokea Januari 3 mwaka huu.
RPC Mara akiwa na mtoto aliyeibiwa(kushoto) ni mama wa mtoto huyo.
Kamanda wa Jeshi hilo mkoani Mara, ACP Philip Kalangi, aliliambia gazeti hili kuwa kwa kushirikiana na askari wa Kanda Maalum ya Kipolisi Tarime/Rorya,wamefanikiwa kuwakamata watu wawili walioshirikiana na hausigeli huyo kumuiba mtoto.
ILIKUWAJE?
Chanzo kilicho karibu na familia hiyo kinasema kuwa Januari 3 mwaka huu, msichana huyo wa kazi alionekana na majirani akiondoka na mtoto huyo na kwenda naye kusikojulikana na tokea wakati huo hakuonekana tena.


HALAFU?
Lakini mara tu baada ya kuondoka nyumbani hapo, mama wa mtoto huyo, Gadioza Meshack alipokea simu kutoka kwa watu wasiojulikana, waliomtaka kuwapa shilingi milioni 3 ili wamrudishe binti yake, vinginevyo wangeenda kumuuza kwa watu wanaonunua watoto.

Kamanda wa Jeshi mkoa wa Mara, ACP Philip Kalangi.
ASHINDWA, ALIFIKISHA POLISI
Kamanda Kalangi alisema baada ya mama huyo kulifikisha suala hilo Polisi, wao kwa kushirikiana na kampuni za mitandao ya simu, walianzisha msako wa kuwasaka watu hao na kufanikiwa kuwanasa Januari 7 mwaka huu katika kijiji cha Kitamwi, kilichopo mpakani mwa nchi jirani ya Kenya.
“Tulifanikiwa kuwakamata Vicent Magesa (19) na Erick Range, wote wakazi wa Getabwaga nchini Kenya, wakiwa na mtoto huyo ambaye pia tulimkuta akiwa salama,” alisema Kamanda Kalangi.

MAMA AELEZA ILIVYOKUWA
Akisimulia mkasa wa kuibwa kwa mtoto wake, Gadioza Meshack alisema Januari 3 mwaka huu, kabla ya kwenda kazini kwake,alimuacha mtoto akiwa na mfanyakazi huyo aliyempa shilingi 15,000 ya kulipa bili ya maziwa na 10,000  ya matumizi.

“Nalishukuru Jeshi la Polisi kwa kufanya jitihada za kupatikana kwa mtoto wangu licha ya kwamba yule mfanyakazi aliyeondoka naye hajapatikana, ila naamini kutokana na kazi kubwa iliyofanywa ya kumpata mtoto hata yeye atapatikana,” alisema mama huyo.
Aliwataka wazazi kuwa makini na watu wanao wachukua kwa lengo la kulea watoto kwani wengine sio wazuri na baadhi hubadilika kwa kushawishiwa.

CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate