EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, January 14, 2015

JIFUNGIENI, ELEZANENI!

KUNA msanii mmoja wa muziki wa kizazi kipya nchini anaitwa Rich Mavoko. Sijamfuatilia sana, lakini nyimbo chache alizoimba, zina ujumbe unaopaswa kupongezwa.
Kuna kibao chake kimoja kinasema Roho Yangu. Kwa sisi wapenzi wa Bongo Fleva, huu ni moja kati ya tunzi zenye kuelimisha, achilia mbali burudani nzuri inayopatikana ndani yake. Katika mstari mmoja miongoni mwa versi, unasema ‘Ukiwa mjanja kuchapiwa ni siri ya ndani.’

Sina uhakika ni watu wangapi wanajua maana ya msemo huu, lakini kwa wale ambao huenda wanapata taabu kidogo, ni kwamba ikitokea umebaini kuwa mwenza wako amechepuka na wewe umegundua, hili si jambo la kuanza kulitangaza kwa marafiki na majirani, bali ni wakati muafaka, wa kulifanya kuwa la kifamilia zaidi.
Utatoka nje ya nyumba yako na kukimbilia kwa marafiki au majirani na kumshitaki mwenza wako jinsi alivyo mchepukaji. Katika hatua za awali, akili yako itaamini kabisa kuwa unajiweka katika nafasi salama na tena, kujaribu kujionyesha kuwa wewe ni mtu safi, unayetiwa dosari na mwenzako.
Ni sawa, lakini nikuambie kitu, sisi, kwa maana ya waswahili, hatuna wema unaodhani tunao. Utajikimbiza hadi kwa shoga yako na kumwelezea jinsi mume au rafiki yako alivyokusaliti kwa kushiriki mapenzi na mtu mwingine. Bila shaka utaomba ushauri, ufanye nini, umuache, mzungumze mbele yake au kwa mjumbe, ama mkakae wenyewe na kujadili.
Labda niongeze kitu kingine, kukimbilia kwa mashoga, majirani na wajumbe hakuishii tu kwenye mambo ya kimapenzi. Yapo mambo mengine pia ya kifamilia ambayo tunadhani hatuwezi kuyamaliza wenyewe pasipo kuwashirikisha watu wa nje.
Mathalani, mume kuwa na mkono wa birika katika kumpendezesha mkewe, mume kuwa mnywaji wa kupitiliza, mke kupenda kugawa vitu ovyo vya ndani, mke kupenda umbeya, mume kukaa vijiweni, mke kuwa na mazoea na vijana wa kiume na mambo mengine chungu nzima kama tunavyojua huko mitaani!
Haya yote, yanajadilika ndani ya nyumba au chumba chenu. Hakuna kitu chochote cha kifamilia kinachoweza kuwa nje ya baba na mama. Nasisitiza, hakuna.
Iko hivi, mnaweza kuwa katika ugomvi mkubwa baina yenu, mkawahusisha wazazi au hata ndugu wengine wa karibu. Lakini mwisho wa siku, wote hao, watataka mshikane mikono, msameheane.
Unajua kwa nini inaishia hivi, ni kwa sababu hakuna mbabe yeyote duniani anayeweza kuwalazimisha nyinyi kuishi pamoja. Sasa basi, mtaenda huko mnakoenda, mnatoleana siri zenu, mnadhalilishana, halafu mwisho wa siku mnaambiwa mshikane mikono msahau tofauti zenu!
Lakini wakati mnasameheana, tayari watu wa nje wameshajua udhaifu wenu, mmeshawapa faida na wanatumia nafasi hiyo kuwang’ong’a.
Kumbe ingewezekana kabisa kabla ya kutoka nje na kuwaalika watu, mngeweza kukaa wenyewe na kuzungumza na kuzimaliza tofauti zenu. Usije ukaniambia baba flani haambiliki, siyo kweli. Hujamjulia tu, hakuna mtu anayependa nyumba yake iwe ya moto, kila mara wote tunapenda nyumbani pawe sehemu salama.
Unachopaswa kufanya ni kupima tu upepo. Kama mke au mume wako ana kawaida ya kukasirika siku tatu au wiki baada ya kukwaruzana, subiri muda huo upite, halafu muombe muda wa kujadiliana naye, kisha mweleze jinsi gani, anavyokunyima furaha kwa matendo yake.
Binadamu ana hulka ya kutaka kuheshimiwa, hata kama ni mkosefu. Ukimweleza kosa lake taratibu, kwa upole, atakuelewa tu. Na ili jambo hili mlimalize vizuri, msitafute mshindi. Hakuna mtu anayekubali kushindwa mbele ya mwenza wake, hasa tunapotoka katika kukwaruzana.
Narudia na kusisitiza, malizeni tofauti zenu ndani ya nyumba, mjifungie, ongeeni kwa sauti za chini, kila mtu aonyeshe heshima kwa mwenzake, mwisho wa siku, mtaishia kicheko na maisha yenu yataendelea kuwa raha mustarehe!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate