EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, January 9, 2015

KISA ZARI DIAMOND AITWA SHOGA

HII ni ‘bad news’ kwa staa namba moja wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’. Mfanyabiashara maarufu nchini Uganda anayefahamika kwa jina la King Lawrence, ameibuka na kumuita nyota huyo shoga.
Staa namba moja wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na Zarinah Hassan ‘Zari’.
ISHU ILIPOIBUKIA
King ambaye ana makazi yake pia nchini Afrika Kusini, amedaiwa kutoa kauli hiyo juzi, Jumatano kupitia mtandao wa Facebook akionesha kukerwa na kitendo cha staa wa muziki Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’ kuangukia katika penzi la Diamond.
ATUMIA GIA YA WATOTO
Awali, King ambaye imeelezwa alikuwa na urafiki na dereva wa aliyekuwa mume wa Zari, Ivan Semwanga, alianza kwa kumchokonoa Diamond kwa gia ya kujifanya anawatetea watoto wa Zari ambapo alitupia picha ya Zari akiwa na Diamond mtandaoni ikiwa na ujumbe wenye kejeli na jeuri ya fedha.
UJUMBE ULIVYOSOMEKA
“As a concerned uncle, Im offering Zari’s tomboy Diamond Dola 40,000 so as to leave the old mom of three to take care of her kids. The young boys miss their mom. Please Diamond do it for the kids.”
(Nikiwa kama mjomba, ninampa jikedume wa Zari, Diamond, Dola 40, 000 (Sh. Mil 66) ili amuache mama wa watoto watatu (Zari) awalee vizuri watoto wake. Watoto wanammisi mama yao.”
Diamond Platnumz na Zari wakidendeka.
ABADILISHA GIA
Kuonesha ana mpango mchafu wa kumchafua Diamond ambaye anaipeperusha vyema bendera ya Afrika kimuziki, badala ya ishu ya watoto, alibadili upepo na kujinadi eti yeye ndiye wa kwanza kutembea na Zari.
Pasipo kueleweka kusudi lake, alimpiga dongo Diamond ambaye usiku wa kuamkia leo alipewa heshima ya kipekee kutumbuiza kwenye Tuzo za Wanamichezo Bora zilizoandaliwa na Shirikisho la Afrika (Caf) nchini Nigeria.


HEBU MSIKIE
“Kwa nini utembee na Diamond shoga? Sijui kama anajua kwamba mimi ndiyo wa kwanza kutembea na wewe (Zari),” aliandika katika mtandao wa Facebook.

AZIDI KUTAPATAPA
Kama hiyo haitoshi, kupitia mtandao wa Facebook, King alitupia mawasiliano yake ya zamani na Zari akidai alikuwa akimuomba fedha.
DIAMOND ANASEMAJE?
Hadi tunakwenda mitamboni, jitihada za kumpata Diamond ili aweze kujibu tuhuma hizo hazikuzaa matunda huenda ni kutokana na ubize aliokuwa nao katika maandalizi ya shoo hiyo kubwa Afrika, simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi, hakujibu.
King Lawrence.
ZARI AMSAFISHA DIAMOND
Kupitia mtandao huo, Zari naye aliibuka na kumtetea Diamond akimwambia King ana chuki binafsi kwani hapendi kumuona akiwa na furaha.
“Hatuna muda wa kukujadili, unafikiri Diamond anaweza kuwa shoga? Unafikiri anaweza kubishana na wewe? Kweli nimeamini, watu wakikuona una furaha, wanaanza kukuchukia,” alijibu Zari maneno hayo ambayo pia ameyaweka katika akaunti yake ya mtandao wa Instagram.
DIAMOND NI SHOGA?
Kutokana na madai hayo ya King, baadhi ya wadau wakubwa wa muziki Bongo walikanusha vikali madai hayo kwa kudai jamaa huyo ana lengo la kumchafua Diamond kwa kuwa kwa sasa anafanya vizuri Afrika nzima.
“Hana lolote huyo King, anatafuta kiki za kipuuzi, atamuitaje Diamond shoga? Amewahi kumuona akifanya vitendo hivyo? Wivu tu wa maendeleo, aache Diamond na Zari wafanye yao, apeperushe muziki wetu nje ya Afrika,” alisema mdau mmoja ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini.
KING ANATESWA NA WIVU?
Licha ya awali King kutoonesha kwamba aliwahi kutembea na Zari, katika maelezo yake ya pili yameonesha dhahiri kwamba anasumbuliwa na wivu wa mapenzi kutokana na kujinadi kuwa yeye alikuwa wa kwanza kutembea na Zari.
“We huoni ameanza kwa kujifanya anawatetea watoto, mara akajifanya rafiki wa dereva wa Ivan mara tena amegeuka anadai alikuwa wa kwanza kutembea na Zari hana lolote wivu tu unamsumbua atakuwa alimtaka mtoto mzuri akamchomolea,” aliandika mdau mmoja katika mtandao wa Instagram.
KING NI NANI?
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, jamaa huyo ni mfanyabiashara maarufu nchini Uganda na Afrika Kusini na amekuwa akijinasibu kuwa na uhusiano na mastaa mbalimbali wa Uganda akiwemo mwanamuziki Julia Kanyomozi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate