EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, January 10, 2015

LULU APELEKEWA BARUA YA UCHUMBA

STAA ndani ya Tasnia ya Filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, amepelekewa barua ya uchumba kutoka kwa mfanyabiashara mmoja jijini Dar na kumfanya mama mzazi wa Lulu, Lucresia Karugila abaki ameshangaa.Tukio hilo lilitendeka Januari 8, mwaka huu, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam ambako ndiko yaliko makazi ya Lulu na mama yake huyo.
Mshenga anayefahamika kwa jina moja la Isaya akipeleka posa kwa akina Lulu Elizabeth Michael.
MSHENGA NI MPAMBE
Kwa mujibu wa watonyaji wetu ambao waliwataarifu mapaparazi wetu wa Kitengo cha Kufichua Maovu (OFM) kuhusu barua hiyo na kutia timu nyumbani hapo, mtu aliyepewa kuifikisha kwenye familia hiyo ni mpambe mkubwa wa mfanyabiashara huyo aliyetajwa kwa jina moja la Isaya, mkazi wa Kinondoni B, Dar es Salaam ambaye sasa amekuwa mshenga pia.

Staa ndani ya Tasnia ya Filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
MSHENGA GETINI KWA AKINA LULU
Ilikuwa saa tano asubuhi, mshenga huyo akiwa ndani ya gari aina ya Toyota Corolla (namba hazikupatikana mara moja), alishuka nje ya geti kuu la nyumbani kwa akina Lulu ambapo anaishi na mama yake.

Mshenga huyo alibisha hodi kwa muda wa kama dakika tano ambapo mfanyakazi wa ndani (hausigeli) alifika getini na kufungua mlango.
Mshenga akigonga hodi getini kwa akina Lulu.
KILICHOZUNGUMZWA GETINI
Haikujulikana mara moja, wawili hao walikuwa wakizungumza nini getini lakini mapaparazi wetu waliweza kushuhudia mshenga huyo akinyoosha mkono na kumpa bahasha msichana huyo kisha geti likafungwa, mshenga huyo akasimama pembeni, huenda kusubiri majibu.
MSICHANA AREJEA
Baada ya dakika kama kumi, msichana huyo alirudi getini, akafungua nusu ya mlango kama awali na kuanza kuzungumza na mshenga huyo.
MSHENGA AONDOKA
Baada ya mshenga huyo kuondoka hatua kama ishirini mbele mapaparazi wetu walimwibukia na kumuuliza shida iliyompeleka kwenye nyumba ya akina Lulu.“Kwani vipi?” aliuliza mshenga huyo kabla ya kusema.
Mshenga akiondoka mara baada ya kumaliza majukumu mazito.
Risasi: “Sisi tulipata habari kwamba wewe umepeleka barua ya posa pale, ni kweli?”
“Kweli nimetoka nyumbani kwao na Lulu, nilipeleka barua ya uchumba ya bosi wangu.
“Nimefurahi nilipofika pale nikagonga geti, akatoka msichana mmoja, nilimuuliza kama mama Lulu yupo akasema yupo, nikampa barua akapeleka maana hakutaka mimi niingie,” alisema mshenga huyo.
MAJIBU YALIKUAJE?
“Baada ya muda yule msichana alirudi, akanipa barua akisema eti si ya Elizabeth wala Lulu. Sasa ni ya nani wakati jina la juu ya bahasha ni Elizabeth Michael.”“Naamini kabla mama Lulu hajaisoma aliangalia juu ya bahasha na kuliona jina la Elizabeth Michael ndiyo maana wakati ananirudisha tayari bahasha ilikuwa imefunguliwa.”
Barua ya uchumba iliyowasilishwa na mshenga kwa mama Lulu.
UTARATIBU ULIFUATWA?
Risasi lilimuuliza mshenga huyo kama bosi wake alifuata utaratibu wa barua za posa katika utamaduni wa Kitanzania ambapo ndani ya bahasha huwekwa pesa kidogo.“Tulifuata utaratibu wote, ndani ya bahasha tuliweka shilingi laki moja na zimerudi zote.”
MAMA LULU ANASEMAJE?
Baada ya kudokezwa ishu hiyo, Risasi lilimtafuta mama mzazi wa Lulu ili kumsikia anasemaje kuhusu madai ya mshenga huyo, kwamba alipeleka kweli barua ya posa kwa Lulu au alikwenda kwa shida nyingine.
“Mimi mwenyewe nawashangaa ninyi waandishi. Mambo ya kuolewa anayetakiwa kuulizwa ni Lulu mwenyewe. Kama mtu alileta barua au nini, Lulu ndiyo atajibu.
Staa ndani ya Tasnia ya Filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
“Halafu naomba kuwaambia kwamba nilishasema siku nyingi mimi sitaki mambo ya magazeti, hata hao mabosi wenu niliwahi kuwaambia,” alisema mama Lulu na kukata simu.
LULU HAPOKEI SIMU
Baada ya kuzungumza na mama mtu, gazeti hili lilimsaka Lulu mwenyewe ili kumsikia anazungumziaje kuhusu barua hiyo lakini simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa.

CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate