EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, January 7, 2015

LUNDENGA; USITAFUTE MCHAWI, BADILIKA! KWAKO


Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga. Bila shaka u-mzima wa afya na unaendelea na michakato yako ya kukufanya mkono uende kinywani.
Binafsi mimi ni mzima wa afya, naendelea na majukumu yangu ya kila siku. Miongoni mwa majukumu yangu ni hili la kukuandikia barua, huwa nawaandikia watu tofauti lakini leo nimekukumbuka wewe kama muandaaji wa shindano kubwa la urembo nchini, Miss Tanzania.

Dhamana uliyokuwa nayo kwa miaka zaidi ya10 sasa kuandaa shindano hilo si ya kubeza. Ni kazi nzito na yenye maslahi makubwa kwa taifa. Warembo ambao wanapatikana kupitia shindano hilo ndiyo wanaotakiwa kutuwakilisha kwenye mashindano ya dunia.
Ukivurunda huku chini, matokeo yake ni kwenda kuharibu kule juu. Msingi ukiwa mbovu katika mashindano ya wilaya, mkoa na hata mshindi wa Miss Tanzania atakuwa hastahili kutubeba katika mashindano ya dunia.
Nimekuwa nikifuatilia mashindano haya kwa muda mrefu kidogo, natambua ugumu wa mchakato mzima wa kuyaandaa lakini kila mwaka malalamiko ambayo si ya msingi yameendelea kuonekana.
Suala la kwamba matokeo yalipangwa, huo ni wimbo ambao umekuwa ukiimbwa mara kwa mara. Majaji kupendelea, ujanjaujanja unaofanywa na washiriki mara sijui amezaa, ametoa rushwa ya ngono ni mambo ambayo tumechoka kuyasikia.
Ujanjaujanja una mwisho wake na ndiyo maana juzi ukaona kilichotokea kwa mshindi, Sitti Mtemvu ambaye ilibainika amefoji suala la umri. Kabla ya hapo, watu walilalamika kwamba hakustaili tangu siku aliyotangazwa.
Wapo waliomkosoa kwa kushindwa kujieleza au kuzidisha mbwembwe kwa kuongea lugha ya Kifaransa kinyume na masharti ya kujieleza yalivyomtaka. Suala la umri liliibua mjadala mkubwa, likasababisha watu wahoji uhalali wake kiasi cha kumshinikiza mshindi huyo ajivue mwenyewe taji.
Anko nakuheshimu sana, katika kipindi hiki ambacho serikali imekufungia shindano hilo kwa miaka miwili, hauna haja ya kushindana kwa kesi, chukulia kama changamoto. Tengeneza mfumo mzuri ambao utakuwa hauna longolongo pindi utakaporudi kwa mara nyingine.
Hatutegemei kuona mshiriki anaingia katika shindano akiwa hana sifa. Jiridhishe mapema ili kuepuka aibu nzito unayokuja kuipata mwishoni. Epuka vishawishi vya kuchafuka katika hali yoyote. 

Hadi kufikia hatua ya kukufungia, najua serikali imevumilia mengi na kuona hakuna haja ya kuendelea kukuvumilia. Hapa lazima uamue kweli kubadilika kama kweli una nia njema katika mashindano haya.
Kila mmoja anapenda kuona Tanzania inafanya vizuri katika tasnia ya urembo. Usiwaangushe, wekeza fedha za kutosha na kama haiwezekani basi tafuta wadhamini wa kutosha watakaoweza kudhamini na kusiwe na longolongo.Kwa leo ngoja niishie hapa, nikutakie maandalizi mema.

Wasalaam, 
Erick Evarist.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate