EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 20, 2015

MBARONI KWA MAPENZI YA JINSIA MOJA

Makongoro Oging’ na Haruni Sanchawa/Uwazi
DUNIA imekwisha! Wasichana wawili warembo, Maua Sadick (24), mkazi wa Stakishari, Ukonga wilayani Ilala na Lucy Fred (23), mkazi wa Karakata jijini Dar es Salaam, wanashikiliwa katika Kituo cha Polisi Stakishari, Ukonga, Dar kwa kesi yenye jalada STK/RB/463/2015 wakidaiwa kufanya mapenzi ya jinsia moja.
Warembo, Maua Sadick (mwenye shati la draft) na Lucy Fred wakipozi kimahaba.
Warembo hao walikamatwa Januari 12, mwaka huu saa sita mchana, nyumbani kwa Maua wakidaiwa kufanya ngono kinyume cha sheria ya kujamiiana ambapo watu wa jinsia moja ni makosa kukutana kimwili.

NDUGU, MAJIRANI WAKERWA
Kwa mujibu wa habari za kipolisi, kukamatwa kwa Maua kulitokana na taarifa za baadhi ya ndugu na majirani zilizopelekwa polisi kwamba, wasichana hao wanapokuwa kwenye tendo la ndoa wamekuwa wakipiga kelele za udhalilishaji kwa familia zao.
Wasichana hao wakiwa maeneo tofauti.
WALISHAONYWA, HAWAKUSIKIA
Vyanzo makini kutoka jirani na makazi ya Maua vinadai kuwa, kutokana na hali hiyo, baadhi ya watu walijitolea kuwaonya wasichana hao kuwa na staha wawapo kwenye faragha yao lakini pia wao ni wanawake haiwezekani wacheze mchezo huo wenyewe kwa wenyewe lakini hawakutaka kusikia.
MAJIRANI WAFUNGULIA REDIO SAUTI YA JUU
“Ilifika mahali wakiingia chumbani kuanza mambo yao sisi majirani tunazidisha sauti za redio ili watoto wasisikie lakini na wao sauti zao zinakuwa juu kushinda za redio,” alisema jirani mmoja akiomba jina lake lifichwe ili kukwepa uhasama.
Alisema kutokana na hali hiyo waliamua kufikisha habari hizo polisi kwani ni kinyume cha sheria watu wa jinsia mmoja kukutana kimapenzi.
Mrembo Lucy Fred ambaye ni mpenzi wa Maua Sadick.
HISTORIA YA LUCY
Wakizidi kuzungumza na Uwazi, majirani hao walisema, Lucy ambaye ndiye anaitwa mke na Maua amekuwa akitoka nyumbani kwa wazazi wake Karakata kwa lengo la kumfuata Maua.
SIKU YA TUKIO
Ilisemekana kuwa, siku ya tukio, majirani walipoanza kusikia ‘zile sauti zao’, waliwapa polisi namba ya simu ya mtu wa jirani na Maua kwa lengo la kusaidia kufika nyumbani hapo.
“Polisi walipofika waligonga mlango kwa muda mrefu bila kufunguliwa na kelele za mahaba zilizidi kusikika. Baadaye, nadhani wakati wanapumzika sasa, Maua alifungua mlango mkubwa na kukutana na macho ya polisi, wakambana na kumtaka waende wote alipo Lucy, wakaenda chumbani na kumkuta.
“Pia polisi walikuta kidude ambacho huwashwa kwa betri kilichodaiwa pia hutumika wakati wa tendo,” kilisema chanzo.
Warembo hao kama wanavyoonekana kwenye picha zao za instagram.
HISTORIA YA MAUA
Maua ni binti ambaye ni yatima, amekuwa akiishi mwenyewe kwenye nyumba hiyo kubwa ya familia hivyo kumwita Lucy mara kwa mara kwa madai ya kufanya ufuska huo kwa vile wana uhuru.
Inasemekana kuwa, Maua siku zote amekuwa akivaa mavazi ya kiume licha ya kwamba, ni mwanamke kamili.
POLISI WASHANGAA
Taarifa kutoka vyanzo vya ndani ya jeshi la polisi zinadai kwamba, hata wakiwa mahabusu ya kituo hicho, wawili hao wamekuwa wakioneshana mapenzi baina yao kitendo kilichowashangaza mahabusu wengine na polisi pia.
Uwazi lilifika nyumbani kwa Maua na kukutana na mdogo wake aitwaye Aziz ambaye alikiri kukamatwa kwa Maua na kwamba tangu akamatwe hajarudi na wala hajui kinachoendelea huku akisema asingependa kuzungumzia suala hilo kwa sababu ya kutupiwa lawama na wanandugu kwamba yeye ndiye aliyepeleka taarifa polisi.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Mary Nzuki.
“Mimi sikai hapa, nimefika hivi karibuni nikitokea mkoani. Ndugu wananituhumu mimi kuita polisi, sijui mtu aliyewapa askari namba yangu wakanipigia kama wageni wanaokuja nyumbani, nikawapa ramani na walipofika ndipo nikagundua ni askari,” alisema Aziz.
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, George Mtambalike alipohojiwa na gazeti hili ofisini kwake alithibitisha kukamatwa kwa wasichana hao kwa madai ya kufanya mapenzi ya jinsia moja na aliwatembelea Kituo cha Polisi cha Stakishari.
Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi Ilala, SACP Mary Nzuki alikiri kukamatwa kwao na akasema uchunguzi unaendelea.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate