EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 29, 2015

MGANGA WA DIAMOND JELA MIAKA 7

Stori: Richard Bukos/Amani
Yule mganga aliyejitapa kumtengenezea nyota ya mvuto staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya amehukumiwa kifungo cha miaka saba (7) jela baada ya kukutwa na hatia katika kisa cha kuchanganya akihusishwa na wizi wa gari.
Ustadh Yahya akiwa chini ya ulinzi.
TUJIUNGE MAHAKAMA YA WILAYA YA ILALA
Habari za uhakika zilieleza kwamba aliyehitimisha kesi hiyo ni Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Ilala jijini Dar, Hassan Kisailo mapema Jumatatu wiki hii wakati jua la asubuhi likiwaka.

HAKIMU ASHUSHA MIWANI
Huku kijasho chembamba kikimtiririka huku akishusha miwani kidogo kuona wahudhuriaji wa kesi hiyo, Hakimu Kisailo alitoa hukumu hiyo kwa maelezo kwamba, mnamo Januari 20, mwaka jana, maeneo ya Kariakoo jijini Dar, Yahya alidaiwa kuiba gari aina ya Toyota RAV4 lenye namba za usajili T 139 BSJ likiwa na thamani ya Sh. milioni 12, mali ya Edrick Elieza.
Wakati Hakimu Kisailo akisoma hukumu hiyo, mshtakiwa na wadhamini wake hawakuwepo mahakamani hapo hivyo alisema mara tu baada ya hukumu wahusika hao watakamatwa ili wakatumikie adhabu inayowakabili.
MAPITIO MTIRIRIKO WA KESI
Huku akiangalia kulia na kushoto, Hakimu Kisailo alisema kuwa, baada ya kuupitia mtiririko wa kesi hiyo, alibaini kwamba ni kweli mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo hivyo alimhukumu kwenda jela miaka 7.
...Ustadh Yahya akilaumu yambo.
BOFYA HAPA KUMSIKIA HAKIMU
Kama ilivyo desturi ya Magazeti ya Global kutaka kujua vitu kwa undani, mwanahabari wetu alizungumza hakimu huyo kuhusiana na hukumu hiyo ambapo alishusha tena miwani kidogo kisha kumwangalia kwa juu na kusema:
“Ni kweli huyo mnayemuita sijui Mganga wa Diamond nimemhukumu kwenda jela miaka 7, ingawa hakuwepo hapa mahakamani.
“Nasikia alitoroka tangu alipowekewa dhamana lakini kifungo hicho kitaanza muda wowote atakapokamatwa.”
WADHAMINI NAO WANALO
Hakimu Kisailo alisema kwamba, Ustadh Yahya aliwekewa dhamana na watu wawili, Moses Msangi na Seme Kisusandi ambao wanatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni moja kila mmoja au kwenda jela miezi sita wakati sangoma huyo akisakwa.
Hakimu Kisailo alisema licha ya jamaa huyo kuingia mitini, wadhamini wake nao hawakuwepo mahakamani hapo na kusema kuwa mkono wa sheria ni mrefu utawafikia popote pale walipo.
MANENO KUNTU
Mmoja wa mashuhuda wa kike aliyekuwa kwenye chumba cha hakimu huyo alisikika akisema: “Huyo mganga wa Diamond hana lolote, iweje ashindwe kuzima kesi yake na kufikia hatua ya kuhukumiwa kifungo hicho wakati huwa anajidai ni mkali kwenye mambo ya kuwatengenezea watu nyota?
“Unaweza kukuta huko mitaani anajifanya kuwaambia wateja wake ana uwezo wa kuzima ‘makesi’ makubwa-makubwa kumbe hata kesi yake mwenyewe inamshinda.”
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
DIAMOND ATUPIWA LAWAMA
Shuhuda huyo alikwenda mbele zaidi na kumtupia lawama Diamond kwamba alishindwaje kumsaidia mtu aliyempaisha hadi sasa hivi anawiki kimataifa?
DIAMOND ANASEMAJE
Amani lilimsaka Diamond ili kumfikishia ‘ubuyu’ kuwa mganga wake amehukumiwa miaka sasa jela lakini simu yake ya kiganjani iliita bila kupokelewa na hata alipofuatwa nyumbani kwake, Sinza-Mori, Dar, hakuwepo.
TUMEFIKAJE HAPA?
Ustadh huyo alidaiwa kukamatwa na gari hilo alilodai kufika mikononi mwake kutoka kwa mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mwanahamis. Ustadh alikamatwa  akikatiza nalo Tabora mjini ndipo akawekwa nyuma ya nondo za mahabusu kabla ya kusafirishwa jijini Dar kwa hatua zaidi za kisheria ambazo zimemhukumu kifungo hicho.
Habari ya kukamatwa kwa anayedai kuwa Mganga wa Diamond, iliandikwa kwa mara ya kwanza na Risasi February 22, 2014 kama inavyoonekana hapa chini......
EXCLUSIVE: MGANGA WA DIAMOND YAMEMKUTA
Stori: CHANDE ABDALLAH NA DENIS MTIMA
KIBAO kimegeuka! Yule mganga anayejitapa kumtengenezea nyota ya mvuto staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ustadh Yahya yamemkuta mazito.
Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zinaeleza kuwa jamaa huyo anahenyeshwa na polisi akiwa mahabusu kufuatia madai ya wizi wa gari aina Toyota Rav 4 ‘milango mitatu’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, gari hilo liliibwa wiki kadhaa maeneo ya Msimbazi-Kariakoo jijini Dar.
HABARI ZA AWALI
Habari za awali zilidai kuwa gari hilo lilifika mikononi mwa Ustadh kutoka kwa mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mwanahamis ambaye ilisemekana kwamba alikuwa akichukua dawa kwa mganga huyo.
Ilidaiwa kuwa mwanamke huyo naye alihongwa gari hilo na mume wa mtu huku akiwa hajui kuendesha hivyo aliliweka poni kwa Ustadh ambaye alimpa dawa ambayo aliipeleka Kigoma kuwauzia watu wake.
Endelea kusoma habari hii hapa ====> Bonyeza hapa

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate