EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, January 12, 2015

P-SQUARE WAKUBALI UWEZO WA DIAMOND

Stori: Musa Mateja MWACHENI Diamond aitwe Diamond! Hiyo kauli pekee unayoweza kuisema kufuatia wakali wa muziki wa R&B kutoka Nigeria, Peter na Paul Okoye ‘P-Square’ kuukubali uwezo wa kimuziki wa bwa’mdogo kutoka Tandale, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ijuma Wikienda linakupa mchapo hatua kwa hatua.
Bwa’mdogo kutoka Tandale, Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa madansa wake ndani ya Lagos, Nigeria.
NI LAGOS, NIGERIA
Wakali hao walionesha kumpigia saluti Diamond baada ya kukutana naye kwenye tamasha la utoaji wa Tuzo za Wanamichezo Bora Afrika lililofanyika Lagos, Nigeria, usiku wa kuamkia Januari 9, mwaka huu.

WALIANZIA HOTELINI
Kwa mujibu wa chanzo kilichoambatana na Diamond nchini humo, saa chache kabla ya shoo kuanza, P-Square walimuibukia kwenye Hoteli ya Eko aliyofikia jijini humo na kummwagia pongezi nyingi sambamba na kumshauri baadhi ya vitu vya kimaendeleo.
‘Diamond Platnumz’ akifurahia jambo na Peter Okoye wa 'P Square'.
TUJIUNGE NA CHANZO
Chanzo hicho kilisema, P-Square walionekana kuvutiwa zaidi na juhudi binafsi za Diamond kiasi cha kuweza kuipeperusha bendera ya Afrika Mashariki katika levo za kimataifa.
“Jamaa walipomuona tu hotelini waliguswa sana na juhudi zake binafsi maana wanatambua jinsi gani muziki ulivyokuwa mgumu kuuvusha nje ya nchi yako lakini kwa kuwa Diamond ameweza, walimpigia saluti,” kilisema chanzo hicho.

ARUHUSIWA KOLABO
Chanzo hicho kilizidi kumwaga data za ndani kwa kusema, mbali na kumpigia saluti, P-Square walionesha wako tayari kumsapoti Diamond kwa kumpa nafasi ya kufanya nao kazi yaani kolabo.
“Wamempa nafasi ya kufanya naye kazi pale atakapojisikia kutokana na mipango yake, kama akiamua kufanya sasa au baadaye ni uamuzi wake lakini jamaa (P-Square) hawana kinyongo naye lengo lao ni kuona muziki wa Afrika unateka dunia,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
‘Diamond Platnumz’ akiwa na Paul Okoye wa 'P Square'.
“Walimwambia the way (namna) alivyo na juhudi kwenye kazi yake anatambulika Nigeria utafikiri ni msanii kutoka Nigeria, walimpa mbinu zao za namna walivyopigana hadi kufika hapo walipo.”
MASTAA WAMUIBUKIA
Mbali na P-Square, mastaa mbalimbali wa Nigeria walimuibukia Diamond hotelini hapo akiwemo Mr Flavour na Jude Abaga ‘M.I’, ambao walimpa pongezi Diamond kwa kujua kumiliki vyema jukwaa kwani wamekuwa wakifuatilia shoo zake hasa anapotupia video zake mitandaoni.
Msanii wa muziki kutoka Nigeria, Mr Flavour akiteta jambo na 'Diamond Platnumz'.
APIGA SHOO YA MAANA
Ulipofika wakati wa kupanda jukwaani, Diamond aliitikisa Nigeria kwani alionesha vitu vya tofauti wakati akiimba nyimbo zake na kuwafanya Wanigeria na waalikwa mbalimbali wapigwe na butwaa huku wengi wakiishia kumpigia makofi na shangwe la kufa mtu.

DIAMOND ANASEMAJE?
Mwanahabari wetu alimcheki Diamond kupitia mtandao wa WhatsApp ambapo aliwashukuru mastaa hao wa Nigeria kwa upendo wao na kuahidi kuendelea kufanya maajabu zaidi katika levo za kimataifa.
“Wana wamenisapraizi hotelini, tumepiga stori nyingi, wameonesha wanakubali kile ambacho mimi nafanya, jukwaani nimefanya vizuri, watu na heshima zao mwishoni walipiga makofi kuonesha wamekubali.
Mkali wa Bongo Fleva kutoka Bongo, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz' akiwa na madansa wake.
KUHUSU KOLABO?
“Kuhusu kolabo na P-Square, ni mapema sana kuzungumzia kwa kuwa nina mipango mingi ya kufanya mwaka huu, mashabiki wakae mkao wa kula, nikiona inafaa, nitafanya nao maana wao hawana shida na mimi,” alisema Diamond.

P-SQUARE NI ZAIDI YA DAVIDO
Awali, kabla Diamond hajakutana na P-Square, alishirikiana na mkali mwingine wa Nigeria, Davido katika wimbo wake wa Number One Remix ambaye inaaminika kwa umaarufu na uwezo wa kimuziki yupo chini ya P-Square.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate