EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, January 13, 2015

MAZISHI MKE WA BILIONEA MIL. 200



Hii ndiyo ajali iliyoondoa uhai wa Carista Charles Makoi (52).
Stori: Joseph Ngilisho, ARUSHA/UWAZI
MAZISHI ya Carista Charles Makoi, 52, (pichani), ambaye alikuwa mke wa mfanyabiashara bilionea jijini hapa, Charles Makoi yamefanyika huku shilingi milioni 200 zikisemekana kuteketea kwa bajeti.
Mfanyabiashara maarufu jijini hapa, Patrick Ngiloi ambaye ni mmiliki wa vituo vya mafuta vya Kampuni ya Panone ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya mazishi hayo.
Baadhi ya wananchi wakishuhudia ajali iliyosababisha kifo cha Carista Charles Makoi.
Kwa mujibu wa chanzo makini ndani ya kamati hiyo, siku ya kwanza tu baada ya kifo hicho, saa tatu mbele zilichangwa zaidi ya shilingi milioni 75 na baada ya hapo ziliendelea kuchangwa hadi kufikia lengo.
WACHANGAJI WAKUBWA
Chanzo kilisema kuwa, wachangaji wakubwa walikuwa wafanyabiashara wakubwa kutoka mikoa ya kaskazini mwa Tanzania, ikiwemo Arusha, Kilimanjaro na Tanga.“Wengi waliowahi kuchanga ni wafanyabiashara wa mikoa hiyo niliyokutajia. Lakini tulidhamiria bajeti iwe ya milioni mia mbili. Unajua shughuli ni shughuli siku zote.

“Tunaposema milioni mia mbili tulimaanisha kwa ajili ya kununulia vinywaji, kama bia, maji na soda. Pia vilinunuliwa vyakula mbalimbali, jeneza, sare na kuandaa mahali pa kukaa waombolezaji kutoka sehemu mbalimbali. Waombolezaji walikuwa wengi sana ndiyo maana bajeti ilikuwa kubwa.
“Kwa kweli tulikwenda sawasawa, hakuna mahali tulikwama. Ni bajeti ya aina yake hii,” kilisema chanzo hicho na kuomba hifadhi ya jina lake.
...Wananchi wakiutoa mwili wa Carista Charles Makoi baada ya kubanwa kwenye gari.
WALIVYOSEMA WAOMBOLEZAJI
Baadhi ya waombolezaji walisikika wakiteta kuwa, bajeti hiyo ilitosha kufanya miradi kadhaa ya maendeleo kama kununua madawati, vyandarua mahospitalini na magari kwenye vituo vya afya.
“Mfano, nimesikia kwamba jeneza peke yake ni shilingi milioni saba, si unaweza kununua Toyota Vitz?” alihoji mwombolezaji mmoja na kujibiwa na mwenzake kwamba, mawazo kama hayo ni kuingilia uhuru wa familia ya marehemu.
“Marehemu alikuwa na gari zaidi ya Vitz, unaposema inaweza kununua Vitz unamaanisha nani sasa? Wakupe wewe ukanunue au ndugu yako? Huko ni kuingilia uhuru wa familia ya marehemu,” alihoji mwombolezaji mwingine.
MAZISHI YA AINA YAKE KIBOSHO
Baada ya msiba Arusha, msafara ulianza kuelekea Kibosho mkoani Kilimanjaro ambako marehemu alizikwa Ijumaa iliyopita nyumbani kwa familia hiyo, Sambani, Kibosho.Yalikuwa mazishi ya kwanza kwa idadi kubwa ya waombolezaji kutoka Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Mwanza, Dar es Salaam, Morogoro huku magari ya kifahari yakiwa mengi.WAOMBOLEZAJI WALIACHA BIA
Wakati wa msiba huo uliokuwa maeneo ya Sakina jijini hapa, waombolezaji wanaopata ‘yale mambo’ walikunywa pombe mbalimbali zikiwemo bia na ilifika mahali walizikodolea macho kwa kinai kama si kulewa.
“Da! Hii balaa, hapa mtu usipojiangalia unaumbuka hivihivi unajiona, mimi bia basi tena, sasa nakwenda na maji kwanza,” alisikika akisema mmoja wa waombolezaji msibani siku ya kwanza.
MAKOI NI NANI?
Mume wa marehemu Carista, Charles Makoi anamiliki hoteli maarufu iliyopo jijini Arusha inayojulikana kwa jina la Aquiline (ghorofa 7), vituo vya mafuta Arusha na Moshi, maduka ya bidhaa mbalimbali jijini Dar, Morogoro, Kilimanjaro, Iringa na Tanga.
Anaishi kwenye nyumba kubwa ya kifahari iliyopo Sakina.
TUJIKUMBUSHE
Marehemu Carista alipata ajali Januari 5, mwaka huu baada ya gari alilokuwa akiendesha kutoka Moshi kwenda Arusha, Mitsubishi Pajero lenye namba za usajili T 930 AVZ kugongana uso kwa uso na basi aina ya Hino (Mrindoko Trans) lenye namba za usajili T 312 AVG maeneo ya Kikatiti, Arumeru, Arusha.
Carista Charles Makoi enzi za uhai wake.
Katika ajali hiyo, marehemu alifariki dunia papohapo huku wifi yake,  Jamhuri Makoi akifia Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi na mtoto wa marehemu, Brayan Makoi aliyekuwa amekaa siti ya nyuma akijeruhiwa vibaya. Hadi sasa amelazwa chumba cha uangalizi maalum (ICU) hospitalini hapo.
Marehemu Carista ambaye siku ya tukio alivaa shati maafuru kwa jina la ‘makenzi’ rangi ya bluu na nyeupe, aliumia kichwani na kifuani na alibanwa na bodi ya gari kiasi kwamba, ili kuutoa mwili wake ilibidi wasamaria wema kutumia shoka kukata mabati sanjari na kuondoa paa la gari hilo.
KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas alisema dereva wa basi bado anashikiliwa na polisi kwa uchunguzi zaidi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate