EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, January 9, 2015

TIKO: SIJUI HATA IDADI YA WANAUME NILIOTOKA NAO

Mwanadada anayefanya vizuri kwenye muziki na uigizaji wa filamu Bongo, Tiko Hassan.
Stori: Gladness Mallya
Leo mwandishi wetu Gladness Mallya amemnasa mwanadada anayefanya vizuri kwenye muziki na uigizaji wa filamu Bongo, Tiko Hassan. Unataka kujua ameulizwa maswali gani na akajibu vipi? Fuatilia hapa chini.

Ijumaa: Wasanii wengi mna tabia ya kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja, yaani yupo wa kukupa fedha, wa mapenzi na wa kujirusha tu sehemu mbalimbali za starehe, vipi kwako likoje hili?
Tiko: Ukweli mimi huwa nikiwa na mwanaume mmoja natulia naye huyohuyo, tukiachana ndiyo nakuwa na mwingine, hiyo tabia ya kuwa na wanaume wengi sina na siipendi kabisa.
Ijumaa: Unazungumziaje tabia ya nyie wasanii wa kike ‘kushea’ mabwana bila aibu?
Tiko: Tabia hii inakera sana na ni ushamba. Mimi sijawahi kumchukua mwanaume wa mtu maana najiamini kama mwanamke, wanaotuharibia sifa ni hao wengine maana lisemwalo lipo.
Ijumaa: Kuna tetesi kwamba wasanii wengi mnafanya mapenzi kinyume na maumbile ili wapenzi wenu wasiwaache, wewe umeshawahi?
Tiko: Sijawahi kufanya wala sifikirii maana hata vitabu vya dini vinakataza, huwa natumia uanamke wangu kumridhisha mpenzi wangu lakini siyo kufanya uchafu huo.
Ijumaa: Je, unakwepaje vishawishi vya wanaume wakware mtaani ambao wakiona wasichana warembo kama wewe hutumia nguvu zote kuwanasa?
Tiko: Huwa nakaza moyo na ninafikiria mbele zaidi maana najua wapo watu nyuma yangu wanaoniangalia na kunitegemea hivyo inanipa nguvu ya kuvishinda vishawishi.
Ijumaa: Siku hizi matumizi ya dawa za Kichina za kuongeza makalio na matiti yamezidi, je ulishawahi kutumia?
Tiko: Hivi unanionaje? Cheki nilivyo, kufungashia huku ni kwa asili na hata matiti yangu pia hayana uhusiano na dawa za Kichina. Waliozaliwa hawana shepu ndiyo wanaohangaika.
Ijumaa: Hivi mpaka sasa umeshatoka na wanaume wangapi?
 Tiko: Ukweli sikumbuki wanaume niliotoka nao maana idadi yao mh!
Ijumaa: Ni changamoto gani unazokutana nazo kwenye kazi yako ya muziki na filamu?
Tiko: Changamoto zipo nyingi tu, wapo wanaotukatisha tamaa lakini kwa kuwa tumedhamiria kwenye fani, naamini tutashinda.
Ijumaa: Kuna wanaosema wewe huwezi kuimba ila unafuata mkumbo, hilo unalizungumziaje?
Tiko: Ndiyo changamoto ninazozizungumzia hizo, kama siwezi kuimba mbona kazi zangu zinakubalika mtaani? Hayo ni maneno ya watu wasiopenda maendeleo yangu.
Ijumaa: Sasa hivi umeelekeza nguvu zako kwenye muziki, vipi filamu umeacha?
Tiko: Filamu sijaacha na siwezi kuacha ila kwa sasa macho yangu yapo zaidi kwenye muziki.
Ijumaa: Kuna hizi rushwa za ngono kwa wasanii wanaoingia kwenye fani ya muziki na filamu hasa kwa wasichana, wewe hujakumbana na kutakwa ili ‘ushaini’?
Tiko: Kikubwa ni kuwa na msimamo, hayo mambo yapo lakini inategemea unajiwekaje, ukijirahisi wanakupitia kweli.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate