EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, January 16, 2015

TUHUMA NZITO: MAMA AMCHARANGA VIWEMBE MWANAYE

Stori: Gabriel Ng’osha na Denis Mtima/Ijumaa
Unyama wa kutisha! Mama mzazi aliyetajwa kwa jina la Feromena, mkazi wa Meko-Mtongani, Kunduchi jijini Dar, anatuhumiwa kumcharanga viwembe mwanaye wa kumzaa aliyetajwa kwa jina moja la Zena mwenye umri wa miaka kumi.
Mtoto anayefahamika kwa jina la Zena anayedai kunyanyaswa na mama yake.
Tukio hilo la kulaaniwa lilijiri Jumanne wiki hii nyumbani kwa mwanamke huyo maeneo hayo ambapo mama huyo inadaiwa alimsulubu mwanaye huyo anayesoma darasa la nne katika Shule ya Msingi Mtakuja.

Sehemu ya majeraha ya viwembe kichwani kwa mtoto Zena.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, mama huyo alidaiwa kumfungia ndani mwanaye huyo na kuanza kumpa kipigo cha mbwa mwizi.Walidai kwamba ukiachana na siku hiyo, mama huyo amekuwa akimsulubu mwanaye huyo mara kwa mara kwa kumcharanga viwembe na vitu vyenye ncha kali hivyo kumwachia majeraha sehemu mbalimbali za mwili.
Sehemu ya majeraha yaliyo mgongoni mwa zena.
Mjumbe wa mtaa huo aliyejitambulisha kwa jina la Elizabeth Mziga alikiri kupokea malalamiko kutoka kwa majirani juu ya unyanyasaji na uteswaji wa mtoto Zena.Mjumbe huyo alisema kuwa tuhuma hizo alishazifikisha polisi ambapo mama huyo alikamatwa lakini baada ya muda alionekana akidunda mtaani kama kawa.
Mama mzazi wa mtoto Zena,Bi.Feromena akibanwa kwa maswali.
Baada kujazwa habari na majirani na mjumbe huyo, kile kikosi kazi cha Oparesheni Fichua Maovu cha Global Publishers kiliingia mzigoni ambapo kilianza kwa kumsaka mtoto huyo na kuzungumza naye.
Alipopatikana, mtoto Zena alieleza namna mama yake alivyokuwa akimfanyia matendo ya kinyama huku akimnyima haki ya msingi ya kwenda shule.
Mama Zena, Bi. Feromena akiwa chini ya ulinzi.
Alisema mama yake amekuwa akimtuhumu kumwibia fedha zake na kwenda kutumia shuleni hivyo hakupaswa kurudi tena shuleni na kuongeza kuwa siku ambazo alikuwa akilala kwa amani ni zile ambazo alikuwa ametoroka nyumbani na kwenda kulala kwa majirani.
Wananchi wakishuhudia mkasa huo wa kusikitisha.
OFM ilishuhudia mwili wa Zena ukiwa na makovu na kuvimba huku akidai kuwa aliunguzwa na ‘frampeni’ (kikaangio) hasa sehemu za kiunoni na mgongoni.Alisema mama yake alimtishia kuwa endapo atamwambia baba yake atakiona cha mtema kuni.
“Jamani mama amekuwa akinipiga na kunikata viwembe bila kuniambia kosa langu. Naombeni msaada nateseka,” alisema Zena kwa masikitiko makubwa.OFM, kwa kwa kushirikiana na mjumbe wa eneo hilo walikwenda kuripoti tukio hilo kwenye Kituo Kidogo cha Polisi cha Mtongani lakini hakukuwa na dawati la jinsia hivyo polisi walikwenda kumkamata mama huyo kwa ajili ya kumpeleka kituo kikubwa.
Moja ya wazee akionesha jalada la kesi aliyofunguliwa mama zena.
Kwa upande wake mama huyo alipoulizwa sababu hasa ya kumsulubu mwanaye alisema si kweli bali anachojua ni siku moja aliyompiga baada ya kuchukua fedha zake na kwenda kununulia maandazi.
“Sijui aliyemkatakata viwembe,” alisema mama Zena kwa kifupi.
Baada ya kufikishwa kwenye kituo kikubwa cha Polisi cha Kawe, mama huyo alifunguliwa jalada la kesi namba KW/RB/439/015-SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI hivyo anasubiri kufikishwa kwenye mkono wa sheria.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate