EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, January 1, 2015

USIWE MBULULA, UNA HAKI YA KUPENDA ILA ‘USIFOSI’ MAPENZI!

Awali ya yote nimshukuru Mungu kwa kunifanya kuwa miongoni mwa wale waliouona mwaka wa 2015 wakiwa wazima. Hili ni jambo la kumshukuru sana Mungu kwani najua wapo waliotamani kuuona mwaka huu wakiwa wazima lakini leo hii wameshatangulia mbele za haki huku wengine wakiwa hoi kwa magonjwa.
Kikubwa ni mimi na wewe ambao tumepata neema hii kuendelea kufanya yale yanayompendezesha Mungu na kuachana na yale yanayomchukiza. Kwa kufanya hivyo mwaka huu utakuwa ni wa furaha kwetu na hata kama mapenzi yamekuwa yakituliza kwa mwaka uliopita, tutafurahia maisha kama wengine.

Mpenzi msomaji wangu, ukijaribu kutafuta maana halisi ya mapenzi utapata tafsiri nyingi sana lakini kwa ninavyojua mimi, mapenzi ni hisia ambazo zipo moyoni mwa mtu kwenda kwa mwingine.
Hisia hizi ili ziweze kuwa mapenzi ni lazima ziwe na ukweli na za dhati huku moyo ukiwa na nafasi kubwa katika hilo.
Hii ndiyo maana ya harakaharaka ya mapenzi. Najua na wewe unaweza kuwa na tafsiri yako lakini leo tusimamie kwenye hii ili niweze kukufikishia kile nilichodhamiria.
Ukweli ni kwamba, unapoingia katika uhusiano wa kimapenzi na mtu uliyetokea kumpenda sana hupaswi kuwa na mtu mwingine kwa kuwa, kufanya hivyo utakuwa unaunyima haki moyo wako.Ndiyo maana kila siku tunasisitizwa kuwa waaminifu na kuridhika na mapenzi kutoka kwa wale tunaowapenda. Hata hivyo, hali sasa hivi imebadilika, maana ya mapenzi imepotoshwa kwa kiwango kikubwa kiasi kwamba sasa umebaki usanii tu.
Leo hii unaweza kumpenda mtu f’lani, ukawa hulali, huli wala kufanya kazi zako vizuri kutokana na unavyomfikiria huyo uliyetokea kumpenda. Hiyo ni hali ya kawaida kwenye mapenzi.Hata hivyo, wewe unaweza kuwa katika hali hiyo lakini cha ajabu huyo unayempenda wala hana taimu na wewe na unaweza kujitahidi kufikisha hisia zako na zikapuuzwa.
Hapo ndipo baadhi wanapofikia hatua ya kuchanganyikiwa na kuhisi hawana thamani. Wanajihisi hivyo kwa kuwa penzi lao halithaminiwi.Nadhani katika hili kuna kitu tunakosea. Hivi unadhani kila utakayetokea kumpenda naye lazima akupende na akubali kuwa na wewe? Ni wangapi ambao huenda wameshawahi kukutokea na kukueleza kuwa wanakupenda sana lakini wewe mwenyewe huna hata chembe ya mapenzi juu yao?
Kama wapo, cha ajabu ni kipi wewe kumpenda f’lani lakini yeye akaonesha kutokuwa na mapenzi na wewe? Kwa nini uumie sasa? Mimi sidhani kama kuna sababu ya kuumia. Ni kweli una haki ya kupenda lakini kama utagundua umependa pasipo na penzi wala huna haja ya kujiona usiye na thamani.
Nilishawahi kusema huko nyuma kwamba, asilimia kubwa wapo kwenye uhusiano na watu wasiowapenda. Hii ni kwa sababu ni nadra sana kumpenda mtu na yeye akawa anakupenda kama unavyompenda wewe.
Jaribu kufuatilia utagundua kwamba ndoa nyingi zinayumba na nyingine zinavunjika kwa kuwa, mmoja hana mapenzi ya kweli kwa mwingine. Wapenzi nao wengi wao wanaishi ili mradi siku zinakwenda na ikitokea wameachana kuna mmoja kati yao atachukulia poa na mwingine ataumia kwa kuwa alipenda zaidi.
Kwa maana hiyo basi ukae ukijua kwamba, kumpenda mtu kisha yeye akawa haoneshi kukupenda wala siyo tatizo, tatizo litakuja tu pale ambapo wewe utakuwa hujagundua kuwa hupendwi. Kwa bahati ukimpenda mtu kisha Mungu akakujaalia ukagundua kuwa yeye hakupendi, chukulia kuwa hiyo ni hali ya kawaida na uamuzi sahihi ni kuamua kuachana naye.
Kosa kubwa ambalo utalifanya ni kung’ang’ania kumpenda mtu ambaye anaonekana kutokuwa na mapenzi na wewe. Kwa nini umuendee mtu kwa mganga eti ili akupende? Hivi unadhani yeye ndiyo yeye na hakuna mwingine wa kuwa na wewe?
Acha umbulula, una kila sababu ya kuhakikisha unajiweka katika mikono salama. Ikiwa umempenda mtu kisha unapomueleza hisia zako haoneshi kujali, mtoe katika moyo wako.
Kumbuka ukiendelea kumsumbua, itafika wakati ataona akukubalie tu akijua atakupelekapeleka, atakutumia na mwisho atakuacha. Ni wangapi ambao unawajua sasa hivi wanalia kwa sababu wamelazimisha mapenzi? Ni wengi sana huko mtaani hivyo ni vyema wewe ukajitoa kwenye kundi hilo. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate