EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 9, 2015

BABA APIGWA PINGU KWA KUMTESA MTOTO

Hekaheka! Baba mkubwa aliyetajwa kwa jina la Mohamed Said a.k.a Muddy, mkazi wa Tegeta-Msufini jijini Dar amepigwa pingu akituhumiwa kumfanyia ukatili wa kutisha wa kumsulubu mtoto wa kiume wa mdogo wake, mwenye umri wa miaka sita (jina linahifadhiwa).
Baba mkubwa aliyetajwa kwa jina la Mohamed Said a.k.a Muddy akiwa amepigwa pingu kwa madai ya kumtesa mtoto wa mdogo wake.
Tukio hilo kusikitisha lilijiri Februari 6, mwaka huu maeneo hayo ambapo awali inadaiwa kuwa Muddy alimchukua mtoto huyo kutoka kwa wazazi wake wanaoishi mkoani Mtwara kwa lengo la kuja naye Dar kwa ajili ya kumsomesha.

DOZI YA VIPIGO
Ilidaiwa kwamba, kinyume na lengo hilo, jamaa huyo alipomfikisha Dar alianza kumfanyia ukatili wa dozi ya vipigo.
Mama mzazi wa mtoto huyo(kushoto) akilia kwa uchungu.
KILIO CHA MAJIRANI
Wakizungumza na Ijumaa Wikienda juu ya tukio hilo, majirani walisema kuwa jamaa huyo amekuwa akimshushia kipigo mtoto huyo mara kwa mara kwa kutumia mti wa ufagio, bomba la plastiki na waya wa umeme huku adhabu kama kumnyanyua miguu juu kichwa chini, kumnyanyua juu kwa kumshika masikio na kushinda muda mrefu bila kula vikiwa ni sehemu ya maisha ya mtoto huyo.
TAARIFA KWA MJUMBE
Majirani hao walidai kuwa walichoshwa na vitendo hivyo na kila walipomkataza Muddy, waliambulia vitisho jambo lililowafanya watoe taarifa kwa Mjumbe wa Shina, Maulid Mheza ambaye aliahidi kulifanyia kazi.
Sehemu ya majeraha mguuni aliyopata mtoto huyo baada ya kuteswa.
SIKU YA TUKIO
Habari zilidai kwamba, siku ya tukio, majira ya asubuhi, Muddy alimwangushia mtoto huyo kipigo kilichomsababishia majeraha sehemu mbalimbali za mwili hadi akaishiwa nguvu.
Ilidaiwa kwamba majirani walipoona hali ya hatari, walitoa taarifa kwa mjumbe wao ambaye alifika nyumbani kwa Muddy akiwa na polisi kutoka Kituo cha Wazo Hill.
MTOTO APUMUA
Wakiwa nyumbani kwa mtuhumiwa huyo walimkuta mtoto huyo akiwa hoi hivyo alipowaona alipumua na kumshukuru mjumbe kwa kufika huku akiwaonesha mahali alipo baba yake ambapo alikuwa akioga bafuni.
Msamaria mwema akiwa na mtoto huyo.
MTUHUMIWA ATOKA KWA MBINDE
Muddy alipoamriwa na polisi atoke bafuni, alitoa lugha chafu jambo lililowafanya askari hao kutumia nguvu kwa kupiga risasi tatu hewani na nguvu za watu watano ndizo zilizofanikisha kumpandisha kwenye karandinga kwa kuwa alikuwa na nguvu za ajabu.
MWENYEWE AJITETEA
Katika utetezi wake, Muddy alisema kuwa alikuwa akimpiga mtoto huyo kwa kuwa hakuwa akielewa wakati alipomfundisha kusoma.
Mjumbe wa Shina, Maulid Mheza akimbeba mtoto huyo.
MJUMBE ATAHARUKI
Akizungumza na waandishi wetu, Mjumbe Mheza alisema kuwa hali aliyomkuta nayo mtoto huyo ilimshtua kwani alikuwa hawezi kutembea wala kuzungumza vizuri kutokana na woga huku mwili wake ukiwa umevimba na kujaa makovu yaliyotokana na vipigo kutoka kwa baba yake huyo.
MTOTO AJAZA UMATI POLISI
Katika hali ya kushangaza kila mtu aliyesikia habari za mtoto huyo alifika kituo cha polisi kujionea kwa macho yake hali iliyowalazimu polisi kuwatawanya kutokana na kuongezeka kwa idadi yao.
RB aliyokatiwa mtuhumiwa kwa shambulio la kudhuru mwili.

VILIO
Naye mama mtu aliyekuwa ametua Dar alipopigiwa simu na mjumbe alifika kituoni hapo na kuungana na wanawake wengine kuangua vilio baada ya kumuona mwanaye akiwa katika hali mbaya kiafya.
Hadi Ijumaa Wikienda linaanua jamvi kituoni hapo, mtuhumiwa alikuwa akishikiliwa na polisi kwa jalada la kesi namba WH/RB/1101/2015 -SHAMBULIO LA KUDHURU MWILI huku mtoto huyo akikabidhiwa kwa mama yake ambaye alipewa fomu ya matibabu P-F3 kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa afya kiafya.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate