EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 24, 2015

KAKA ADAIWA KUMTOROSHA DADA YAKE KWA MUME

ALLY Issa anayeishi Mombasa nchini Kenya, anadaiwa kumtorosha dada yake Hasina Issa (22)  aliyekuwa akiishi na mumewe, Baraka Ally (32), Mbezi Mwisho jijini Dar es Salaam.Tukio hilo lilitokea siku ya mkesha wa Siku ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’.
Hasina Issa siku ya harusi yake.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Ally alisema alitoa taarifa polisi na kufunguliwa jalada namba KMR/RB/1996/15 Kimara, akiamini mke wake ametoroshwa.
Alisema mkewe huyo, aliyemuoa Julai 6, mwaka 2013 Tandale, alitoweka baada ya kaka yake huyo akiwa na mkewe Mzungu, kuwatembelea nyumbani kwao.

“Ninakumbuka siku mbili kabla ya kutoroshwa, nikiwa kazini, shemeji yangu mmoja alinipigia simu akiniambia nikamuone shemeji yangu mwingine wa Mombasa ambaye alikuwa amekuja na mwanamke wa Kizungu.
“Nilipotoka kazini nilikwenda Tandale ambako nilimkuta akiwa na huyo Mzungu, alisema ametutembelea hivyo niwapeleke kwangu, wana hamu ya kumuona mke wangu.“Walikodisha teksi hadi nyumbani, tulifika saa mbili usiku, wakasema kisipikwe chakula bali tukale hotelini, tulifurahi sana, wakawa wanatupiga picha, baadaye wao walienda hotelini Sinza walikofikia wakiahidi kurejea kesho yake.
“Lakini nikapata safari ya kikazi kwenda Mtwara kwa siku moja, niliporudi mke wangu alinikaribisha vizuri, asubuhi nikaenda kazini, nikiwa njiani alinipigia simu mara nne kwa nyakati tofauti akiniuliza nilipokuwa, haikuwa kawaida yake kufanya hivyo.
“Muda si mrefu nami  nikawa nampigia hadi mara tano lakini hakupokea, nilipotuma ujumbe hakujibu, nilipofika nyumbani sikumkuta,” alisema Ally.Aliongeza kuwa alipojaribu kumpigia shemeji yake kumuulizia alipokuwa dada yake, alimjibu kuwa hajui kwani kwa wakati huo alikuwa mjini Bukoba akiwa njiani kuelekea Uganda.
Alisema alipowasiliana na wakwe zake Tandale, Dar alitakiwa kwenda huko, lakini cha kushangaza alipofika, alitakiwa kuandika talaka ya kumtaliki mkewe.
“Nikawauliza nitatoaje talaka wakati mke wangu hayupo? Sasa nitampa nani? Simu zao hazipatikani, ila mmoja wa shemeji zangu anayenipenda aliniambia mke wangu alionekana na kaka yake wa Mombasa kituo cha mabasi Ubungo, ndipo nikaenda kutoa taarifa polisi.”
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate