EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, February 24, 2015

MAITI YA MCHUNGAJI YAZUA TAFRANI

MAITI ya Mchungaji James Regnald Mhando  aliyefariki  Februari 18, mwaka huu imezua tafrani nzito kwa ndugu na jamaa baada ya kujulikana kuwa alikuwa na wake wawili ambapo mke mmoja alitaka mwili uagwe hospitali na upande wa pili ukitaka ukaagwe kwa mama yake marehemu.
Mchungaji James Regnald Mhando enzi za uhai wake.
Katika msiba huo ilibainika kuwa, mchungaji huyo (kanisa lake tunalihifadhi kwa sababu maalum), alikuwa na watoto sita kwa mama tofauti na wote walijitokeza katika mazishi ya baba yao.
Inadaiwa  kuwa Mchungaji Mhando alianza kuumwa Jumamosi ya Februari 14, mwaka huu lakini inadaiwa baadhi ya watoto na ndugu wengine hawakujulishwa hadi Jumanne ambapo inadaiwa alibebwa na gari la wagonjwa kutokea Morogoro hadi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Jeneza la mchungaji James Regnald Mhando.
Habari zinasema ilipofika Jumatano saa tano usiku, mchungaji huyo aliaga dunia na mbali ya kuaga dunia, bado tukio hilo lilikuwa ni siri na ilidaiwa ilikuwa afanyiwe shughuli za mazishi kwa siri bila ya baadhi ya watoto wake wakubwa kujua.

Hata hivyo, habari za msiba huo zilizagaa haraka na kumfikia mke wa kwanza wa ndoa ambaye alikuwa nchini kwa ajili ya mapumziko kwani anafanya kazi nje ya nchi, hivyo ukoo ukaanza kutaarifiana.
Mchungaji Mhando alioa na kufunga ndoa Novemba 17,  1979  katika Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano, jijini Dar es Salaam,  hata hivyo,  ilidaiwa kuwa mwaka 1985 mtumishi huyo wa Mungu aliamua kuondoka nyumbani alikokuwa akiishi na mkewe na kwenda kuishi na mwanamke mwingine ambaye inadaiwa kuwa alikuwa ni wa dhehebu lingine na wakafunga ndoa serikalini.
Habari zinadai kwamba mwanamke huyo alikuwa anaitwa Mwanaheri kabla ya kubadili dini na kuitwa Glory na wakafanikiwa kuzaa  watoto wawili, mmoja akapewa jina la Reginald Junior na mtoto mwingine anaitwa Sada au Doreen Mhando. Habari zinasema kabla ya kuondoka kwa mke wa kwanza, mchungaji huyo alizaa naye watoto wawili, wa kiume na wa kike....Askari akiwa eneo la tukio.
Hata hivyo, wakati wa msiba huo watoto wengine wawili walijitokeza nao wakidai kuwa ni baba yao, hali iliyozusha minong’ono kwa watu walioshangazwa na mwenendo wa marehemu.Akizungumza na Uwazi, mama mzazi wa mchungaji huyo aliyejitambulisha kwa jina la Dorofea Mhando (82) alisema kitendo kilichofanywa na mwanamke huyo ni kibaya kwani alimshawishi mwanaye kuisaliti familia yake.
“Mwanamke huyo mwingine alikuwa akiishi na mwanangu kwa siri kubwa  sana, kama vile marehemu hakuwa na familia na akawa anajifanya kuwa yeye ndiye mke wa kwanza, kitu ambacho ni cha uongo kwani marehemu alishaoa kanisani mwaka 1979.
“Marehemu baada ya kumpata mwanamke huyo alikuwa hashiriki shughuli nyingi za hapa nyumbani kwa kuhofia watu  watajua kuwa alikuwa na familia nyingine,  kitu ambacho kilinisikitisha,” alidai mama huyo.
Mwili wa marehemu ukiagwa.
Mama  huyo aliongeza  kuwa  maisha ya mchungaji huyo yalikuwa sehemu mbili, Morogoro na jijini Dar  es Salaam, alikuwa akifikia Mivinjeni kwenye ofisi ya shughuli zake.“Baada ya kupata taarifa ya msiba niliagiza mwili uletwe hapa Ukonga Majumba Sita ukitokea Muhimbili kwa ajili ya shughuli za kuagwa lakini mke mdogo akawa anapinga,” alidai mama huyo.
Hata hivyo, ilidaiwa kuwa mke mdogo alisisitiza kuwa baada ya kuandaa mwili wa marehemu uagwe Muhimbili, kisha  upelekwe katika Makabauri ya Kinondoni kwa mazishi.   Kulitokea mabishano ambapo mtoto mkubwa wa marehemu aliyefahamika kwa  jina Feda, alisema  baba yao hawezi  kuagwa kama mkimbizi kwani ana watoto, mke na mama yake mzazi, hivyo akaamuru mwili ukaagwe kwa bibi yake Ukonga Majumba Sita.
Habari zinadai kuwa mvutano huo ulifikishwa Polisi Kituo Kikuu ambapo lilifunguliwa jalada namba CD/ RB/ 2627/ 2015 ambao waliamuru shughuli za mazishi zisifanyike hadi muafaka upatikane.
Habari zinadai kikao kilifanyika polisi na muafaka ukapatikana kwamba mwili ukaagwe kwa mama yake mzazi Ukonga Majumba Sita.
Maofisa wa polisi walitoa askari wenye silaha chini ya kamanda wao aliyefahamika kwa jina moja la Manyama aliyeongozana na wana familia hao hadi Muhimbili kisha Ukonga, baadaye kwenye Makaburi ya Kinondoni ambapo mchungaji huyo alizikwa chini ya ulinzi.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate