EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 6, 2015

NAPE AWAKABIDHI MATREKTA WAKULIMA NI YALE YANAYOTOLEWA KWA MKOPO NA KAMPUNI YA KARIATI TRACTOR‏

 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kariati Tractor ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kwadelo, Omary Kariati (kulia), akisalimiana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye alipofika kuwakabidhi matrekta wakulima kutoka mikoa mbalimbali Dar es Salaam jana mchana.

 Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye akisalimiana na Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Edmund Mndolwa mara baada ya kuwasili kwenye hafla hiyo ya kukabidhi matrekta.
 Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Edmund Mndolwa (kulia), akimuelekeza jambo Nape.
 Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Edmund Mndolwa akijaribu kuendesha moja ya matrekta hayo.
 Mwalimu Hamza Haji mmoja wa wanufaika wa mkopo wa matrekta hayo akizungumza na waandishi wa habari.
 Mkulima Khalifa Kuluvi kutoka Kata ya Kwadelo akizungumza na waandishi wa habari.
 Mhe. Nape Nnauye akitia saini kwenye kitabu cha wageni katika ofisi ya Kampuni ya Kariati Tractor.
 Baadhi ya matrekta waliogaiwa wakulima hao pamoja Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Edmund Mndolwa ambaye amenunua ekari 100 kwa ajili ya kutekeleza mpango wa kilimo kwanza.
Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye (katikati), akijaribu moja kati ya matrekta saba aliyowakabidhi wakulima wa mikoa kadhaa Dar es Salaam leo, kwa ajili ya kutekeleza kilimo kwanza. Matrekta hayo yanakopeshwa kwa wakulima mbalimba nchini na Kampuni ya Kariati Tractor. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Kariati Tractor ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kwadelo, Omary Kariati na kushoto ni Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Edmund Mndolwa.
 
Dotto Mwaibale
WANANCHI wa Kata ya Kwadelo iliyopo Kondoa mkoani Dodoma wamemuomba Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye awasaidie kuwaombea serikali wamegewe kipande cha ardhi kwenye hifadhi ya Taifa ya Mkongonelo ili wakitumie kwa kilimo.
 
Ombi hilo limetolewa kwa Nape na Diwani wa Kata ya Kwadelo Alhaji Omary Kariati Dar es Salaam jana kwenye hafla fupi ya kukabidhi matrekta saba ambapo Nape alikuwa mgeni rasmi.
 
" Mheshimiwa pamoja na jitihada hizo zote za kamapuni yangu ya Kariati Tractor kuwawezesha wananchi wa kata yangu kuwakopesha matrekta changamoto kubwa tuliyonayo ni ukosefu wa ardhi iliyochukuliwa na serikali kwa ajili ya hifadhi ya Taifa ya Mkongonelo tunakuomba utusaidie kutuombea Wizara ya Maliasili na Utalii watukatie kipande cha kilomita mbili katika hifadhi hiyo kitumike kwa kilimo" alisema Kariati.
 
Kariati alisema baada ya kupimwa kwa eneo hilo maeneo yote yaliyokuwa yakitumika kwa kilimo yamechukuliwa na serikali jambo lililosababisha wananchi kukosa mashamba.
 
Akijibu ombi hilo Nape alisema atalipeka ombi hilo serikalini ili kuona namna watakavyosaidia na kuwa maeneo mengi ya hifadhi za taifa yalipimwa kwenye miaka 1975 wakati idadi ya watu ilikuwa ndogo ukilinganisha na sasa.
 
"Wakati yanapimwa maeneo haya idadi ya watu ilikuwa kidogo lakini sasa idadi imekuwa ni kubwa hivyo ni vema serikali ikaangalia mahitaji ya matumizi ya ardhi hiyo kwa wananchi na kutenga mengine kwa ajili ya hifadhi" alisema Nape
 
Alisema mwenye uwezo wa kumaliza suala hilo ni Serikali ya CCM ambayo imeshika dola na kuwa moja ya ilani ya chama hicho ni kutekeleza kilimo kwanza kinachofanywa na diwani huyo na washirika wake.
 
Nape alimpongeza diwani huyo na Mjumbe wa Halmshauri Kuu ya Taifa (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk.Edmund Mndolwa kwa kutekeleza ilani hiyo kwa vitendo kwa kununua ekari 100 kwa ajili ya kilimo ambapo alisema angependa wajumbe wengine kuiga mfano huo ambao ni ilani ya chama.
 
Diwani Kariati alisema kuwa matreka hayo saba yaliyokabidhiwa kwa wakulima wa kutoka mikoa mbalimbali yanafikisha  idadi ya matrekta 100 yaliyokopeshwa kwa wakulima mbalimbali nchini na kuwa mmoja wa watu walionufaika nayo ni walimu wanne akiwepo Mwalimu Hamza Haji wa Shule ya Msingi ya Kwadelo.
Kariati alitoa mwito kwa walimu nchini kujitokeza kwa wingi kukopa matrekta hayo ili kuinua uchumi wao na hivyo kuondoa dhana potofu ya kuogopa kwenda kufanya kazi vijijjini kwa madai ya kuwa na maisha magumu wakati wenzao wamepiga hatua ya maisha.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate