EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, February 6, 2015

MTOTO WA FLORA MBASHA AIBUA MAZITO



Stori:MWandishi wetu
HAKUNA dogo! Siku tano zimekatika baada ya mwimba Injili nyota nchini, Flora Henry Mayalla Mbasha kujifungua mtoto wa kike huku kichanga hicho kikiibua mazito kwenye mitandao ya kijamii, Ijumaa ‘Kubwa’ linakupa zaidi.
Kwa mujibu wa chanzo, Flora alijifungua mtoto wa kike kwa njia ya upasuaji Jumanne iliyopita kwenye hospitali moja iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mwimba Injili nyota nchini, Flora Henry Mayalla Mbasha akiwa na mtoto wake wa kike baada ya kujifungua.
MSHTUKO KWANZA
Baadhi ya mitandao ya kijamii ilitundika picha ya Flora akiwa kitandani hospitalini na kichanga chake huku watu wakitupia maneno yenye kuonesha mshtuko, kama vile:
“He! Kwani Flora alikuwa na mimba? Mbona alikuwa kawaida sana?”
“Wanawake wengine wameumbwa hivyo, matumbo yao hayawi makubwa. Nampa hongera kwa kujifungua.”
“He! Jamani! Dada Flora kajifungua kweli au ni igizo? Maana isijekuwa sinema halafu tukampa hongera za bure tu.”
Mtoto anayedaiwa kuibuwa mazito.
‘UTABIRI’ WAANZA
Kama ilivyo kawaida kwa baadhi ya mitandao ya kijamii Bongo. Kusema chochote bila kusikia kauli ya mhusika, baadhi ya mitandao ikaanza kupitisha mitazamo kwamba, mtoto huyo amefanana na Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima.

Flora Mbasha akiwa na mumewe Emmanuel Mbasha kwenye pozi la kimahaba.
KIGEZO
Kigezo walichotumia watu hao ni ule mgogoro kati ya Flora Mbasha na mumewe, Emmanuel Mbasha miezi saba iliyopita ambapo Flora aliondoka kwa mumewe, Tabata na kudaiwa kuishi kwa Gwajima.

MPAKA PICHA
Baadhi ya mitandao ilipitiliza kwa kutundika picha ya Gwajima akiwa ameshika kipaza sauti sanjari na ya mtoto huyo akiwa ndani ya ‘bebi shoo’.

Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Uzima na Ufufuo la jijini Dar, Josephat  Gwajima.
IJUMAA LAZUNGUMZA NA FLORA
Baada ya kutokea kwa hali hiyo ndani ya mitandao, Ijumaa lilimsaka Flora kwa njia ya simu ili kujua ukweli wa yeye kujifungua mtoto na pia kumtaja baba wa mtoto.
Ijumaa: “Mambo Flora? Hongera kwa kujifungua.”
Flora: “Asante sana.”
Ijumaa: “Kumbe umejifungua bwana!”
Flora: ”Mbona umechelewa kujua!”
Ijumaa: “Mtoto gani?”
Flora: “Wa kike.”

MBASHA APIGA CHENGA
Ijumaa liliamua kumuuliza Flora kama mumewe, Mbasha ameshafika kumuona mtoto huyo.
Ijumaa: “Oke! Mungu amtunze na kumsimamia katika afya njema. Vipi baba yake (Emmanuel) ameshakuja kumuona?”
Flora: “Hajaja. Lakini it’s ok! Maana Mungu mwenyewe atamlea.”

MADAI ETI NI WA GWAJIMA
Ijumaa: “Sasa baadhi ya watu wameanza kusemasema eti ni mtoto wa Gwajima. Watu bwana!”
Flora: “Acha tu waseme lakini uzuri mtoto kamfanana baba yake (Emmanuel) kwa kila kitu. Wanaosema kuhusu Gwajima wana lao jambo na hawajui walisemalo.”
Mwimba Injili Bongo, Flora Mbasha.
ANENA MAZITO
Ijumaa: “Nashukuru sana Flora.”
Flora: “Asante na wewe, lakini narudia tena, wanaosema ni mtoto wa Gwajima Mungu na awabariki tu maana mimi sitishwi na maneno ya wakosaji. Namwangalia Mungu tu aliyeniumba na kunifanya niwe hivi nilivyo leo.
“Isitoshe picha walizoeneza mitandaoni si za mwanangu, so hata sipati shida. Biblia inasema pande zote twadhikika bali hatusongwi, twaona shaka bali hatukati tamaa, twaudhiwa bali hatuachwi, twatupwa chini bali hatuangamizwi.
“Kwa hiyo hatulegei bali ijapokuwa utu wetu wa nje umechakaa lakini ndani wafanywa upya siku kwa siku.”

KUMBE PICHA SI ZA MTOTO WAKE
Flora alisema anachomshukuru Mungu picha zilizosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimwonesha mtoto kama wa siku kumi si za mtoto wake.
Flora: “Kwanza hiyo picha iliyosambaa kwenye mitandao namshukuru Mungu si ya mtoto wangu. Mimi nimeshawasamehe wote walio kinyume na mimi na wale wasioujua ukweli lakini wanasambaza taarifa.”
Ijumaa: “Asante sana Flora.”
Flora: “Nashukuru sana.”

MBASHA HAPOKEI SIMU, SI KAWAIDA YAKE
Baada ya kumaliza kuwasiliana na Flora, Ijumaa lilimpigia simu Emmanuel Mbasha ili kumsikia anasemaje kuhusu ujio wa mtoto huyo hasa ikizingatiwa kwamba, mkewe aliondoka nyumbani kwa muda mrefu.
Simu ya Mbasha iliita bila kupokelewa hata ilipopigwa mara kadhaa jambo ambalo si kawaida yake. Hata pale alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno, Mbasha hakujibu kitu!
 
GWAJIMA KAMA MBASHA TU
Baada ya ukimya wa Mbasha, Ijumaa lilimtafuta Gwajima kwa njia ya simu yake ya mkononi, naye iliita kwa mara kadhaa bila kupokelewa. Lengo la kumtafuta Gwajina ni kutaka kumsikia anasemaje juu ya madai ya watu mtandaoni kudai mtoto ni wake na nini  kauli yake dhidi ya watu hao.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate