EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 9, 2015

WAMASAI WATAKA UWEKEZAJI KUSITISHWA NGORONGORO


DSC_0200

Kiongozi wa mila tarafa ya Ngorongoro, Augustino Pakai Olonyokei akizungumza na Meneja uendeshaji wa mtandao wa habari wamodewjiblog, Zainul Mzige aliyefika eneo hilo kwa ajili ya kuangalia miradi mbalimbali inayoendeshwa kusaidia jamii ya wafugaji wa kimasai hivi karibuni.
Na Mwandishi wetu, Ngorongoro
KIONGOZI wa mila tarafa ya Ngorongoro Augustino Pakai Olonyokei ameitaka serikali kusimamisha uwekezaji katika Mamlaka ya Ngorongoro ili kupunguza shinikizo la raslimali katika eneo hilo.
Alisema kuendelea kuwekeza katika mahoteli,makambi ya watalii, miundombinu katika hali ilivyo sasa ni kuzidisha migogoro iliyopo kati ya wakazi wa eneo hilo na mamlaka ambayo tayari ipo.
Olonyokei alisema hayo hivi karibuni wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ambaye alifika eneo hilo kwa ajili ya kuangalia miradi mbalimbali inayoendeshwa kusaidia jamii ya wafugaji wa kimasai.

Alisema hali ya sasa ni ngumu na inayosikitisha hasa kutokana na sheria iliyoanzisha mamlaka ya Ngorongoro kuwanyang’anya umiliki wa eneo ambalo wao wamelilinda miaka yote ndiyo maana wanyama wanapatikana na utalii unakuwepo.
Aidha alisema mabadiliko ya hali ya hewa yanafanya mazingira yao kuwa magumu , wanakuwa na njaa huku wakiwa wamekatazwa kulima hata eneo dogo.
“Tuna changamoto nyingi…hatuna ajira, ushiriki wetu katika bodi ni mdogo na baraza la wafugaji linapewa hela kidogo katika mazingira ya kuwa na miradi mingi,” alisema Olonyokei.
Alisema Baraza hilo kupewa sh bilioni moja tu haitoshi wakati utalii ukiingiza mabilioni ya fedha.
Pamoja na kuelezea changamoto hizo na kuitaka serikali kuzuia kuongezeka kwa shughuli zaidi katika eneo hilo, aliwataka watanzania kujua mazingira ya jamii ya wafugaji na adha wanazokutana nazo.
Hata hivyo Mhifadhi wa mamlaka ya Ngorongoro Dk. Freddy Manongi amesema kwamba pamoja na malalamiko hayo, mamlaka hiyo iliyoanzishwa mwaka 1959 kwa ajili ya kutoa huduma kwa jamii, utalii na kuhifadhi mazingira mwaka jana pekee ilitumia sh bilioni 60.
Fedha hizo ni kwa ajili ya kuhifadhi, kuendeleza jamii na utalii.
Alisema msaada mkubwa wanaoufanya ni katika sekta ya elimu ambapo imejenga shule 21 na kila mwanafunzi anayekwenda sekondari kutoka katika eneo hilo hupatiwa udhamini wa masomo.
Aidha alisema kutokana na wananchi kuzuiwa kulima, huwapatia mahindi kwa ajili ya chakula na ingawa kunatakiwa kuangaliwa namna bora zaidi endelevu ya wananchi kupata chakula lakini kwa sasa hilo ndilo wanalofanya.
DSC_0041
Mhifadhi wa mamlaka ya Ngorongoro, Dk. Freddy Manongi katika mahojiano maalum na Meneja uendeshaji wa mtandao wa habari wamodewjiblog, Zainul Mzige (hayupo pichani).
“Mahindi ya bure yanapokosekana anagalau yawepo ya kununua kwa bei ya chini, na tunauza kwa shilingi 5000 kwa debe” alisema.
Dk. Manongi alisema pia kwamba fedha nyingine zinatumika katika sekta ya afya na pia kuboresha hali ya mifugo kwa kuwezesha uharamishaji mifugo na kujenga majosho.
Alisema ongezeko kubwa la watu katika eneo ambalo haliongezeki ni dhahiri linaleta migongano lakini mamlaka hiyo inafanya shughuli zake kwa kushirikiana na Baraza la wafugaji ili kupunguza migongano.
Wakati mamlaka inaanzishwa 1959 eneo hilo lilikuwa na wakazi 8,000 baada ya wengine 4000 kuhamishiwa hapo kutoka Serengeti. Kwa sasa eneo hilo lina watu takaribani 90,000 katika eneo lilelile la kilomita za mraba 8,262.
Alisema baraza hupewa sh bilioni 2 kwa mwaka wakati shughuli nyingine za maendeleo zinazofanywa na Mamlaka hugharimu sh bilioni 11.
Kuhusu changamoto za elimu amesema kwa mwaka jana hali haikuwa njema kwa ufaulu lakini sasa wametafuta sababu na kuanza kuhakikisha kwamba walimu wanapewa motisha na pia wanafunzi wanapata mlo wa mchana ili kuwafanya wasitoroke.
Kuhusu suala la ajira Dk. Manongi amesema ni tatizo la tafsiri tu lakini kila nafasi zinazpopatikana hujitahidi kuajiri watu kutoka katika eneo hilo.
Alisema kuna mambo mengi yanayofanywa kuimarisha eneo hilo kuendeleza jamii na kuendeleza hifadhi ili kuwezesha utalii ambao ndio unatoa fedha kwa ajili ya mambo yote.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate