EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, February 9, 2015

NGASSA IS BACK AFANYA VITUADIMU


Wachezaji wa Yanga wakishangilia goli.
Sweetbert Lukonge, Hans Mloli na Wilbert Moland
BEKI na nahodha Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, jana alitoa kauli ambayo inaweza kuwa shangwe kubwa kwa mashabiki wa timu yake baada ya kusema kuwa ‘anayejua anajua tu’, ikiwa ni muda mfupi baada ya kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Mtibwa Sugar.
Cannavaro alitoa kauli hiyo baada ya kushuhudiwa kiungo mshambuliaji wa timu yake Mrisho Ngassa akifunga mabao mawili na kuthibitisha kuwa kiwango chake hakijafikia tamati kama wengi walivyokuwa wakisema awali.

Ngassa aliondoka katika Uwanja wa Taifa akiwa shujaa kutokana na kufunga mabao mazuri katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara dhidi ya wabishi hao wa Morogoro ambao walishindwa kabisa kujibu mapigo na kujikuta wakipata kipigo chao cha pili msimu huu.
Mabao ya Ngassa ambaye aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Kpah Sherman huku mashabiki wake wakiimba Ngassa is back, yaani Ngassa amerudi, yameiwezesha Yanga kufikisha pointi 25 na kuwa kinara katika Ligi Kuu Bara ikifuatiwa na Azam FC yenye pointi 22.
Akizungumzia mechi hiyo, Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm ambaye alionekana kuwa na furaha, alimsifia Ngassa kwa kuonyesha uwezo mzuri lakini akasema nyasi za uwanjani zilikuwa zikipoozesha baadhi ya matukio kutokana na mpira kutokwenda kwa kasi inayotakiwa.
Upande wa Kocha wa Mtibwa, Mecky Maxime, alisema: “Nimekubali matokeo, hakuna mchezaji wa kumlaumu, tunajipanga kwa mechi ijayo.”Ngassa ambaye alifunga mabao katika dakika ya 56 na 63 alisifiwa na kocha wake ambaye alisema anakubali kiwango chake na ndiyo maana kazi aliyomtuma aliitekeleza inavyotakiwa.
Ngassa alionekana kuleta mabadiliko muda mfupi tu baada ya kuingia akichukua nafasi ya Sherman ambaye inaonekana mpira wa Bongo umeanza kumshinda, kwani katika michezo sita ya ligi aliyocheza, hajafunga bao lolote.
Kuhusu mechi hiyo, Ngassa alifunguka: “Naamini uwezo wangu, sikuwa sawa kutokana na matatizo ya nje ya uwanja ambayo bado hayajaisha.“Matatizo ya madeni na kutolipwa mshahara kwa miezi miwili sasa, vilichangia nisiwe sawa kisaikolojia, kama nilivyosema nitapambana kuipa mafanikio timu yangu katika muda huu mfupi uliosalia wa mkataba wangu.
“Kocha aliniambia nikacheze katikati kwa kuwa mabeki wa Mtibwa ni wazito, hivyo niwaache (Simon) Msuva na (Andrey) Coutinho wawakimbize pembeni kisha mimi niingie katikati, kweli maelezo yake yakazaa matunda.”
Katika mechi hiyo washambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe na Sherman walikosa nafasi nyingi za wazi, kama timu hiyo isingepata ushindi basi hali ingekuwa tete kwao hasa kwa kuwa mashabiki wao walionekana kukerwa na hali hiyo.
Mashabiki wamvaa Ngassa
Mara baada ya mechi hiyo mashabiki wengi wa Yanga walimzunguka Ngassa ambapo walikuwa wakimpongeza huku wakipigana vikumbo katika kutaka kupiga naye picha.
Ngassa alienda kwenye gari ya Msuva aina ya Toyota Altezza akiwa na Msuva na Tegete ambaye ndiye aliyeendesha gari hilo kutoka uwanjani hapo huku umati wa mashabiki ukiwashangilia kwa nguvu.

Katika hatua nyingine, Msemaji wa Mtibwa ambaye alikuwa na tambo nyingi kabla ya mechi hiyo, Thobias Kifaru, alipotafutwa, alipozungumza alionekana kama ameikimbia mechi hiyo kwani alisema: “Sipo Dar, nipo Iringa kikazi.” Kisha akakata simu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate