EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, March 19, 2015

DIAMOND, PENNY MZOZO UPYA

IMEVUJA! Ile mimba ya aliyekuwa Mtangazaji wa Efm Radio, Penieli Mungilwa ‘Penny’ ambayo ilijulikana alipachikwa na staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ imezua mzozo upya baada ya kuvuja kwa madai mengine.
Staa wa muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Chanzo makini kimeliambia Amani kwamba, tofauti na madai ya Diamond kwamba Penny alitoa mimba yake, lakini kumbe Diamond hakumpa mimba ila ilikuwa ni magumashi ya Penny.
SIKIA HII
“Hali ilikuwa hivi! Kutokana na Diamond kutafuta mtoto kwa muda mrefu, hasa kwa mpenzi wake wa nyuma Wema Sepetu kushindikana, ikabidi Penny atumie mbinu yake ili kufaidika na pesa za Diamond.
“Penny aliahidiwa na Diamond kwamba, kama atakubali kuzaa naye atamnunulia gari zuri, kwa hiyo kazi ikawa kwa Penny sasa, afanyaje?
“Siku moja Penny alimwambia Diamond kwamba amenasa, Diamond akafurahi sana, lakini kumbe Penny alishaenda kwenye hospitali moja kubwa iliyopo Kinondoni (jina tunalo), akaongea na nesi mmoja kwamba kama atakwenda na Diamond kupima mimba akubali kwamba anayo, lengo lake ni kupata gari,” kilisema chanzo hicho.
Mtangazaji wa Efm Radio, Penieli Mungilwa ‘Penny’ akiwa na aliyekuwa mpenzi wake Nasibu Abdul ‘Diamond’.

IKAZIDI KUDAIWA
Chanzo kikazidi kudai kwamba, ili amridhishe Diamond, Penny alimchukua mpenzi wake huyo hadi kwenye hospitali hiyo na kukutana na yule nesi ambaye alimwambia Diamond kwamba kweli mchumba wake huyo (kwa wakati ule) alikuwa amenasa.“Ndipo Diamond ikabidi amnunulie gari Penny aina ya Toyota Brevs la rangi ya bluu iliyoiva. Siku mbili tatu, akageuka, akamwambia Diamond mimba imetoka, ndiyo kikawa kisa cha kumwagana,” kiliongeza chanzo chetu.
PENNY ASAKWA NA AMANI
Baada ya kupata madai hayo mazito, Amani lilimvutia ‘waya’  Penny  na kumsomea mashtaka yake ambapo alisema kuwa, hafikirii katika kumbukumbu zake kama alishawahi kusema yeye ni mjamzito au alikuwa na mimba ya Diamond kama siyo mwanamuziki huyo kutangaza mwenyewe.
“Hivi jamani! Mimi sijawahi kusema kama nina mimba ya Diamond hata siku moja, sasa hapo hushangai aliyekuwa akisema nina mimba ni Diamond na siyo mimi. Kwanza Diamond hajawahi kunipa mimba hata siku moja, muulizeni aseme ukweli wake. Kama ni gari ni mapenzi yake lakini si zawadi ya mimba,” alisema Penny.
‘Penny’ akiwa na mama Diamond.
DIAMOND NAYE
Kwa upande wake, Diamond alipoulizwa kuhusu madai ya kuingizwa mjini na Penny kuhusu mimba, alikuwa na haya ya kusema:“Mm! Hiyo kali zaidi! Mimi Penny aliponiambia ana mimba yangu, asubuhi nilimkurupua mwenyewe, nikampeleka kwenye hospitali yangu mimi, hakunipeleka yeye.
“Tena hakujua kama nampeleka hospitali gani. Kule daktari wangu akampima, akamuona amenasa kweli. Sasa mnaposema eti alinipeleka kwenye hosptali yake aliyokwishapanga na nesi, nashangaa, siyo kweli bwana.“Yeye kama alifanya hivyo labda alimfanyia mtu mwingine, si mimi. Sasa naona kama kuna mzozo unataka kuibuka upya hapa.”
PENNY, ARUDIWA, HAPOKEI SIMU
Jumatatu iliyopita, Penny akapigiwa simu tena ili kupewa majibu ya Diamond, lakini simu yake iliita kwa muda mrefu bila kupokelewa. Lakini Amani linaendelea kumfuatilia ili kumsikia atasema nini kuhusu majibu ya Diamond.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate