EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 24, 2015

HAYA NDIYO MAAJABU YAKE MTOTO ALIYENUSURIKA KWA MKONO WA MUNGU


Na Haruni Sanchawa
MTOTO Jacqueline Lepenza, aliyenusurika katika ajali mbaya ya basi lililogongana na lori huko Mafinga mkoani Iringa wiki mbili zilizopita, ameripotiwa kuwa na maajabu baada ya baba yake mzazi kujitokeza na kusimulia, Uwazi linakutaarifu.
Jacqueline Lepenza, akiwa na baba'ke.
Willy Lupenza, baba mzazi wa mtoto huyo mwenye umri wa miaka mitatu na nusu, alisema marehemu mke wake, Anjela Osward (35) (pichani) alikuwa amekwenda nyumbani kwao Ilembula mkoani Njombe kwa ajili ya ubatizo wa binti yao huyo.
Alisema katika hali ya kushangaza, siku ya ubatizo huo, Jacqueline alibatizwa peke yake pasipo watoto wenzake kupewa baraka hizo kwa sababu ambazo hazikueleweka.“Ndugu mwandishi, hili ni tukio ambalo sitalisahau katika maisha yangu, kwa sababu haiwezekani mtoto abatizwe peke yake halafu kwenye ajali, idadi kubwa ya watu wapoteze maisha lakini yeye anusurike.”
Alisema baada ya ajali, mtoto wake huyo alikutwa na watu waliojitokeza kuwasaidia majeruhi akiwa amelala juu ya bati la kuzuia matope kwenye tairi ya lori lililokuwa limebeba kontena huku akilia na matairi yakiendelea kuzunguka.
Alisema haelewi mtoto huyo alitokaje ndani ya basi hadi kwenye bati hilo la lori, kwani licha ya kukutwa mzima, lakini eneo hilo pia lilikuwa hatarishi kwa mwanaye ambaye alimpoteza mama yake aliyekuwa mmoja kati ya watu zaidi ya 50 waliofariki dunia.

...Akiwa na bibi yake.
Willy alisema Machi 11, mwaka huu alipata taarifa kwa njia ya simu kutoka kwa shemeji yake ambaye yuko mkoani Iringa kwa shughuli zake za kibiashara juu ya tukio hilo, baada ya yeye naye kuarifiwa na Jeshi la Polisi Iringa baada ya kuokotwa kwa simu ya mkewe.
Alisema baada ya kupigiwa na polisi waliofika katika eneo la tukio mapema, shemeji yake huyo alimpigia na kumjulisha juu ya mkewe kupata matatizo Mafinga.“Nilianza safari mara moja kuelekea huko, lakini nilipofika Morogoro nilipata taarifa za uhakika zilizoniaminisha kuwa mke wangu alikuwa amefariki dunia,” alisema.
Aliongeza kuwa aliendelea kufanya mawasiliano na ndugu kujua alipo mtoto, hadi alipoambiwa kuwa kulikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa wodini (Hospitali ya Wilaya Mafinga), hivyo akaambiwa kama anaweza kuwatumia picha yake kwa njia ya mtandao ili waweze kumfananisha.
“Niliwatumia picha kwa Mtandao wa WhatsApp, kumbe siku ya ajali mwanangu alikuwa amevaa gauni ambalo aliwahi kulivaa siku za nyuma, na ndiyo picha niliyowatumia, walimtambua kirahisi na alipofanyiwa uchunguzi wa kidaktari ikagundulika kuwa hakuwa na matatizo yoyote kiafya,” alisema baba huyo.
Mamam wa Jacqueline, Anjela Osward enzi za uhai wake.
Kufuatia kufika Mafinga na kuutambua mwili wa mke wake, aliomba mwili huo kutopelekwa sehemu yoyote ili urudishwe nyumbani kwao Ilembula kwa mazishi yaliyofanyika katika Kijiji cha Mwambaga.Kuhusu hali ya mtoto kwa sasa, Willy alisema anaendelea vizuri na anamshukuru Mungu pamoja na madaktari na polisi walioshiriki katika tukio hilo ambalo mwanaye huyo alipona kimaajabu.
Ajali hiyo ilihusisha lori aina ya Scania namba T 689 APJ mali ya Cipex Company lililokuwa likiendeshwa na Maka Sebastian (26) na basi aina ya Scania namba T 438 CED mali ya Majinja lililokuwa likiendeshwa na Baraka Gabriel (38).

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate