EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 24, 2015

MUME ALIVYOMFANYIA UKATILI MKEWE

HUU ni ukatili uliopitiliza! Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Neema Mwita, anateseka katika Hospitali ya Mkoa wa Mara kufuatia jereha kubwa alilopata baada ya mumewe aliyemtaja kwa jina la Juma Mwita kummwagia uji wa moto kisa kikiwa ni kuchuma mahindi shambani bila ridhaa ya mumewe huyo.Akizungumza na Uwazi huku akimwaga machozi kila wakati, mwanamke huyo alisema siku ya tukio, yeye na mumewe walikuwa kazini na mwanaume huyo ambaye alipata tenda kubwa ya kufyatua matofali.
Neema Mwita akihojiwa.
MSIKIE MWENYEWE
“Nilikuwa nakusanya majani. Baada ya kukusanya kwa muda mrefu ambapo niliagizwa na mume wangu, niliamua kwenda shambani kuchuma mahindi kisha nikarudi nyumbani kupika chakula cha mchana ili akitoka kazini ale.
“Nikiwa jikoni nasubiri uji uchemke ili nisonge ugali, mume wangu alirudi ghafla na kuanza kunigombeza eti kwa nini nilichuma mahindi shambani na nilirudi nyumbani bila ridhaa yake?” alisema na kuanza kulia.

MUME ACHUKUA UJI WA UGALI
Mwanamke huyo aliendelea kusema: “Alinihoji ni kazi gani kubwa niliyoifanya kule kwenye matofali mpaka nikaamua kurudi nyumbani. Kabla sijajibu aliifuata sufuria yenye uji unaochemka jikoni na kunimwagia ambapo ulitua kifuani kwangu na kuniunguza vibaya, kama unavyoona. Sijajua mume wangu alikusudia nini kunifanya hivi!”
JIRANI AMWOKOA
Mwanamke huyo aliendelea kusema kuwa, baada ya kumwagiwa uji huo na kuungua, alianguka chini na kulia kwa maumivu, ndipo jirani yake mmoja alimwona akihangaika na kumchukua hadi ndani.
AKAA NYUMBANI SIKU SABA
“Ndani nilikaa kwa wiki nzima, maumivu yalikuwa makali sana. Ndipo wazazi wangu walipopata taarifa wakaja kunichukua. Hata hivyo, wazazi wangu nao hawakunipeleka hospitali, waliniweka nyumbani na kuniletea mganga wa kienyeji.”
Mwandishi akizidi kumuhoji Neema Mwita.
MUME AKIMBILIA KUSIKOJULIKANA
Neema alisema mumewe aliyeoana naye kwa upendo na kiapo cha kuishi katika shida na raha mpaka kufa, alikimbia baada ya tukio hilo na hajawahi kuonekana mpaka sasa ambapo polisi wanaendelea kumsaka usiku na mchana.
TAARIFA ZINAFIKA SERIKALINI
Mwanamke huyo ambaye kutokana na kuungua huko mishipa yake ya sehemu ya kidevuni imeshikana na ya shingo, alisema baada ya wiki moja, taarifa zilimfikia Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyamisanga, Boke Chacha ambaye alimchukua mikononi mwa wazazi hao na kumpeleka hospitali kwa matibabu.
LICHA YA KUUNGUA, AMETELEKEZWA
Neema, anasikitisha sana kwani licha ya kupitia kipindi hicho kigumu, anadai ametelekezwa na wazazi wake  na mtu anayemsaidia ni mwanaye wa kiume anayeitwa Wambura Juma aliyekuwa akisoma kidato cha tano.
“Mtoto wangu huyu kwa sasa hasomi kwa sababu ya kunisaidia mimi, alilazimika kuacha masomo toka tukio hili liliponitokea,” alisema Neema.
ANA MIEZI NANE HOSPITALINI
Neema anasema tangu alazwe hospitalini hapo, sasa ni mwezi wa nane lakini anamshukuru Mungu ameanza kujikongoja kutembea japo kwa taabu sana.

Muonekano wa jeraha alolipata Neema baada ya kuunguzwa na mumewe kwa uji wamoto.
MADHARA ALIYOYAPATA
Neema amepata madhara makubwa kufuatia tukio hilo kwani kwa sasa mkono wa kulia haukunjuki sawasawa kama zamani, hawezi kunyoosha shingo kutokana na nyama za shingo kuungana na kidevu, mdomo wake umepinda kidogo huku titi la upande wa kulia likiwa halipo tena!
APATIWA SIMU YA MKONONI
Joyce Kiria ni Mtangazaji wa Kipindi cha Wanawake Live kinachorushwa hewani na Runinga ya EATV, alimtembelea Neema hospitalini na kumpa msaada wa simu ya mkononi ili iwe rahisi kwa wale watakaojitokeza kutaka kumsaidia kwa ajili ya pesa za matibabu kutumia simu hiyo.
ANAHITAJI MSAADA
Ndugu msomaji, Neema anahitaji msaada wako wa hali na mali. Kama utakuwa na chochote na umeguswa na maumivu yake, unaombwa kutumia mawasiliano yake  0656 151 072 au 0756 768 305.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate