EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, March 7, 2015

MADAI MAZITO: UTAJIRI WA ZARI MAGUMASHI

Mwandishi Wetu
NI madai ya chini kwa chini kutoka vyanzo vilivyo karibu na mwanamuziki nyota nchini Uganda, Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’ ambaye kwa sasa ameshikamana kimapenzi na Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwamba, utajiri anaoutangaza kuwa nao siyo kweli!Mwanamuziki nyota nchini Uganda, Zarina Hassan ‘Zari The Bosslady’.
Madai hayo yalilishangaza Risasi Jumamosi kiasi cha kutaka kusikia kwa kina kwa nini utajiri huo siyo wa kweli wakati Zari anaonekana kwenye mitandao ya kijamii akiwa na mali zake, kama nyumba na magari?

MSIKIE HUYU
“Mimi ndiyo nawaambia. Zari kweli anajiwezaweza lakini si kwa mali anazozitangaza kuwa nazo. Mimi naishi Uganda, namjua vizuri sana Zari,” alisema mtoa habari huyo.
Risasi Jumamosi: “Twende polepole. Ina maana yale magari ambayo kwenye namba za usajili badala ya namba kumeandikwa ZARI GP, ZARI 3 GP, ZARI 1 GP, ZARI H GP na mengineyo mengi si ya kwake?”
Mtoa habari: “Mengine yake, mengine si yake.”
Risasi Jumamosi: “Kwa nini yawe si yake wakati yameandikwa Zari?”
Mtoa habari: “Kuna makampuni ya nje ambayo yakitoa magari yanaingia naye mkataba yeye ili kuyatangaza. Sasa kwenye mkataba Zari anatakiwa kubandika jina lake ili watu wajue staa mkubwa kama Zari naye anatumia magari kama yale.”
Moja kati ya magari ya kifahari anayomiliki.
KUHUSU NYUMBA?
Mtoa habari huyo alisema anavyojua yeye, Zari ana nyumba moja nchini Uganda na nyingine Afrika Kusini ambazo aliachiwa na mumewe wa ndoa, Ivan Ssemwanga wakati wanatengana.
“Ile nyumba alijenga akiwa na mume wake, Ivan, lakini Zari kama Zari hajajenga. Hata sehemu kubwa ya mali zake Zari mumewe ndiyo amefanikisha.”
VIGEZO VYA MADAI
Mtoa habari wetu alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, kwa uhalisia wa magari ya Zari yanaweza kufika ishirini jambo ambalo alisema haoni mantiki yake.“Zari anasema anamiliki shule, vyuo, magari na mahoteli, lakini ili avipate hivyo maana yake amefanya biashara za kumzalishia, si ndiyo? Sasa kwa mfanyabiashara wa kweli anaweza kununua magari ya kutembelea ya kifahari kumi na tano na yuko yeye na watoto wake watatu tu? Tena wadogo.
“Tabia ya mtu kununua kila gari la kifahari linaloingia ni ya wale watoto ambao baba zao ndiyo wenye mali. Lakini kwa mfanyabiashara anayetunza mtaji wake, hawezi kununua kila toleo la gari.
“Kama itatokea hivyo, basi atauza lile gari la mwanzo na kununua jingine. Matajiri wote duniani wana magari ya kifahari ya saizi ya familia. Anaweza kuwa nayo mengi lakini matumizi pia ni hivyohivyo, sasa Zari magari kumi na tano halafu yeye na wanae watatu, wadogo. Mimi nakataa jamani,” alisema mtonyaji huyo.
KUJA KWAKE BONGO
Mtu huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa, kama Zari anamiliki zile Hammer ambazo bei ya chini kabisa moja ni kama shilingi milioni mia mbili, basi hata kuja kwake Bongo kumfuata Diamond, angekuwa na utaratibu huu:
“Kwanza, kwa utajiri anaosema anao, mjue pesa ina tabia ya kusema. Zari angekuwa akitaka kuja Bongo kumfuata Diamond, angekuwa anatanguliza gari lake moja la kifahari likiwa na dereva ambalo angekuwa akilitumia nchini halafu yeye angekuwa anafuata na ndege. “Sasa yeye anakuja na ndege, akifika anategemea kutumia BMW C6 la Diamond. Sidhani kama kwa utajiri anaoutangaza anao angekuwa anafanya hivyo,” alisema mtu huyo.
TURUDI KWENYE MADAI YA ZARI
Katika mahojiano na Kipindi cha The Sporah Show cha mtangazaji Sporah Njau nchini Uingereza,  Zari mwenye maskani yake Kampala na Afrika Kusini, alisema anamiliki ndinga kibao za kifahari zenye thamani kubwa.
MITANDAO YA UGANDA
Mitandao mbalimbali ya nchini Uganda, imebainisha kuwa Zari anamiliki BMW (2006) lenye thamani ya dola 47, 000 (Sh. milioni 75.2), Black Chrysler (2008) dola 16,000 (Sh. milioni 25.6) na Audi Q7 (2010) la dola 53,000 (Sh. milioni 84.8).
Mengine ni Silver Chrysler (2008) la dola 13,000 (Sh. milioni 20.8), Jetta Volkswagen (2006) linalomgharimu dola 27,000 (Sh. milioni 43.2), Mercedes Benz Convertible (2008) linalouzwa dola 26,000 (Sh. milioni 41.6) na Range Rover Sports (2010) lenye thamani ya dola 109,000 (Sh. milioni 174.4).
Pia ana Lamborghini Gallardo (2010) lililomgharimu dola 198,000 (Sh. milioni 316.8), Hummer H2 la dola 150,000 (Sh. milioni 240) na mengine mengi, yote yakiwa na jina lake badala ya namba za usajili.
KWENYE MAHOJIANO NA SPORAH
Zari alisema ana mjengo wa nguvu mjini Cape Town, Afrika Kusini na Apartments (nyumba za kupangisha na kila kitu ndani) jijini Kampala, Uganda.Jarida la Times la nchini Uganda linamtaja Zari kama mwanamke anayekaribia kuingia kwenye orodha ya wanawake matajiri Afrika.
DIAMOND ASHTUKA
Alipotafutwa Diamond na kuambiwa kwamba kuna habari utajiri wa Zari ni magumashi, alishtuka.
“Khaa zimetoka wapi hizo habari? Mbona mimi najua ni mali zake?” alisikika Diamond na kukata simu.
Jitihada za kumpata Zari ili aweze kuzungumzia utajiri wake hazikuzaa matunda kufuatia simu yake kutopatikana hewani. Jitahada zinaendelea.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate